Lissu: Polisi hawana uwezo wa kukaa na Mbowe muda mrefu gerezani. Mbowe na CHADEMA hatutatoa ushirikiano

Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu akiwa katika mtandao wa Kijamii wa “Club House” katika chumba kilichofunguliwa na CHADEMA cha “Mashtaka ya Ugaidi ya Mbowe na Katiba Mpya” amesema CHADEMA haitashiriki katika kesi ya Ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wao, Freeman Mbowe

Amesema “Hatutaandika barua ya kuomba dhamana, wala yeye hataomba. Mwenyekiti hatatoa ushirikiano wa aina yoyote, sio Polisi sio Mahakamani. Waamue wao wanataka kumfanya nini”

Ameongeza, “Wakikaa naye wajue hii kelele itakuwa kubwa. Wamuachie menyewe, wakimuachia kwa masharti ya kurudi Polisi siku nyingine hatarudi. Na wakimuachia atarudi Mwanza kwenye Kongamano”

Amesisitiza, “Kama wanamuachia waamue wenyewe, na wamuachie bila masharti yoyote. Sisi hatutashiriki kwa lolote katika kesi hii tunayojua ni ya kijinga”

Awali, Lissu alieleza kuwa kabla ya Mbowe kwenda Mwanza walizungumza naye na kusema tabia ya Polisi kuwakama, kukaa nao kwa muda na kisha kuwaachia kwa masharti ya kurudi kuripoti Kituo cha Polisi kila mara wamechoka na sasa hawatakubali.
Awali, Lissu alieleza kuwa kabla ya Mbowe kwenda Mwanza walizungumza naye na kusema tabia ya Polisi kuwakama, kukaa nao kwa muda na kisha kuwaachia kwa masharti ya kurudi kuripoti Kituo cha Polisi kila mara wamechoka na sasa hawatakubali.
 
Aliitisha juzi kwenye Twitter vijana wa mwanza waingie ,lakini hata panya hakutokea barabarani.

Walimdharau Sana
Aaah yaani huyu Lissu yeye yuko Ulaya anakula maisha mema sisi tuingie barabarani watuvunje makongoro na ninani atawapa ugali watoto wetu? Watanzania ni watu wa aina yake ki asili si watu wa vurugu hata kama wameonewa linapokuja swala kama hilo huwezi kuona hata mmoja barabarani..... nahisi kuna jambo ambalo viongozi wa vyama pinzani hawajalijua vizuri juu ya mioyo ya watanzania
 
Aaah yaani huyu Lissu yeye yuko Ulaya anakula maisha mema sisi tuingie barabarani watuvunje makongoro na ninani atawapa ugali watoto wetu? Watanzania ni watu wa aina yake ki asili si watu wa vurugu hata kama wameonewa linapokuja swala kama hilo huwezi kuona hata mmoja barabarani..... nahisi kuna jambo ambalo viongozi wa vyama pinzani hawajalijua vizuri juu ya mioyo ya watanzania
Utajua tu utapokazika vizuri
 
Mama ka nchi kamemshinda miezi 4 tu ? Hana maanuzi au ? Anashindwa ashike wapi issue kibao kifua kudogo? 2025 atapita huyu
 
Basi utakuwa uko kwenye System na ndio hujali
Hapana si kwamba sijali na si kwamba kwasababu niko kwenye mfumo, nadhan kinachotusumbua ni hisia binafsi, huyu mama ana miezi 4 tu tangu awe rais wa hili taifa na, kama unafuatilia vizuri sana huyu mama suala la katiba hakukataa bali aliomba apewe muda.... ghafla anaibuka mtu kama yule Mdude tena ameachiwa nadhan kwa huruma ya mama japo kesi yake haikuwa na kichwa wala miguu....anatoa kashfa kwa mtu aliyechagiza kuachiwa kwake...huyu kijana alikosa uungwana kabisa... Nadhani wapinzani wametaka kupima kina cha maji kwanza....hata siku moja sikuwahi kufurahia uminyifu wa haki za binadamu mwenzangu.......
 
Back
Top Bottom