Uchaguzi 2020 Lissu: Nikichaguliwa, ndani ya siku 100 za kwanza masheikh wa Uamsho wataachiwa huru

Jifunzeni uarabuni huko waislamu wanavyouzana kwa marekani, list ni ndefu kuanzia sadam, Osama, Ghadafi na wengine wengi wameuzana na kuuawa

Hawa wa bakwata ukiwapa ubwabwa wanatulia tuliiii kama maji mtungini
 
Mwacheni JPM mashehe walikamatwa na waislamu wenzao na rais wote wawili na Znz na SmT wote ni waislamu sasa leo jumba anaangushiwa JPM mbona Belgium au USA au Uk au Amnesty hatuwaoni kulalamika? Haki za binadamu wapo wapi?
 
Halafu unakuta muislamu anashabikia haya kwa kuwa sehemu ya udhalimu
Sio Waisilamu wote wanaoshabikia CCM 2015 walidanganywa kuhusu Mahakama ya kazi

Safari hii wengi wako ACTwazalendo na kura za Raisi wanazimimina kwa Jemadari Lissu the Greatest
 
Mwacheni JPM mashehe walikamatwa na waislamu wenzao na rais wote wawili na Znz na SmT wote ni waislamu sasa leo jumba anaangushiwa JPM mbona Belgium au USA au Uk au Amnesty hatuwaoni kulalamika? Haki za binadamu wapo wapi?
Hii si habari ya Waislamu au Wakristo.

Hii ni habari ya Watanzania kupata haki.

Ndiyo maana Tundu Lissu Mkristo, lakini anatetea haki za mashehe Waislamu.

Kitu cha muhimu hapa ni haki sawa kwa Watanzania wote.

Umeelewa somo hili?
 
Lissu hapa anatuonyesha, UNAFIKI wa hali ya juu sana. Anakubaliana na wengi tuonao hawa Mashekhe wamedhulumiwa na hawana hatia yoyote. Lakini anasema akipewa ridha na akawa Raisi atachukua muda wa siku 100 au miezi 3, kuwapa UHURU WAO HAO MASHEKHE, kwa nini muda wote huo, na unaamini kuwa hawana hatia, kama anataka kuhakikisha kesi yao, jee hatoweza kuwapa dhamana kwanza na ndani ya wiki mbili ama wakapandishwa kizimbani kwa tuhuma zozote ama kuachiwa huru.

Inawezekana miaka 7 uchunguzi haujakamilika na Lissu pia anahitaji siku 100???????? HUU NI UNAFIKI EXPRESS, AKATAFUTE HOJA NYENGINE, TUNAJUA HAWA MASHEKHE KINA JAMBO HADI VATICAN ITOE RUHUSA HAWATOKI.
 
Sio Waisilamu wote wanaoshabikia CCM 2015 walidanganywa kuhusu Mahakama ya kazi

Safari hii wengi wako ACTwazalendo na kura za Raisi wanazimimina kwa Jemadari Lissu the Greatest
Wapo wanaomshabikia mbaguzi wa dini kwenye teuzi
 
Kwani mwanasiasa kutafuta kura imekatazwa?

Unategemea mwanasiasa asitafute kura? Nini maana ya kampeni?

Kama anataka kusimamia haki na ili asimamie haki anahitaji kura, kutafuta kura ili asimamie haki kuna tatizo gani?
Haki inatafutwa wakati wowote, ni vizuri umekubali kuwa yote hii ni siasa tu sio kwamba linawauma sana hawa mashekh wamefungwa toka wakati wa Kikwete hatukuona watu kuwalilia 2015 tulisikia Babu Seya nikichaguliwa nawaachia na Magufuli akaingia katika siasa hizo chafu akawaachia watu wamehukumiwa sasa 2020 wote wanatumia karata ya uamsho tena.
 
Haki inatafutwa wakati wowote, ni vizuri umekubali kuwa yote hii ni siasa tu sio kwamba linawauma sana hawa mashekh wamefungwa toka wakati wa Kikwete hatukuona watu kuwalilia 2015 tulisikia Babu Seya nikichaguliwa nawaachia na Magufuli akaingia katika siasa hizo chafu akawaachia watu wamehukumiwa sasa 2020 wote wanatumia karata ya uamsho tena.
Ushasema haki inatafutwa wakati wowote, kwani wakati wa uchaguzi si ndani ya huo wakati wowote?

Wapi nimekubali kwamba yote hii ni siasa tu sio kwamba linawauma sana?

Siasa ni nini?

Unajua kusoma kwa ufahamu?
 
kwa nini kila uchaguzi wanasiasa wanatumia Mashek wa uamsho kama kete ya kutaka kura? kama hao mashee wana haki kwa nini hawapewi lkn ktk kila kipindi cha uchaguzi utasikiaa wagombea wana watumia kama kete....halafu uchaguzi ukiisha hakuna atakaye wazungumzia!! Lowasa aliiahidi hivyo hivyo ktk uchaguzi wa mwaka 2015 Lisu naye tena mwaka huu 2020...kuna jambo la kutafakari
Upizani ulishakufa tangu kipind cha Dr slaa, saiv tuna upigaji... Hawana sera nyingne
 
Lissu amewauliza waislam wa nchi hii kwa nini hawapazi sauti kuhusu unyama wanaofanyiwa waislam wenzao? Hapo hapo akawaomba watumie kura yao vizuri katika uchaguzi huu ili ndugu zao waweze kuachiwa huru.
Kauli hii moja kwa moja inaonyesha nia iliyojificha ya Lissu ya kuhakikisha Tanzania inaingia kwenye mgogoro na vurugu ili wale wanaodhaniwa kumtuma watimize azma yao ya kuitokomeza Tanzania kama alivyowahi kuahidi Lissu mwenyewe. Katika suala hili, Lissu alitakiwa kutumia lugha unganishi kwa watanzania badala ya lugha farakanishi aliyoitumia. Kutaja kuwa watanzania wa dini fulani ndiyo wahusike kufuatilia suala la namna hii inaonyesha wazi Lissu ana nia ovu dhidi ya Watanzania. Kwa hili lazima Lissu aadhibiwe kwa kunyimwa kura katika ifikapo tarehe 28/10/2020.
 
View attachment 1602807

Mgombea urais Tundu Lissu ameendelea kusisitiza na kumtaka Rais Magufuli awaachie mara moja mashekhe wa Uamsho na mahabusu wengine waliofungwa kwa hila.

Tundu Lissu ameahidi ndani ya siku 100 za kwanza atakapo ingia madarakani ataawachia mashekhe wa Uamsho kwani kesi yao haina msingi wowote.

Lissu amewauliza waislam wa nchi hii kwa nini hawapazi sauti kuhusu unyama wanaofanyiwa waislam wenzao? Hapo hapo akawaomba watumie kura yao vizuri katika uchaguzi huu ili ndugu zao waweze kuachiwa huru.

Tundu Lissu ameshangaa iweje mashekhe hao wasipelekwe mahakamani kama kweli wana kesi ya kujibu ili mahakama iweze kuamua kama wamevunja sheria ama lah.
Lowasa alisema haya haya
 
Kasema specific mashekh wa uamsho na wengine sasa nauliza hao wengine kina nani na anawajuaje hao wengine huko tunaelekea kulekule kwa kina Babu Seya. hii ni kutafuta points tu ila kama asingetaja kikundi chochote na kuongelea kiujumla system yote ya watu kukamatwa bila kufungulia kesi halafu ndio angechambua ni kina nani na nani.
Yani ulitaka Tundu Lissu aseme "Mimi natetea haki za mashehe wa uamsho tu, sitetei haki za Watanzania wengine wowote"?

Au ulitaka Tundu Lissu asitaje kesi ya uamsho kama mfano?

Wapi imekatazwa kutoa mfano wa kesi katika kampeni?
 
Back
Top Bottom