Uchaguzi 2020 Lissu: Nikichaguliwa, ndani ya siku 100 za kwanza masheikh wa Uamsho wataachiwa huru

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
48,771
102,124
121653778_2898621913571857_6471276036883440628_o.jpg


Mgombea urais Tundu Lissu ameendelea kusisitiza na kumtaka Rais Magufuli awaachie mara moja mashekhe wa Uamsho na mahabusu wengine waliofungwa kwa hila.

Tundu Lissu ameahidi ndani ya siku 100 za kwanza atakapo ingia madarakani ataawachia mashekhe wa Uamsho kwani kesi yao haina msingi wowote.

Lissu amewauliza waislam wa nchi hii kwa nini hawapazi sauti kuhusu unyama wanaofanyiwa waislam wenzao? Hapo hapo akawaomba watumie kura yao vizuri katika uchaguzi huu ili ndugu zao waweze kuachiwa huru.

Tundu Lissu ameshangaa iweje mashekhe hao wasipelekwe mahakamani kama kweli wana kesi ya kujibu ili mahakama iweze kuamua kama wamevunja sheria ama lah.
 
Kwa nini kila uchaguzi wanasiasa wanatumia Mashek wa uamsho kama kete ya kutaka kura? kama hao mashee wana haki kwa nini hawapewi lkn ktk kila kipindi cha uchaguzi utasikiaa wagombea wana watumia kama kete....halafu uchaguzi ukiisha hakuna atakaye wazungumzia!! Lowasa aliiahidi hivyo hivyo ktk uchaguzi wa mwaka 2015 Lisu naye tena mwaka huu 2020...kuna jambo la kutafakari
 
Mimi muumini wa sheria na kisheria walitakiwa wafunguliwe mashtaka hukumu itolewe ila kuwafunga watu miaka bila kesi hilo tatizo kubwa lakini nataka niende mbali kidogo tusitumie hii issue kisiasa zaidi kupatia kura ila iwe ni kwa wote ambao kwa sababu moja au nyingine wako ndani au mahabusu bila kuhukumiwa kinyume sheria wafanyiwe haki.

Hapa angesema siku 100 za mwanzo nitahakikisha mahakama inasimama kama huru na sheria za kesi zinafuatwa maana sheria ziko na makosa yote kuwa na dhamana na sheria za dhamana ziko haki itendeke kwa wote.
 
Wana haki ndo maana hawapewi HAKI YAO.
kwa nini kila uchaguzi wanasiasa wanatumia Mashek wa uamsho kama kete ya kutaka kura? kama hao mashee wana haki kwa nini hawapewi lkn ktk kila kipindi cha uchaguzi utasikiaa wagombea wana watumia kama kete....halafu uchaguzi ukiisha hakuna atakaye wazungumzia!! Lowasa aliiahidi hivyo hivyo ktk uchaguzi wa mwaka 2015 Lisu naye tena mwaka huu 2020...kuna jambo la kutafakari
 
kwa nini kila uchaguzi wanasiasa wanatumia Mashek wa uamsho kama kete ya kutaka kura? kama hao mashee wana haki kwa nini hawapewi lkn ktk kila kipindi cha uchaguzi utasikiaa wagombea wana watumia kama kete....halafu uchaguzi ukiisha hakuna atakaye wazungumzia!! Lowasa aliiahidi hivyo hivyo ktk uchaguzi wa mwaka 2015 Lisu naye tena mwaka huu 2020...kuna jambo la kutafakari
kana kwamba hujui kama Magu alizuia siasa tangu alipoingia madarakani na kuleta sheria kandamizi za kuzuia kuongea. Haitoshi baada ya Magu kuingia madarakani Lowasa alichikonoa hili, Magufuli akasema hatasita kumchapa bila kujali mwendo wake.
 
Mimi muumini wa sheria na kisheria walitakiwa wafunguliwe mashtaka hukumu itolewe ila kuwafunga watu miaka bila kesi hilo tatizo kubwa lakini nataka niende mbali kidogo tusitumie hii issue kisiasa zaidi kupatia kura ila iwe ni kwa wote ambao kwa sababu moja au nyingine wako ndani au mahabusu bila kuhukumiwa kinyume sheria wafanyiwe haki. Hapa angesema siku 100 za mwanzo nitahakikisha mahakama inasimama kama huru na sheria za kesi zinafuatwa maana sheria ziko na makosa yote kuwa na dhamana na sheria za dhamana ziko haki itendeke kwa wote.
Kuwaweka watu detention hasa ukijua wanaweza kukughasi katika 'uovu' wako ni kawaida ya madikteta wote.
 
Ila anavyowataja Waislamu kama specific group linaloonewa hapo hayuko sawa naona kama kuna Udini ndani yake, anataka kura za huruma kutoka Dini hiyo
 
54 Reactions
Reply
Back
Top Bottom