REALITY
JF-Expert Member
- Jul 2, 2014
- 4,297
- 1,828
1.lissu amesema kuhusu ushoga hiyo ni faragha ya mtu binafsi,na katiba ya Tanzania imesema ni mwiko serikali kuingilia faragha ya mtu binafsi,na pia utafatiliaje mambo ya mtu binafsi kitandani nyumbani kwake,akasema makonda alivyosema mbona magufuli na maige walijitoa na kusema sio maneno yetu hayo ni ya makonda pekeyake baada ya misaada kuzuiwa.
2.kuhusu mabeberu,lissu anauliza mabeberu ni watu wa aina gani,je ni wale ambao mmenunua ndege kwao,wale ambao mkiumwa mnaenda kutibiwa kwao,wale ambao wanawapa misaada ya dawa,wale ambao wanawafundisha askari wenu counter terrorism ambao ni FBI Marekani,au ni ambao wanawauzia silaha,wale ambao wanatoa misaada ya elimu na mikopo au wale waliomfundisha shule nyerere,marehemu mkapa au mimi tupate elimu au ni wapi?anasema anataka magufuli aseme mabeberu ni wakina nani na ni nchi ipi.
3.kuhusu act wazalendo kushirikiana na chadema amesema lipo wazi na hawawezi sema updates maana mitego ni mingi sana kwao,kwa kifupi kutoa siri watakuwa ni wajinga kiasi gani.
4.kuhusu kesi amesema kama walisimamisha kesi miaka mitatu watashindwaje kusogeza miezi miwili mbele ili jambo la kikatiba linalotokea maramoja ndani ya miaka mitano likamilike kikamilifu.
5.Dunia nzima inaangalia huu uchaguzi kwelikweli,na macho yapo kwa IGP,NEC,JAJI MKUU,MSAJILI WA VYAMA NA USALAMA.
6.Akiingia madarakani kutakuwa na uhuru wa vyombo vya habari,katiba mpya,haki ya mfanyabiashara,kutibiwa kwanza malipo baadae,kuwatoa jela wote ambao wamebambikiziwa kesi,kufutilia mbali vitambulisho vya mmachinga,uhuru wa maoni,kufuta sheria kandamizi na mwisho mihimili kujitegemea,mengine SUBIRIENI KAMPENI
ASANTENI.
2.kuhusu mabeberu,lissu anauliza mabeberu ni watu wa aina gani,je ni wale ambao mmenunua ndege kwao,wale ambao mkiumwa mnaenda kutibiwa kwao,wale ambao wanawapa misaada ya dawa,wale ambao wanawafundisha askari wenu counter terrorism ambao ni FBI Marekani,au ni ambao wanawauzia silaha,wale ambao wanatoa misaada ya elimu na mikopo au wale waliomfundisha shule nyerere,marehemu mkapa au mimi tupate elimu au ni wapi?anasema anataka magufuli aseme mabeberu ni wakina nani na ni nchi ipi.
3.kuhusu act wazalendo kushirikiana na chadema amesema lipo wazi na hawawezi sema updates maana mitego ni mingi sana kwao,kwa kifupi kutoa siri watakuwa ni wajinga kiasi gani.
4.kuhusu kesi amesema kama walisimamisha kesi miaka mitatu watashindwaje kusogeza miezi miwili mbele ili jambo la kikatiba linalotokea maramoja ndani ya miaka mitano likamilike kikamilifu.
5.Dunia nzima inaangalia huu uchaguzi kwelikweli,na macho yapo kwa IGP,NEC,JAJI MKUU,MSAJILI WA VYAMA NA USALAMA.
6.Akiingia madarakani kutakuwa na uhuru wa vyombo vya habari,katiba mpya,haki ya mfanyabiashara,kutibiwa kwanza malipo baadae,kuwatoa jela wote ambao wamebambikiziwa kesi,kufutilia mbali vitambulisho vya mmachinga,uhuru wa maoni,kufuta sheria kandamizi na mwisho mihimili kujitegemea,mengine SUBIRIENI KAMPENI
ASANTENI.