martini enock
JF-Expert Member
- Jul 31, 2015
- 634
- 271
Kaimu jaji mkuu jina kaandika kwa pencel akizingua linafutwa fasta.
Kaimu jaji mkuu jina kaandika kwa pencel akizingua linafutwa fasta.
Ana waanhusha nini ?Mrema anatuangusha wachaga dah!! Tulipasa kumwacha apumzike maana akili pia huchoka jameni. Pole mzee wetu Kiraracha oldboy
We ungerudisha hiyo posho au unataka tuuwane kisukari,?Mrema aburuzwe mahakamani ili uteuzi wake utenguliwe na arudishe posho zote alizowahi kupokea
Nimesoma maandiko mahali ,anamshukuru raisi kwa matibabu aliyomuwezesha huko India.Mrema anatetea ugali kwani asingeteuliwa kuwa mwenyekiti wa parole sukari ingeshammaliza
Mkemia ni mtumishi wa serikali, vipi kama akiambiwa aandike kuwa unatumia? Utabishia wapi!?Ana waanhusha nini ?
Kwani yeye ni kiongozi wa wachaga au wa taifa?
Kwani alichokosea ni kipi haswa ,kwenda kupima kwa mkemia majibu ndio yatakayokufanya uwe msafi au mwenye makosa
Lissu amekosa umaarufu? Kwa taarifa yako tu, kama Ni umaarufu, nadhani Lissu Ni Maarufu kuliko hata TZ! Tatizo lako Ni kuzaliwa majuzi!Kuna vitu vingne lisu anatufumbua macho ila vingne anajitafutia umarufu
Ile nafasi ni kweli kutibiwa bure tu India ametoka India juzi juzi tu......ashukuru hivyo hivyo njaa mchezo....tena ikiwa kichwani!!!Mrema anatetea ugali kwani asingeteuliwa kuwa mwenyekiti wa parole sukari ingeshammaliza
Uelewa wa Lissu ndio unawafanya watawala watishie kuifuta TLS maana wanajua hawafuati katiba wala sheriaduuuuu lisu ni shidaaa
Wote waseme lakini hata mrema?
ndio hakunaga kaimu Chief Judge!!Hio ndio sheria ambayo Magufuli kavunja?
Ni kweli Mkuu unachosema maana hata sielewi mrema anachokifanya, ningeshauri angenyamaza kimyaMrema Ni Msaka Tonge Aache Kukurupuka Afanye Kazi Yake
.........tungo tata lakini kitaeleweka tuKuna vitu vingne lisu anatufumbua macho ila vingne anajitafutia umarufu
Tatizo linaanzia kwa mwenye nyumba kwa kuwa anateua tu bila kuzingatia matakwa ya kisheria katika nafasi za uteuzi na mifano ya mikoroganyo hii ipo wazi mojawapo ni ile nafasi ya kuteua wabunge kumi.MWENYEKITI wa Parole, Augustino Mrema amemshukia Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chaydema), kuwa anafanya makosa makubwa kutetea watuhumiwa wa dawa za kulevya.
Akizunguma na MTANZANIA kwa simu jana, Mrema alisema anamshangaa Lissu kuwatetea watu wanaojihusisha na dawa za kulevya na kumshauri atumie elimu yake ya sheria kuwatetea waathirika na wanaotaja wahusika wa dawa za kulevya akiwamo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.
Mbali na Lissu, Mrema aliigeukia mahakama itambue kuwa pamoja na kutafsiri sheria, jukumu la kuzuia dawa za kulevya lipo mikononi mwao.
“Nashangazwa na hawa wanaotuhumiwa kukataa kwenda kupimwa na kuonyesha juhudi za kuzuia zoezi hilo, wakubali kwenda kupimwa kwani ndio itakuwa kusafishwa kwao kama majibu yatatoka kuwa hawatumii,” alisema Mrema.
Akizungumzia kauli hiyo, Lissu alisema Mrema anapaswa kujiuzulu cheo alichopewa cha Mwenyekiti wa Parole kwa sababu alipewa kinyume cha sheria.
Alisema sheria ipo wazi kwamba Mwenyekiti wa Parole awe jaji au alishawahi kuwa jaji na si mwanasiasa kama Mrema.
“Ninapoona Mrema anapiga kelele, anatetea chakula chake na si vinginevyo, kisheria Mwenyekiti wa Palore anapaswa kuwa jaji au alishawahi kuwa jaji,”alisema Lissu.
Aidha kuhusu kuwatetea watuhumiwa, Lissu ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa Chadema, alisema sheria ipo wazi kwamba Wanachofanya mawakili kwa sasa ni kuwatetea watuhumiwa wote hata wanaotuhumiwa na dawa za kulevya, kwani sheria inamtaka wakili kutetea yeyote bila ubaguzi.
Chanzo: Muungwana