Lissu: Mtu/Watu wenye nguvu walipanga kuniua kwa namna ambayo ingekuwa fundisho kwa wengine

Mtini

JF-Expert Member
Apr 28, 2011
1,486
2,332
Hakuna njia nzuri ya kufahamu una marafiki kiasi gani au una maadui kiasi gani kama ukiwa na shida na hasa ukiwa na shida ambayo si ya bahati mbaya.

Kuna shida ambazo ni za bahati mbaya na kuna nyingine ni za kutengenezwa kabisa. Watu wanakaa wanapanga wakutengenezee shida fulani. Kwangu mimi somo kubwa la hii miezi 16 ni hilo.

Nimeweza kufahamu nimegusa maisha ya watu kiasi gani. Nimeendelea kujifunza kuna watu kiasi gani ambao wangefurahi sana kama nisingekuwa kwenye dunia hii. Na hii story bado ina unflod.

Nimegundua kuna mahali nimefanya vitu sawa sawa na pengine kuna mahali nimefanya vitu sio sawa sawa. Nimepigwa risasi ambazo nisingemaliza nusu saa katika hali ya kawaida.

Ukiniangalia hivi unaniona kama Lissu yule wa Bungeni na hakuna namna ya kuwaonesha nyuma ya nguo hizi nikoje lakini ni makovu matupu ya risasi na visu vya hospitalini. Huu mwili umechanwa chanwa sana.

Kushambuliwa kwangu haikuwa ajali, haikuwa bahati mbaya. Kuna watu walikaa mahali wakaamua huyu Tundu Lissu stahili yake afe na afe kwa namna ambayo itatoa fundisho kwa akina Lissu wengine na wanaofikiria kuwa yeye.

Walipanga nife saa 7 mchana katikati ya vipindi vya Bunge. Wakatuma watu wa kuja kutekeleza hivyo ndio maana nasema haya si mazingira ya kawaida.

Baada ya kutengeneza huo mpango wao kelele ilikuwa kubwa sana juu ya matibabu yangu na Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu alisema Dada Alice(mke wangu) tunaomba uandike barua ya maombi na Spika naye akasema tunawasiliana na familia tunahitaji tu waandike maombi ili utaratibu wa sisi kulipa gharama ufanyike.

Tuna barua 5 toka Bungeni kuhusu matibabu. Ya mwisho inasema Bunge haliwezi kulipa gharama sababu kwanza hakuna barua ya kibali cha madaktari watatu toka Muhimbili, hakuna kibali cha K/Mkuu Afya na tatu hakuna kibali cha Rais cha kuidhinisha malipo.

Bunge lililipia gharama za matibabu ya Samwel Sitta ambaye hakuwa Mbunge kwa wakati ule lakini alituma email ya maombi ya kutibiwa na akalipiwa. Mimi niliyepigwa risasi nikiwa natoka kuchangia Bungeni nimepewa majibu kama hayo.

Eneo nililopigiwa risasi ile siku hakukuwa na ulinzi. Ni mtu mwenye nguvu kiasi gani anaweza kutoa amri ya ulinzi kutolewa mahali wanapoishi viongozi wa juu ikiwemo Mawaziri? Someone very powerful wanted me dead.

Rais Magufuli anavyopenda Televisheni lakini tangu 07.09.2019 hajawahi kutaja hata jina Tundu Lissu. Kuna katweet kamoja kanatembea sana ila siamini kama ni ya Magufuli. Ile ni ya Gerson Msigwa.

Someone ambaye sitilii shaka maneno yake aliniambia the order was akifa, hakuna shughuli Bungeni na msimlete Dar mkimbizeni kijijini mkamzike as soon as possible. Nahofia kutaja majina ila kuna siku nitayataja. Itakapokuwa salama kwao, si kwangu maana mimi ni survivor wa 16 bullets.
 
Naona ndio sasa anaingia ukumbuni akiwa ameongozana na mkewe na wanawapokea kwa wimbo wa kizalendo.

Lengo la mkutano ni kuwashukuru wote waliomchangia matibabu.

Nampongeza sana MC kwa kumsifia Mke wa Lissu kwa kuwa bega kwa bega na mumewe katika kipindi chote cha matatizo.

Lissu ndio sasa anaanza kuzungumza.

Ngoja tumsikilize na ninaamini hata Jiwe pale Magogoni anafuatilia ila kamruhusu mke wake aeleze ya moyoni kwanza ndio yeye aendelee kuongea.

Mke wa Lissu anawashukuru kwa support waliotoa.


Maelezo anayotoa kuhusu mwili wake baada ya shambulia yanasikitisha na kuumiza sana ila uzuri mwenyewe yuko happy siku zote.
 
Hii ni kauli ya Lissu aliyoitoa leo huko Washington DC wakati akiongea na watanzania wanaoishi nchini Marekani kuwashukuru kwa michanga yao ya matibabu.

Ila kasema kwa sasa anasita kutaja majina ila kuna siku atataja na kaongeza hata kama atakuwa amekufa, ipo siku watatajana.

Kazi ipo!
 
Tatizo la Mh lissu ni kuwa anajihami sana, kingne hana ushahidi kama angelikuwa na ushahidi angeutoa mapema, kingne Mh ni muoga sana inawezekana ushahidi anao lakni akawa muoga.

Kwan anatoa ushahidi wa waliompga au waliofanya mbinu za kumpga?

Je hao waliompga risasi wanaweza wakawa hai mpaka sasa?

wakati ukuta.
 
Jiwe ndio muuaji.

Hii ni moja ya sababu kwanini anamlinda sana Bashite kwani siri za maovu yote haya anahusika katika mikakati yake!!!! Akimuondoa Bashite atamwaga mboga!!! Lakini kuna siku huko mbele mboga lazima itamwagwa kwani si tunaona yanayomtokea TRUMP na wale waliokuwa wasaidizi wake!!! Learn from the experience of other people.
 
Tatizo la Mh lissu ni kuwa anajihami sana, kingne hana ushahidi kama angelikuwa na ushahidi angeutoa mapema, kingne Mh ni muoga sana inawezekana ushahidi anao lakni akawa muoga.

Kwan anatoa ushahidi wa waliompga au waliofanya mbinu za kumpga?

Je hao waliompga risasi wanaweza wakawa hai mpaka sasa?

wakati ukuta.
....
.....pancha ya baiskeli ikilumba mbele yako tutakuweka kwenye gari taka..jomba shatap hayajakukuta kale Matobolwa
 
Tatizo la Mh lissu ni kuwa anajihami sana, kingne hana ushahidi kama angelikuwa na ushahidi angeutoa mapema, kingne Mh ni muoga sana inawezekana ushahidi anao lakni akawa muoga.

Kwan anatoa ushahidi wa waliompga au waliofanya mbinu za kumpga?

Je hao waliompga risasi wanaweza wakawa hai mpaka sasa?

wakati ukuta.


Kupambana na someone very powerful usifikiri Ni mzaha
Yes kila kiumbe hai kinaogopa kufa.
Forces behind his assassination Hakuna ambaye asingeogooa. Hata hivyo Tundu Ni Jasiri Sana anampeleka muuaji kwenye Kona . Wanaanza kupagawa na kutenda mambo ya hovyo.
 
Kupambana na someone very powerful usifikiri Ni mzaha
Yes kila kiumbe hai kinaogopa kufa.
Forces behind his assassination Hakuna ambaye asingeogooa. Hata hivyo Tundu Ni Jasiri Sana anampeleka muuaji kwenye Kona . Wanaanza kupagawa na kutenda mambo ya hovyo.
.....
.....Mkuu mhurumie huyo Amevimbiwa matobolwa
 
Kama siyo mzaha unafikiri anaweza kuutoa ushahidi pasipo kudhibitiwa mapema, sasa hapo ndpo uoga ulipo anaweza akawa na ushaidi lakini akaogopa ilo!
Kingne anaogopa kufa baada ya jaribio la kutaka kuuliwa mwanzo!
Kupambana na someone very powerful usifikiri Ni mzaha
Yes kila kiumbe hai kinaogopa kufa.
Forces behind his assassination Hakuna ambaye asingeogooa. Hata hivyo Tundu Ni Jasiri Sana anampeleka muuaji kwenye Kona . Wanaanza kupagawa na kutenda mambo ya hovyo.

wakati ukuta.
 
Back
Top Bottom