KalamuTena
JF-Expert Member
- Jul 7, 2018
- 13,189
- 17,157
EeeenHeeee Heee!Vijana wa kitanzania tuna safari ndefu sana ya kuelewa maana ya siasa za nchi hii.
Yaani siku mtakapojua hata hao mnaowaunga mkono, (akina tundu et al) kwamba na wao wapo kwa maslahi yao binafsi; mnaweza kutamani kuhama dunia!
Kwa upande wangu naona ccm hakina tatizo, isipokuwa hakiwezi kutimiza matakwa ya kila mtu kwa wakati wote!
Ushauri wa bure: Ni afadhali sana katika maisha kusimamia kile unachoamini, pasipo kufuata ushawishi wa mtu/watu fulani. Hata kama utakuwa pekeeyako, ni afadhali kuliko kuwa wengi ambao hujui kila mmoja anawaza nini na kwa nia gani!
Hapa unajisikia umetoa bonge la hoja; kumbe hakuna kitu ila muunganisho wa maneno tu yasiyoleta maana yoyote.
Hebu rudi nyuma ujisomee mwenyewe uliyoandika, kama utaelewa ulichoandika.