macho_mdiliko
JF-Expert Member
- Mar 10, 2008
- 21,770
- 39,557
Achana na huyo hajui analosema. Madhali kiongozi anasimamia ukweli na haki basi huyo huyo ndiye tutakayempa sapoti. Akibadilika wala tusikate tamaa.dada hapa kuna pande 2 tu. wanaotaka Katiba na wasiotaka. zingine zoote ni means tu. Watu kama nyinyi ndo huwa mnakuja maelezo meengi ya kinafiki kama kinyonga
Watanzania tu wavivu kusoma ndiyo maana tunakata tamaa mapema au tunavunjika moyo kiongozi anapogeuka na kuwa upande wa CCM. Ukisoma historia za ukombozi duniani kote watu wanaoishia njiani au kubadilika na kuamua kushikamana na wakandamizaji ni wengi. Hata hapa tulipo bado wengi wataishia njiani. Lakini hili lisitukatishe tamaa.
Zitto mimi namfananisha na kiongozi mmoja alikuwa anaitwa Ndabaningi Sithole wa Zimbabwe. Wamefanana sana kitabia. Halafu Zitto ana wivu sana na hataki mtu mwingine au chama kingine kiwe na umaarufu kuliko yeye.
Baada ya kuhangaika na ATC Wazalendo kwa muda mrefu na kukosa waungaji mkono ameona ni bora ajipendekeze kwani hana cha kupoteza. Alidhani kujenga chama ni mchezo.
Ndiyo maana 2020 mgombea wao wa urais bwana Membe alikuwa anahutubia watu watatu tena huko kwao.