Na Shilatu, E.J
Matendo anayoyafanya Mgombea anayeitwa Tundu Lissu si mapya, yalikuwepo na waliyoyafanya waliishiwa kupata kichapo kikali.
Ngoja nimkumbushe kidogo. Kama suala la wafuasi na mashabiki walikuwepo Augustine Mrema akachapwa na Hayati Benjamin Mkapa; Alikuwepo Dk. Slaa akachapwa na Dk. Jakaya Kikwete; Alikuwepo Edward Lowassa mwaka 2015 aliyekuwa na mafuriko ya Watu akachapwa na Dk. John Pombe Magufuli. Hivyo Lissu asidanganywe na anayoyaona kichapo chake kipo pale pale.
Kama suala la kupondwa na uwongo kusemwa Wagombea wa upinzani walishapayuka sana kwa takribani miaka 28 lakini kichapo cha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kipo pale pale siku zote.
Kama suala ni kwenda Sokoni, mwaka 2015 Lowassa alienda masokoni ya Tandika na Kariakoo mpaka akanywa maji ya kufunga almaarufu maji ya Kandoro lakini bado kichapo akachezea. Lissu naye ajiandae kichapo kikali, maana hana jipya la ziada.
Kama ni kupanda mwendo kasi, Lowassa naye alipanda daladala lakini haikumsaidia kwani kichapo alichezea. Lissu hata apande Farasi nini mwendo kasi bado kichapo kipo pale pale.
Narudia tena kusema anayoyafanya Lissu si mapya kwenye ulimwengu wa sanaa za kisiasa kwani atavuna kichapo kikali maana anapita mule mule wenzake walipocharazwa, walio karibu nae wamueleze ukweli utakaomuandaa kisaikolojia ya kichapo kikali.
*Shilatu, E.J*
Matendo anayoyafanya Mgombea anayeitwa Tundu Lissu si mapya, yalikuwepo na waliyoyafanya waliishiwa kupata kichapo kikali.
Ngoja nimkumbushe kidogo. Kama suala la wafuasi na mashabiki walikuwepo Augustine Mrema akachapwa na Hayati Benjamin Mkapa; Alikuwepo Dk. Slaa akachapwa na Dk. Jakaya Kikwete; Alikuwepo Edward Lowassa mwaka 2015 aliyekuwa na mafuriko ya Watu akachapwa na Dk. John Pombe Magufuli. Hivyo Lissu asidanganywe na anayoyaona kichapo chake kipo pale pale.
Kama suala la kupondwa na uwongo kusemwa Wagombea wa upinzani walishapayuka sana kwa takribani miaka 28 lakini kichapo cha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kipo pale pale siku zote.
Kama suala ni kwenda Sokoni, mwaka 2015 Lowassa alienda masokoni ya Tandika na Kariakoo mpaka akanywa maji ya kufunga almaarufu maji ya Kandoro lakini bado kichapo akachezea. Lissu naye ajiandae kichapo kikali, maana hana jipya la ziada.
Kama ni kupanda mwendo kasi, Lowassa naye alipanda daladala lakini haikumsaidia kwani kichapo alichezea. Lissu hata apande Farasi nini mwendo kasi bado kichapo kipo pale pale.
Narudia tena kusema anayoyafanya Lissu si mapya kwenye ulimwengu wa sanaa za kisiasa kwani atavuna kichapo kikali maana anapita mule mule wenzake walipocharazwa, walio karibu nae wamueleze ukweli utakaomuandaa kisaikolojia ya kichapo kikali.
*Shilatu, E.J*