voicer
JF-Expert Member
- Jul 13, 2020
- 5,550
- 11,879
Hili lazima tuliangalie kwa jicho la tatu!jana akiwa pale Temeke alitoa tamko. Kwamba, atawaomba Watanzania na wanachama wa Chadema kuingia mtaani kuhakikisha katiba mpya inapatikana kabla ya Mwaka 2025.
Lakini wakati akisema hayo.
Lissu ametelemka uwanja wa Ndege wa "JNIA" Dar es Salaam, akiwasili bila kuandamana na familia yake!
Kwa maana kwamba amewaacha watoto wake,wakiendelea na mihula yao ya Masomo,huko Ulaya,
sambamba na mkewe ambae kimsingi ndie msimamizi wa familia.
Pia hata aliekuwa dereva wake, ambae walikimbia wote. Huenda anaendelea na kibarua chake huko huko,akaendelea kuwapeleka watoto shule na huduma zingine.
Hivyo, Lissu yuko hapa kimwoli,lakini kimawazo na kimaslahi. Yeye yuko Ulaya!
Na ikitokea akahsmasisha vurugu,zikitokea kutodhibiyika Lissu yeye atatimkia tena Ubelgiji,akiwaacha mkiumia kama alivyokwisha fanya hapo awali mwaka 2020,baada ya uchaguzi mkuu.
Lissu amekwisha lipwa stahiki zake zote,ikiwemo pia na gharama zake za matibabu (hii ni kwa mujibu wa kauli za serikali, pamoja na Lissu mwenyewe). Hata shavu lake linaashiria kwamba yuko kwenye neema.
Sasa anakuja kuwahamasisha watu walioko kwenye hizi dhiki za "Tozo", kwamba tatizo la dhiki zoote,litaondoka pale tu,watakapoamua kuingia mtaani kudai katiba mpya kwa kutumia. People's Power
Waumie wanyonge, wafe wanyonge,wapate vilema wanyonge, yaani Punda afe, ila Mzigo ufike!
Kisha siku ikitokea ndoto yake ikatimia.
Ndio familia yake ije nchini na kuendelea kulamba asali,baada ya kuwatumia wanyonge kwa utofahamu wao wa mambo!
Lissu na wanasiasa wengi wa kariba yao,hawana mapenzi ya dhati na watanzania wanyonge wa nchi hii.
Ndio maana yeye kwa ubinafsi wake,hufurahia pale mali za nchi hii kukamatwa nje ya nchi na kupelekea serikali kulipa mapesa mengi ambayo kimsingi ni jasho la walipa kodi wa nchi hii, ambao ndio sisi wanyonge anaotudhihaki kila uchao!
Ni Lissu huyuhyu ambae huwa ni mtetezi wa wezi wa madini yetu toka Ulaya, akifikia hadi kutoa ushirikiano kwao kitupeleka "MIGA" ili watushinde na kulipwa fidia na kisha yeye apate ujira wske kwa mchango wake.
Pia atutolee udafanuzi kuhusu hii picha hapa. Rais mtarajiwa wa Chadema,kwamba huyu mzungu ndie nani,na wakati haya yakiendelea. Mkeo alikuwa wapi hapo airport?
Hii ilikuwa juzi Huko Ubelgiji,muda mfupi kabla ya kuingia ndani ya ndege kuanza safari ya Tanzania.
Nimekuja na nimetoa nilichokiona. Wale wa matusi pia karibuni, ila jiwe la gizani limerushwa!
Alamsikhi.
10101.
Lakini wakati akisema hayo.
Lissu ametelemka uwanja wa Ndege wa "JNIA" Dar es Salaam, akiwasili bila kuandamana na familia yake!
Kwa maana kwamba amewaacha watoto wake,wakiendelea na mihula yao ya Masomo,huko Ulaya,
sambamba na mkewe ambae kimsingi ndie msimamizi wa familia.
Pia hata aliekuwa dereva wake, ambae walikimbia wote. Huenda anaendelea na kibarua chake huko huko,akaendelea kuwapeleka watoto shule na huduma zingine.
Hivyo, Lissu yuko hapa kimwoli,lakini kimawazo na kimaslahi. Yeye yuko Ulaya!
Na ikitokea akahsmasisha vurugu,zikitokea kutodhibiyika Lissu yeye atatimkia tena Ubelgiji,akiwaacha mkiumia kama alivyokwisha fanya hapo awali mwaka 2020,baada ya uchaguzi mkuu.
Lissu amekwisha lipwa stahiki zake zote,ikiwemo pia na gharama zake za matibabu (hii ni kwa mujibu wa kauli za serikali, pamoja na Lissu mwenyewe). Hata shavu lake linaashiria kwamba yuko kwenye neema.
Sasa anakuja kuwahamasisha watu walioko kwenye hizi dhiki za "Tozo", kwamba tatizo la dhiki zoote,litaondoka pale tu,watakapoamua kuingia mtaani kudai katiba mpya kwa kutumia. People's Power
Waumie wanyonge, wafe wanyonge,wapate vilema wanyonge, yaani Punda afe, ila Mzigo ufike!
Kisha siku ikitokea ndoto yake ikatimia.
Ndio familia yake ije nchini na kuendelea kulamba asali,baada ya kuwatumia wanyonge kwa utofahamu wao wa mambo!
Lissu na wanasiasa wengi wa kariba yao,hawana mapenzi ya dhati na watanzania wanyonge wa nchi hii.
Ndio maana yeye kwa ubinafsi wake,hufurahia pale mali za nchi hii kukamatwa nje ya nchi na kupelekea serikali kulipa mapesa mengi ambayo kimsingi ni jasho la walipa kodi wa nchi hii, ambao ndio sisi wanyonge anaotudhihaki kila uchao!
Ni Lissu huyuhyu ambae huwa ni mtetezi wa wezi wa madini yetu toka Ulaya, akifikia hadi kutoa ushirikiano kwao kitupeleka "MIGA" ili watushinde na kulipwa fidia na kisha yeye apate ujira wske kwa mchango wake.
Pia atutolee udafanuzi kuhusu hii picha hapa. Rais mtarajiwa wa Chadema,kwamba huyu mzungu ndie nani,na wakati haya yakiendelea. Mkeo alikuwa wapi hapo airport?
Hii ilikuwa juzi Huko Ubelgiji,muda mfupi kabla ya kuingia ndani ya ndege kuanza safari ya Tanzania.
Nimekuja na nimetoa nilichokiona. Wale wa matusi pia karibuni, ila jiwe la gizani limerushwa!
Alamsikhi.
10101.