Lissu atifulia vumbi Serikali kukiuka katiba wabunge walio RC/DC kuendelea na ubunge

Viongozi wa serikali ya ccm hawaheshimu katiba waliyoapa kuilinda! rais ndiye mhusika mkuu wa uvunjifu wa katiba kwa kuteua wabunge wa chama chake kuwa wakuu wa mikoa na wilaya huku akiwaacha kuwa wabunge!
 
2015 tunahitaji Lissu 49
John Mnyika 35
Zitto kabwe 27
Dr Slaa 7
Tupate wabunge 49 ngumi mkononi,
just in case mtu analeta zake bungeni,
hasa matusi ya nguoni.


Pia tunahitaji kundi la,
wapiganaji wapya kabisa na agenda mpya kabisa,
kama;
Wizi wa kampuni za simu Rate za kuua,
Huu mchezo wa kutoza rate za kubana mbavu Watanzania,
ni lazima uishe.

Mifereji Mikubwa ya maji machafu,
Hasa miji mikubwa kama Dar ni lazima
tuchimbe mifereji mizito ya chini kwa chini,
Kuondoa kabisa tatizo la maji machafu mijini.

Ujenzi holela na uharibifu wa mazingira,
Sheria ya umiliki wa ardhi na biashara. WaTanzania kwanza.
Mgeni yeyote ni lazima awe na 30 hisa za Watanzania wa kawaida,
katika biashara yake. Hataki kwenda kwao.

Watanzania ni lazima wamiliki 30%++ ya kila kampuni iliyopo Tanzania.
Hili ni lazima hata kama kwa kufanya hivyo 50% ya wana CCM watakufa kwa kihoro.

Nchi kugeuzwa dampo na vibaka wa CCM
Uingizaji wa vyakula vyenye sumu Ufisadi ndiyo asii
ya kuagiza vyakula hivi toka nje.

Walimu wa vyuo vikuu nje ya nchi moja kwa moja,
kupewa status ya Ualimu vyuo vya Tanzania

Urai wa nchi mbili,watu tunataka huku na kule,
Dunia ya kwanza tunaizimia na ya Tatu tunaizimia vilevile.


Mtu mmoja vyeo 7 wakati akili finyu.Huu ujinga na ushenzi wa vilaza
wakongwe wa CCM kushika nyadhifa kubwa uwe mwisho.

Pasipoti ni haki ya kila Mtanzania
Mtu kamwe asiulizwe swali kwa nini anataka pasipoti.

Mtwara kuwa Zone ya Viwanda,Utafiti na Maendeleo.

Jenga upya reli ya Mtwara ili Malawi Congo na Zambaia watumie Bandari ya Mtwara.


Rekebisha sheria,Fungua kesi za wezi wote Tanzania,
bila kujali vyeo vyao,
Kila mtu ni lazima abebe msalaba wake hata uwe mzito vipi.
Jenga Barabara inayoambaa ziwa Tanganyika,
kigoma mpaka Ziwa Nyasa Kyela ili kukuza utalii kanda ya Magharibi.

Weka Master planer ya miaka 100,
Ili Mikoa ya Dar na Pwani miundo mbinu yake ijengwe Tayari,
kwa Population ya watu 25,000,000 ifikapo 2030,
katika Satelite City 25

R.I.P
Mawazo mfu ya CCM na Serikali yake ni vema yaishie October 2015,
Sivyo tunatafuta kiama cha nchi yetu.
 
images


Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, (Chadema), amesema kitendo cha wabunge wameteuliwa kuwa wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa kuendelea kuruhusiwa kushiriki katika vikao vya Bunge ni kinyume cha Katiba.

Lissu ambaye ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi bungeni, alitoa kauli hiyo, wakati alipokuwa akiulizwa maswali ya papo kwa papo bungeni mjini Dodoma jana.

Alisema Katiba inakataza mtu ambaye ni afisa mwandamizi katika utumishi wa serikali ya Jamuhuri ya Muungano kuwa mbunge ama inamnyanga sifa yule ambaye ameteuliwa kuwa afisa mwandamizi kwenye utumishi wa serikali kuendelea kuwa mbunge.

Alisema kuna wakuu wa wilaya na mikoa ambao wamechaguliwa wakiwa wabunge na kwa hiyo wananyang’anywa sifa za kuendelea kuwa wabunge.

Alihoji kwa nini serikali inaendelea kuwaruhusu wakuu wa mikoa na wilaya hao kuendelea kuja bungeni wakati ni maofisa wa serikali.

Akijibu Pinda, alisema hana uhakika na linalosemwa kama ndio lilivyo. “Lakini kama ndivyo lilivyo bahati nzuri Mwanasheria Mkuu wa Serikali yupo hapa analisikia atalifanyia kazi.”
Kaazi kweli kweli. Mpaka ifike 2015. Legitimacy ya CCMABWEPANDE itakuwa 0 hakutakuweko na sababu ya uchaguzi. Yule kiazi mwanasharia mkuu aliweza kujibu kitu kweli!!! he he!!! Wanachowaza ni kuvizia na kuteka na kupeleka MABWEPANDE yameamua kuwa majambazi hayana kitu tena,
 
Hivi hapa lisiloeleweka ni nini ?

Tunaweza kujitungia sheria au kanuni halafu tushindwe kuzifuata, lakini sheria mama kama katiba! Inatisha!

Uelewa wa viongozi wa ccm na washauri wao ni mdogo mno... !! ni wavivu na wadhaifu katika mambo ya muhimu.
Mwanasheria mkuu wa serikali ya ccm sijui atakuja na maelezo gani hapo!!
 
Uelewa wa viongozi wa ccm na washauri wao ni mdogo mno... !! ni wavivu na wadhaifu katika mambo ya muhimu.
Mwanasheria mkuu wa serikali ya ccm sijui atakuja na maelezo gani hapo!!


Mwanasheria Mkuu wa serikiali bwana Werema atakuja na jibu laini na rahisi kwamba watu wana vichwa ambavyo kazi yake ni kuotesha nywele tu badala ya kutumika pia kwa ajili ya kufikiri.
 
72. Iwapo mtu yeyote mwenye madaraka katika utumishi wa
Serikali, madaraka ya aina iliyotajwa katika ibara ya 67(2)(g)
ataamua:-
(a) kuwa mgombea uchaguzi wa Rais au wa nafasi
nyingine yoyote chini ya Katiba hii;
(b) kugombea uongozi wa ngazi yoyote katika chama cha
siasa kinyume na masharti ya ajira,
mtu huyo atahesabiwa kuwa utumishi wake umekoma tangu
tarehe yake ya kuwa mgombea uchaguzi au ya kugombea
uongozi katika chama cha siasa.

Wakuu wa wilaya na mikoa sio maofisa waandamizi?


Kweli hii katia itakamilika, nikisoma huwa nasikia kinzungnzungu.
 
Hivi hapa lisiloeleweka ni nini ?

Tunaweza kujitungia sheria au kanuni halafu tushindwe kuzifuata, lakini sheria mama kama katiba! Inatisha!

66. (3) Where a Regional Commissioner is elected a Member of Parliament representing a constituency or where a Member of Parliament representing a constituency is appointed a Regional Commissioner, the National Assembly shall be deemed to consist of the requisite number of members and its proceedings shall be valid notwithstanding that the ordinary total number of members in terms of this Article shall have been reduced by reason of such election of the Regional Commissioner or such appointment of a constituency member.

Ni jambo la kusikitisha na kustaajabisha serikali wanasheria wake wanapkuwa mbumbumbu katika kuzidadafula sheria za nchi, papo wapinzani mahiri kwa sheria wakisaidia kuweka sawa mikondo ya sheria inayokwenda kinyume serikali inaendelea ni usanii wa kupuuzi hoja za kisheria.

Kuna ukweli wazi hapa alichokisema Mwanasheria wa Serikali Werema kwa Lisu kwamba ana kichwa ambacho kazi yake ni kuotesha nyele tu badala ya kutumika kwa kufikiri, kwa mtazamo wangu ni
vise versa.
 
Back
Top Bottom