Lissu asema CHADEMA itaigawa Tanzania kwa Majimbo. Kila jimbo litakula kwa urefu wa kamba yake

Serikali ya majimbo ndiyo majibu ya kuondokana na huu umasikini unaotengenezwa na mfumo wa kigandamizaji. Sasa hivi kila mtu anajitoa fahamu kumshukuru Rais wakati na yeye mtumishi tu wa wananchi kwa sababu yeye ndiye anaamuwa wapi kuendelezwe na wapi kusiendelezwe hadi anasema wasipochagua CCM hawawezi kujengewa lami bunda hivi kodi inayokusanywa pale bunda anahaki ya kwenda kuendelezea majimbo ya CCM badala ya Bunda ilipotoka kodi. Ni sawa kabisa kuwa na serikali za majimbo kwanza kutakuwa na kushindana kwa maendeleo kati ya jimbo na jimbo na hivyo kuchochoa kasi ya maendeleo. Hata viongozi wa hayo majimbo watawajibika kwa wananchi wa kwenye majimbo husika badala ya kuwa na hao mapandikizi ambao hawana uchungu wowote na maeneo wanayoyaongoza sababu wanawajibika kwa aliyewateua. Hata Haya maamuzi ya kutumia polisi kupiga wananchi yatakomeshwa kabisa sababu viongozi wote watakuwa wanawajibika kwa wananchi kama ilivyo katika katika kuwa mamlaka inatoka kwa wananchi siyo kwa Rais.
Dawa ya upuuzi huu wa CCM ni serikali za majimbo tu. Leo hii Kuna sehemu hazina hata barabara kisa tu zinaongozwa na upinzani alafu kibaya watu wanajisifu mchana kreupel Eti ole wenu mchague upinzani kama mtapata maendeleo!!!
 
Kwani Amajenga Burundi au Rwanda Tumia akilia wakati Mwingine hata ka ni BAVICHA KAJENGA TANZANIA HUTAKI HAMIA UBELIGIJI RUDI 2025 UJE UGOMBEE NA WEWE
Basi ka chemka kweli kweli, na litamkosti. Watanzania wengi wamechoka hii mfumo bandia wa demokrasia, tunahitaji mabadiliko ya ziada... na kama katiba ya Warioba itapewa kipau mbele na itatendewa haki, maendeleo ya kijumuishi na wa uhakika tutakuwa tumeshaiona na kuipima mpaka 2025...Na isitoshe Rais mpendwa ameshatuonesha njia sahihi ya kufanya kazi kwa bidii, Mungu akipenda atakae shika mpini hapo Oktoba atajaaliwa kuvunja rekodi ya mkulu, ondoa shaka kwa hilo...
 
Hii ni hoja ya Chadema ya siku nyingi tu, walikuwa wanaifunika blanketi ndio wafu wasione mpaka wakichukua dola. Tatizo Lissu ulimi hauna breki, kalimwaga mchana kweupe.
Hakuna cha kuficha,hili limekuepo kwenye ilani za miaka yote za chedema na kuonesha hilo wameigawa chedema katika kanda.
 
Ulidhani maendeleo yanaanzia wapi??

Sijui kama umewahi kifuatilia sera hizi za Mwalimu Nyerere.
i. Uanzishaji wa vijiji vya Ujamaa
ii.Madaraka mikoani.
iii.De centralization/ ugatuzi.

Maendeleo yanapaswa kuanzia levo ya chini kabisa ya Mtu, Kaya, kitongoji, kijiji, mtaa , kata Jimbo nk nk.

Ni yeye
 
Hakuna cha kuficha,hili limekuepo kwenye ilani za miaka yote za chedema na kuonesha hilo wameigawa chedema katika kanda.
Chadema wanatumia nguvu nyingi kuficha hii sera, hujawai kusikia kiongozi yoyote wa Chadema ana simama jukwaani na kusema nia ni kuigawa Tanzania kwa vipande. Hata kama iko kwenye sera lakini hainadiwi ki wazi-wazi. Lissu pekee ndio mwenye uwezo wa kumwaga mboga na ugali hadharani.

Kugawa majimbo, sio kugawa nchi. Huwezi kugawa nchi bila kubadili katiba. Na Chadema bila wabunge itabadili nini? Je vile vyama ambavyo Chadema inataka kushirikina navyo, na wao wanakubaliana kuimega Tanzania kwa vipande?
 
Hoja ya kiduanzi kabisa..na ambao wamekwisha neemeka na huu mfumo wa Sasa tutawadai warudishe fidia kwenye majimbo yaliyotoa hiyo michango..
 
Selfish oriented policy...maana baada ya hapo kila mtu ataenda kwenye Kanda yke kufanya maendeleo..mwisho utaskia wachaga wote,mwanza, kahama ,dar na other places warudi kwao..wakinga nao the like.

Kutakuwa na wasomi nao watataka wafanye kazi kwenye Kanda/Jimbo lao and the story goes on..
 
Selfish oriented policy...maana baada ya hapo kila mtu ataenda kwenye Kanda yke kufanya maendeleo..mwisho utaskia wachaga wote,mwanza, kahama ,dar na other places warudi kwao..wakinga nao the like..
Kutakuwa na wasomi nao watataka wafanye kazi kwenye Kanda/Jimbo lao..and the story goes on..

..wakati wa utawala wa Muingereza Tanganyika ilikuwa imegawanywa ktk majimbo.

..baada ya Uhuru, nadhani mwaka 1962, majimbo yaligawanywa zaidi na kuunda mikoa.

..hata wakati tuna majimbo wananchi walikuwa wanaweza kwenda maeneo mbalimbali na kufanya kazi au kujitafutia riziki.

..au kama tunaogopa nchi kugawanyika mbona sasa hivi kuna mikoa?
 
Majimbo au states ziko nchi ambazo watu wake walipigana Vita za wenyewe kwa wenyewe wakagawana kila bwana wa Vita kipande chake nchi hizo ni Kama Marekani , Afrika ya kusini,Nigeria na Sasa hivi Kenya imeingia utawala wa majimbo baada ya kutwangana kwa wao
 
Wasalaam wana jamvi

Leo Lissu kaendelea na kampeni lakini jambo la kushitua zaidi ni mpango wa chadema wa kuigawa Tanzania kwa majimbo kwa kisingizio kuwa majimbo ndio chanzo cha maendeleo!

Lissu ameendelea kusema kuwa nchi ikagawiwa kwa majimbo ndio watu watapata maendeleo na kila mtanzania atakula kwa urefu wa kamba zake!



Wasalaam wana jamvi
Ungeanza na Mwalimu Nyerere alianzisha madaraka mikoani japo hayakudumu kutokana na kutokuwa na ufuatiliaji. Tatizo ni kukurupuka na kutojaribu kuuelewa utawala wa majimbo ni nini na unafanyaje kazi. Mleta mada uliposikia hilo mara moja ukakimbilia kuandika bila kujenga hoja zaidi ya kubwabwaja.

Kwa kifupi utawala wa majimbo unarahishisha maamuzi ya matatizo kwenye eneo husika badala ya kupeleka kwa Rais ambaye atajibu kaeni na Bwege wenu si mlimchagua wenyewe! Tutaona kama atawaletea maendeleo.

Ungeisikiliza hotuba yake yote huko Mufindi ungeelewa kwani alikuwa akihutubia anawauliza anaowahutubia kisha anatoa mifano, hakuwa anafoka kama bwana yule.
 
Wasalaam wana jamvi

Leo Lissu kaendelea na kampeni lakini jambo la kushitua zaidi ni mpango wa chadema wa kuigawa Tanzania kwa majimbo kwa kisingizio kuwa majimbo ndio chanzo cha maendeleo!

Lissu ameendelea kusema kuwa nchi ikagawiwa kwa majimbo ndio watu watapata maendeleo na kila mtanzania atakula kwa urefu wa kamba zake!

Mtakumbuka huko nyuma Chadema walishasema kuwa wangependa Kaskazini wajitenge!

Wasalaam wana jamvi

Unahangaika na key board usiku , nenda kakojowe ukalale , au Lumumba wanakupa buku saba??

Mwinyi kajimilikisha ekari 60 000 kule Morogoro na Marehemu Mkapa kajimilikisha ekari 60 00 na kujiuzia mgodi , wewe hata sijui hata baisikeli walikupa unahangaika tu

Haya subiri sahani ya pilau, soda, kikoi na paketi ya sigara kali labda ndivyo unavyopigania
 
Hata mgombea wenu wa urais Meko ameshatugawa kikanda.

Kuna kanda ya kubomoleshewa nyumba na kuna kanda ya kulindwa

Kuna kanda ya kuongea kisukuma na kuna kanda ya kuongea broken swahili

Kuna kanda zinapewa ajira serikalini na kuna kanda zimetengwa kwa muda usiojulikana.
Sasa wewe unaisema Kigoma ambavyo hataki kabisa kuisikia kisa eti walimchagua upinzani na ndiyo kawaida yake kusema hivyo, ni bahati nzuri Chadema wanamstahi japo yeye hawapendi.
 
Hii ni hoja ya Chadema ya siku nyingi tu, walikuwa wanaifunika blanketi ndio wafu wasione mpaka wakichukua dola. Tatizo Lissu ulimi hauna breki, kalimwaga mchana kweupe.
Waliifunika au kwa sababu hujui kinachoendelea nchini kwako ndo maana unaona waliifunika?! Hivi si miaka michache tu iliyopita walipoanza kutumia sera yao ya majimbo kwa kuanzisha Majimbo ya Kisiasa?!
 
Ubaguzi na upendeleo wa Maguful kwa kanda ya ziwa na kijijini kwake kumeonesha tema umuhimu wa sera ya majimbo. Kanda ya Ziwa ingekuwa jimbo lenye serikali yake wakaamua kujenga CIA hamna mtu angeuliza.

Tatizo linakuja anapoamua kupendelea anapotoka na kuona kwingine hawastahili au wasubirie. Siyo haki


Kabisa.

Tena, tatizo siyo uwanja wa ndege, tatizo ni kwa nini chato na siyo Geita mkoani?

Ushauri:-
Jenga kwanza kwenye Makao makuu ya MIKOA, kisha WILAYA hatimaye TARAFA na KATA halafu malizia na kila KIJIJI.

Hospital kila Mkoa ni SAWA,hongera Rais.

Hospital kila WILAYA ni SAWA, hongera Rais.

Hospital kila Tarafa ni SAWA.

Hospital kila Kijiji ni SAWA.

"TATIZO KUAJIRI WATUMISHI"

NA UJENZI WA VIWANJA VYA NDEGE UNGEFUATA MTURIRIKO HUO, HAKUNA SHIDA.

Au kuna MPANGO wa kuanzisha Mkoa wa Chato, maana Katoro wameahidiwa WILAYA.
 
Dhambi ya kuwagawa Watanzania Ikianzaaa katika hayo majimbo mikoa inayochangia zaidi nayo itataka kujitenga kisha wilaya zinazozalisha sana nzao zitataka kujitenga mwisho Wa Siku Hii haitakuwa Nchi Moja Tena Na Rais Atakuwa Fala maana Yeye atakuwa na nguvu gani kwa hiyo Jimbo EBU TUACHIENI TANZANIA YETU ASEEE
Kama yalivyotaka kujitenga majimbo ya nchi gani kwa sababu yaliona yanachangia sana?!

Hata usipoweka sera za majimbo, usipojenga haki miongoni mwa maeneo mbalimbali, bado watu watakuwa na hisia za kujitenga!!

Miaka kadhaa iliyopita, kulikuwa na mbunge mmoja Kusini mwa Tanzania ambae alizoelea umaarufu kwa kuitetea Kusini hadi akafikia kusema haya mambo yakiendelea "Mikoa ya Kusini Tutajitenga na mpaka utakuwa Mto Rufiji"!

Alisema hayo si kwa sababu aliamini kusini inazalisha sana bali kwa sababu aliamini kusini inatengwa sana kwenye mipango ya serikali!
 
Mkuu wewe unadhani chanzo cha maendeleo ni nini?

Sijui unajua habari za ugatuzi/Decentralizatio?
Ama sijui unajua madaraka kwa Uma
Ama unajua Madaraka mikoani sera ya Ama vijiji vya ujamaa

Sera za Mwalimu Jk Nyerere
Umenikumbusha mbali sana nikiwa mdogo."Madaraka Mikoani"
 
Constitution law yenyewe hajui tofauti ya unitary na federal constitution ni kwamba kwenye federal (majimbo) Mkuu wa mkoa na serikali ya mkoa wanaamua budget yao ya mkoa wanatumia vipi katika fungu lao watakalopewa kutoka central government na kukusanya yale yale wanayoruhusiwa kama ilivyo leo kwenye mapato ya halmashauri.

Lakini mambo ya natural resources, corporate taxes, laws na kila kitu kinabaki serikali kuu kwenye federal wanaachiwa mambo machache sana.

Hivi huyu mbona mnamkuza sana, yeye ameishi sehemu na kujionea mambo fulani hata hajui how those systems work anajiropokea tu na kuna mijitu inashangilia.
 
Hii ni hoja ya Chadema ya siku nyingi tu, walikuwa wanaifunika blanketi ndio wafu wasione mpaka wakichukua dola. Tatizo Lissu ulimi hauna breki, kalimwaga mchana kweupe.
Wewe Leta Ilani ya CDM tangu mwaka 2000 ambayo haitaji ugatuzi wa madaraka kwenye majimbo?
 
Naunga mkono hoja ya Lissu kwa sababu anaweza kutekeleza ndoto zangu!!

Kwenye laptop yangu kuna unpublished manuscript niliyoandika 11 years ago! The title is Tanzania's Economic Development Bible!

Among other things ni kuunda Majimbo ya Kiuchumi with full autonomy ya kuendesha majimbo yao kiuchumi!
 
Back
Top Bottom