Tundu Lissu: Anayelishwa na kodi zetu ndio anasema Tanzania hakuna njaa

themagnificient

JF-Expert Member
Dec 13, 2016
965
3,277
Tundu Lissu akihojiwa na DW muda mfupi uliopita anasema kuwa Magufuli anachukulia jambo la njaa kuwa ni habari za uwongo kwa sababu yeye anaishi vizuri kwa kodi za wananchi.

''Hakuna njaa kwa sababu Magufuli anakula, na mamlaka zinazohusika na kutangaza njaa haziwezi kutangaza kwa kuwa watafukuzwa kwa kutofautiana na msimamo wa Rais'', alisema Lissu ambaye ni Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA na Wakili katika Mahakama Kuu.

Tundu Lissu pia amesema mitandao ya kijamii ina mchango mkubwa sana katika kuwapa jamii elimu kuhusu nchi yao na utendaji wa serikali lakini Magufuli anadhani mitandao na vyombo vya habari vipo kwa ajili ya kumsifia tu.

Anaendelea kueleza kuwa, kukamatwa kwa sababu ya kumkejeli Rais ni udikteta kwa kuwa katika nchi za demokrasia kwa kuwa rais akifanya mambo ya hovyo raia akimkejeli hana hatia.

Amezungumzia uchaguzi wa jimbo la Dimani ni wa muhimu ukizingatia hali ya siasa ya sasa, katika mwaka mmoja wa utawala wa Magufuli amevuruga sana haki za kidemorasia na kutumia mabavu kukandamiza haki za Wazanzibar na ametanabasha kwamba wakifanya vizuri kwenye uchaguzi huo ni wazi kuwa wananchi wa Zanzibar wameona utawala huu haufai.

Lissu amezungumzia pia uchaguzi wa Kenya na kudai ndio kwenye afadhali kwa nchi za Afrika Mashariki na utatoa fursa ya kujifunza kwa nchi zisizozingatia demokrasia.


CHANZO: DW Habari

 
hivi kwan yy tundu lisu kwani si anakula kwa kodi zetu au!mbunge anapata msharaha mkubwa,posho kibao,mafuta nk!,kweli mkuu kusema hakuna njaa kakosea ila na LISU nae alitakiwa aangalie point ya kuangalia kumshambulia maana ishu ya kodi mbnma lema tunamlipa mshahara kwa kodi zetu afu yupo ndani!
 
hivi kwan yy tundu lisu kwani si anakula kwa kodi zetu au!mbunge anapata msharaha mkubwa,posho kibao,mafuta nk!,kweli mkuu kusema hakuna njaa kakosea ila na LISU nae alitakiwa aangalie point ya kuangalia kumshambulia maana ishu ya kodi mbma lema tunamlipa mshahara kwa kodi zetu afu yupo ndani!
Ila mkulu wetu yeye anakataa yakuwa hakuna baa la njaa,yeye tundu lisu japokuwa anapokea na kula kodi zetu lakini kakubali yakuwa nchi ina njaa
 
Chadema haina ofisi, chadema inapokea mafisadi, chadema inasafisha mafisadi, chadema wamempoteza saa8 ,Mbowe ni mwenyekiti wa kudumu.

Lisu hiyo democrasia unayohubiri iko wapi ndani ya chadema??
Umeshikwa pasipostahili naona.
 
Chadema haina ofisi, chadema inapokea mafisadi, chadema inasafisha mafisadi, chadema wamempoteza saa8 ,Mbowe ni mwenyekiti wa kudumu.

Lisu hiyo democrasia unayohubiri iko wapi ndani ya chadema??
Richmond ni ya kikwete,nani alikula pesa za Escrow, kivuko, mabehewa feki, ukarabati uwanja wa ndege, malipo hewa wizara ya ujenzi?ni chadema wamekula pesa hizo zipo wapi chenji za Rada?pesa mnakula CCM.
 
Chadema haina ofisi, chadema inapokea mafisadi, chadema inasafisha mafisadi, chadema wamempoteza saa8 ,Mbowe ni mwenyekiti wa kudumu.

Lisu hiyo democrasia unayohubiri iko wapi ndani ya chadema??
Sio vipaumbele katika age CCM wameshaharibu kila kitu kinachoua uhai na usitawi wa taifa
 
Lupyee Mkuu usiongee mambo kwa matamanio yako kama kuna mafisadi

Uyo magu anae piga tarumbeta atawashtaki na kafungua mahakama ya mafisadi asha mshtaki nani?? Zaidi wanatumbuana wao kwa wao

Embu jifunze kuelewa jambo usiwe bendera fuata upepo

Nakuropoka jambo ambalo ushahidi nalo huna

Tatizo jf watu wanatumia fek account then wanajiona wanajua kila kitu kumbe ni mbululaaazz no moja

Sishangai lowassa kunadi elim elim elim kwasababu kuna watu wanaa macho lakini hawaoni wanamasikio lakini hawasikii
 
Back
Top Bottom