Lissu ambana Mbowe: Aelezea Historia yake, adai hajawahi omba kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA, "Nimekijenga chama kwa jasho na nguvu zangu"

CCM Wana mfumo mzuri wa kuachiana madaraka kila baada ya miaka kumi, ndiyo maana wanapeta tu.
Kwani kwa miaka 60 ya uhuru wa nchi hii ccm imewafanyia nini watanzania zaidi ya kuwatia umasikini ulio topea?
 
Kwa hiyo Mbowe akifa na chadema inakufa?
Of coz asipopatikana mtu kama MBOWE chama kinakufa hilo lipo wazi

Na ni ngumu sana kumpata mtu kama mbowe otherwise Mungu mwenyewe aamue kumleta wa kufanana nae

Na ndio maana and anibidi awe mwenyekiti yeye tu kwa sababu hakuna mbadala wake kwa sasa
 
CCM Wana mfumo mzuri wa kuachiana madaraka kila baada ya miaka kumi, ndiyo maana wanapeta tu.
Usitudanganye. CCM inabadilisha Mwenyekiti kila baada ya miaka kumi kwa sababu Rais mpya anaingia madarakani. Isingekuwa hivyo nao wangebaki na yule aliyeshindwa uchaguzi.
Tofauti kubwa na CCM ni kuwa Chadema wanakubali mtu ambae sio Mwenyekiti kugombea urais. Ni lini CCM wameruhusu mwanachama mwingine kushindana na Mwenyekiti aliyepo kugombea urais kwa niaba yao? Hiyo inatokea pale tu ambapo Mwenyekiti anakuwa hawezi kugombea tena urais kikatiba. Na hata hivyo, kama JK, alivyotufahamisha Mwenyekiti ana maamuzi makubwa kuhusu nani agombee.

Waacheni Chadema waendelee na mfumo ambao wao wanaona unawafaa. Ni wao peke yao ndio wenye maamuzi, sio wapinzani wao.

Amandla...
 
We ni moja ya kundi la watu wajinga ambao hata Mwenda alipokuwa anauwa watu na bado mlimshangilia. Lini uliona mbowe akitoa maneno ya Dharau kwa Dr slaa?.
Leo hii dr Slaa anaitwa dr Mihogo na misukule yako huku wengine wakiambatanisha na matusi, ww kama mwenyekiti umeshindwa kutoka hadharan kuwakemea hao mbwe.ha koko waliokuwa wanamchafua yule mzee alietumia nguvu zake na mali zake kupigania chama. Ilifikia kipindi dr Slaa alionekana hana thaman hata mbele ya "mr zero" kisa tu mshiko wake aliotumia kuhonga chama. Ki ukweli na bado dhambi ya kumtukana na kumdhalilisha dr Slaa itaendelea kukitafuna chama na wanachama kwa ujumla. Hongera pesa kwa kutuonesha ni nani mwenye roho ya utu na nani mwenye roho ya kutu.
 
Usitudanganye. CCM inabadilisha Mwenyekiti kila baada ya miaka kumi kwa sababu Rais mpya anaingia madarakani. Isingekuwa hivyo nao wangebaki na yule aliyeshindwa uchaguzi.
Tofauti kubwa na CCM ni kuwa Chadema wanakubali mtu ambae sio Mwenyekiti kugombea urais. Ni lini CCM wameruhusu mwanachama mwingine kushindana na Mwenyekiti aliyepo kugombea urais kwa niaba yao? Hiyo inatokea pale tu ambapo Mwenyekiti anakuwa hawezi kugombea tena urais kikatiba. Na hata hivyo, kama JK, alivyotufahamisha Mwenyekiti ana maamuzi makubwa kuhusu nani agombee.

Waacheni Chadema waendelee na mfumo ambao wao wanaona unawafaa. Ni wao peke yao ndio wenye maamuzi, sio wapinzani wao.

Amandla...
Inawezekana ikawa hivyo kweli, lakini kuna kigezo kimoja ambacho lazima Mgombea Urais anapaswa awe nacho Kaka Mbowe hana.

Hitaji la Mgombea lazima awe na Elimu ya Degree kutoka katika chuo kinacho tambulika.
 
Chadema kila siku mnasisitiza kutengeneza mifumo imara ya uongozi na siyo kutegemea mtu mmoja. Mbona nyie hamuonyeshi mfano kwenye chama chenu? Kwa hiyo Mbowe akifariki leo na Chadema ndo basi tena?
Akikujibu nitagi
 
Inawezekana ikawa hivyo kweli, lakini kuna kigezo kimoja ambacho lazima Mgombea Urais anapaswa awe nacho Kaka Mbowe hana.

Hitaji la Mgombea lazima awe na Elimu ya Degree kutoka katika chuo kinacho tambulika.
Mbowe amewahi kugombea ubunge mara mbili .
Unataka kusema NEC hawakujua kuwa Mbowe hana degree?
 
Akikujibu nitagi
Nakuona upo kwenye ubora wako.
Screenshot_20210309-134942.jpg
 
Back
Top Bottom