TandaleOne
JF-Expert Member
- Sep 4, 2010
- 1,644
- 709
Lisu akoroga msafara wa Slaa
Monday, 06 September 2010 20:13
Salim Said, Singida
MGOMBEA wa kiti cha ubunge wa Singida Mashariki kupitia tiketi ya Chadema, Tundu Lissu, amevuruga msafara wa mgombea urais wa chama hicho, Dk Willbrod Slaa, baada ya kumuamuru dereva wa gari lililokuwa limembeba mgombea urais, kuingia ghafla katika kituo cha mafuta cha Singida mjini jambo ambalo ni hatari.
Tukio hilo la aina yake na ambalo liliwashangaza na kuaacha midomo wazi watu waliokuwa katika msafara huo, lilitokea saa 7:25 mchana wa juzi, wakati msafara wa Dk Slaa ukiwa njiani kuelekea katika Kata ya Iglansoni, ukitokea Kata ya Sepuka katika Wilaya mpya ya Ikungi, mkoani humo.
Msafara huo ulikuwa na magari matano yaliyoongozana, mbele yakiongozwa na gari la polisi.
Tukio hilo lilikuja baada Lissu kugundua kuwa gari la Dk Slaa, lilikuwa na upungufu wa mafuta na hivyo akaamua lipelekewe kwenye kituo cha mafuta, lakini bila kutoa taarifa kwa polisi na viongozi wengine.
Baadhi watu, waliielezea kitendo hicho kuwa ni hatari na kwamba kilikuwa ni cha kuwadharau polisi waliokuwa wakiongoza msafara huo.
Watu walioshuhudia tukio hilo, walisema kitendo hicho, kingeweza kusababisha ajali katika msafara huo.
Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema Sabula, alikemea kitendo hicho na kutaka kusirudiwe tena kwa kuwa kinahatarisha maisha ya mgombea na watu wengine katika msafara.
"Sasa umefanya nini Lissu, huwezi kuitoa gari ya mgombea katikati ya mwendo na kuiingiza sheli, wakati mbele tunaongozwa na polisi, ni hatari, kisijirudie tena kitu hicho," alisema Sabula kwa hasira.
Baada ya kuingia katika kituo hicho cha mafuta, Lissu alishuka katika gari la mgombea na kwenda kwenye gari lake na kulipia mafuta.
Baadaye, alipanda gari lake badala ya lile la mgombea kama ilivyokuwa kabla ya tukio hilo.
Wakati hayo yakifanyika gari la polisi lililokuwa na askari sita wakiwemo wawili wenye silaha, lilikwenda kuegesha umbali wa mita 300, ili kusubiri msafara huo, uliokuwa umekatika.
Katika tukio lingine, gari hilo la Dk Slaa lilipata pancha wakati likielekea katika mkutano uliopangwa kufanyika Iglansoni saa 9:00 alasiri.
Hata hivyo, Dk Slaa alifaulishwa katika gari la Lissu ili awahi katika eneo la mkutano na kumwacha dereva na mlinzi mmoja wakibadilisha tairi.
Source:Mwananchi
Monday, 06 September 2010 20:13
Salim Said, Singida
MGOMBEA wa kiti cha ubunge wa Singida Mashariki kupitia tiketi ya Chadema, Tundu Lissu, amevuruga msafara wa mgombea urais wa chama hicho, Dk Willbrod Slaa, baada ya kumuamuru dereva wa gari lililokuwa limembeba mgombea urais, kuingia ghafla katika kituo cha mafuta cha Singida mjini jambo ambalo ni hatari.
Tukio hilo la aina yake na ambalo liliwashangaza na kuaacha midomo wazi watu waliokuwa katika msafara huo, lilitokea saa 7:25 mchana wa juzi, wakati msafara wa Dk Slaa ukiwa njiani kuelekea katika Kata ya Iglansoni, ukitokea Kata ya Sepuka katika Wilaya mpya ya Ikungi, mkoani humo.
Msafara huo ulikuwa na magari matano yaliyoongozana, mbele yakiongozwa na gari la polisi.
Tukio hilo lilikuja baada Lissu kugundua kuwa gari la Dk Slaa, lilikuwa na upungufu wa mafuta na hivyo akaamua lipelekewe kwenye kituo cha mafuta, lakini bila kutoa taarifa kwa polisi na viongozi wengine.
Baadhi watu, waliielezea kitendo hicho kuwa ni hatari na kwamba kilikuwa ni cha kuwadharau polisi waliokuwa wakiongoza msafara huo.
Watu walioshuhudia tukio hilo, walisema kitendo hicho, kingeweza kusababisha ajali katika msafara huo.
Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema Sabula, alikemea kitendo hicho na kutaka kusirudiwe tena kwa kuwa kinahatarisha maisha ya mgombea na watu wengine katika msafara.
"Sasa umefanya nini Lissu, huwezi kuitoa gari ya mgombea katikati ya mwendo na kuiingiza sheli, wakati mbele tunaongozwa na polisi, ni hatari, kisijirudie tena kitu hicho," alisema Sabula kwa hasira.
Baada ya kuingia katika kituo hicho cha mafuta, Lissu alishuka katika gari la mgombea na kwenda kwenye gari lake na kulipia mafuta.
Baadaye, alipanda gari lake badala ya lile la mgombea kama ilivyokuwa kabla ya tukio hilo.
Wakati hayo yakifanyika gari la polisi lililokuwa na askari sita wakiwemo wawili wenye silaha, lilikwenda kuegesha umbali wa mita 300, ili kusubiri msafara huo, uliokuwa umekatika.
Katika tukio lingine, gari hilo la Dk Slaa lilipata pancha wakati likielekea katika mkutano uliopangwa kufanyika Iglansoni saa 9:00 alasiri.
Hata hivyo, Dk Slaa alifaulishwa katika gari la Lissu ili awahi katika eneo la mkutano na kumwacha dereva na mlinzi mmoja wakibadilisha tairi.
Source:Mwananchi