Lishe kwa mtoto - Unampikia nini mtoto wako (miezi 6-12)

Achana na habari za uji huo mnaouita wa "lishe", kiukweli hauna lishe yoyote!! Wataalamu wa magonjwa ya watoto, na wataalamu wa lishe hawashauri kabisa matumizi ya hiyo kitu kwa sababu zifuatazo,
1.Contents za huo uji mnaoita wa "lishe" ni kama 6 hivi (mahindi,soya,ulezi,karanga,n.k.) ambapo hivyo vitu kila kimoja kinaiva katika temperatures tofauti. Kwa hiyo ukichanganya huo mchanganyiko unakuwa katika hatari ya kumlisha mtoto baadhi ya content ambazo eidha zinakuwa zimeiva kupitiliza na hivyo kuharibu virutubisho, au kumlisha contents ambazo hazijaiva.
2.Mchanganyiko wa hivyo vitu pia mara nyingi zinakuwa na virutubisho vile vile (mara nyingi ni wanga, na protini kwa kiasi, hivyo basi hakuna haja ya kuchanganya vitu vingi ambavyo vinakaribiana au kulingana aina ya virutubisho)
3.Pia ukichanganya mseto huo, contents za huo mseto pia zinakuwa na different shelf lives (muda wa kuweza kukaa bila kuharibika), hivyo basi unaweza kuwa unamlisha mtoto vitu vilivyooza. Mfano, karanga huwa zinaoza ndani ya wiki 1-2 tuu; hivyo component ya karanga ndani ya mseto huo, within 2 weeks tuu zinakuwa zimeshaoza tayari!!

Je, kitu gani cha kumlisha mtoto ambae tayari amefikisha umri wa miezi 6 na kuendelea?
Wataalamu wa lishe huwa wanashauri kuwa mtoto apewe a variety of foods (sio kupewa huo uji wa "lishe" kila saa, kila siku,asubuhi hadi jioni). Pia, inashauriwa mtoto apewe chakula mabacho familia inakula, ila kiweze kuandaliwa katika hali ya ulaini ambayo itampelekea mtoto aweze kula vizuri bila kukabwa; Pamoja na kuongezewa "snacks" yaani, milo midogo katikati mara 3-4. Kwa mfano: asubuhi kabisa mtoto akiamka, say saa 1 asbh anaweza akapewa uji wa unga wa mahindi, halafu labda saa nne akanywa chai pamoja na familia (labda akapewa slesi ya mkate uliolainishwa kwa kuchovya kwenye chai ya rangi,kwa mfano), halafu saa saba akala chakula cha mchana ambacho familia inakula (mfano kama familia inakula ugali maharage,ugali ukapondwa pondwa na kulainishwa na mchuzi wa maharage), then saa kumi mtoto akapewa uji wa unga wa ulezi kwa mfano, na kwenye saa moja wakati familia inakula pia akala chakula cha familia (mfano kama familia inakula wali samaki, wali ukachanganywa kwenye mchuzi wa samaki hadi ulainike, na mtoto akapewa pamoja na vipande vya samaki pia).
Hivyo basi, kama una uwezo wa kuwa na unga wa aina tofauti tofauti, ni afadhali ukawa na unga wa aina hizo tofauti tofauti (e.g. unga wa ulezi,unga wa mahindi,unga wa soya separately), halafu ukawa unampa mtoto uji wa tofauti tofauti ili kumbadilishia ladha; kuliko kuchanganya mseto wote huo na kumlazimisha mtoto kunywa uji huo huo, kila saa, kila siku; ndio maana watoto wengi muda wa kunywa huo mseto mnaouita "lishe" inakuwa ni kama vita kwa sababu na wao pia wanachoka ladha hiyo hiyo kila saa. Kama hauna uwezo wa kuwa na unga wa aina hizo tofauti tofauti pia, sio ishu kabisa mtoto wako anaweza kukua vizuri tuu kwa kula chakula cha familia ambacho kiko modified kidogo ili kilainike, na uji mmojawapo kati ya wa mahindi/ulezi au pia hata maziwa kama mtoto wako ni moenzi wa maziwa!!
Ni hayo tuu, mnisamehe kwa maelezo marefu.
chifu77
Nashukuru sana mkuu. Nilikuwa sijui kama karanga inawahi kuharibika kiasi hicho. Sasa mbona ukiuonja huo uji wa huo mchanganyiko una ladha nzuri na ni mtamu?
 
Nashukuru sana mkuu. Nilikuwa sijui kama karanga inawahi kuharibika kiasi hicho. Sasa mbona ukiuonja huo uji wa huo mchanganyiko una ladha nzuri na ni mtamu?
Karibu mkuu, ni jukumu letu kuelimisha jamii kuhusu haya mambo.
Karanga zinaharibika mapema sana; probably huwezi kudetect kwa kuonja kwa sababu kwa kawaida kiasi cha karanga kwenye huo mseto huwa kinakuwa ni kidogo ukilinganisha na components zingine. Pia mkuu, utamu wa kitu hauna uhusiano na afya au wingi wa virutubisho kwenye chakula husika. Kuna vitu vingi tuu ambavyo vina ladha tamu sana, lakini kiafya si salama, na havina virutubisho vyovyote. Mfano soda. chifu77
 
BUTTERBUT SQUASH;LISHE YA WATOTO KUANZIA MIEZI 6 NA KUENDELEA
Posted on AUGUST 8, 2015 9:14 PM by AFYABORAKWAMTOTO
Butternut squash ni jamii ya maboga ila hili linavirutubisho zaidi na ndio mana madaktari wengi wa watoto wanashauri mtoto apewe butternut squash akifika miezi sita muda sahihi wa mtoto kuanza kujifunza kula.





Umbo lake lipo kama kibuyu ,butternut ni chakula chepesi na laini kwa mtoto anaenza kufunzwa kula solid food ,lina lainisha tumbo na kumfanya mtoto kupata choo kwa urahisi kwa wale watoto wenye matatizo ya choo (constipation )linafaa zaidi.






Jinsi ya kupikwa
Butternut squash linanjia nyingi za kupikwa hapa nitakupa baadhi ya recipes unaweza mwandalia mtoto ,ukampumzisha kula viazi kila siku


  • Chemsha kwa dakika 10-15 likiiva mwaga maji weka maziwa ya baby formula (kopo) au maziwa ya mama nusu kikombe baada ya kukamua (pump) saga pamoja tayari kuliwa.


  • Butternut squash changanya na carroti 1 chemsha pamoja ikiiva saga na tayari kuliwa


  • Viazi vitamu changanya na butternut squash chemsha pamoja na kusaga


  • Zucchini chemsha pamoja na butternut ikiiva saga tayari kuliwa

HILI NDIO ZUCCHINI LINAUMBO LA TANGO

  • Butternut,kiazi ulaya,karoti na njegere kidogo pika pamoja weka butter au olive oil kidogo ikiiva saga tayari kuliwa.


Utakapo pika chakula cha mtoto tumia butter au olive oil kwa watoto walio chini ya mwaka 1
 
BUTTERBUT SQUASH;LISHE YA WATOTO KUANZIA MIEZI 6 NA KUENDELEA
Posted on AUGUST 8, 2015 9:14 PM by AFYABORAKWAMTOTO
Butternut squash ni jamii ya maboga ila hili linavirutubisho zaidi na ndio mana madaktari wengi wa watoto wanashauri mtoto apewe butternut squash akifika miezi sita muda sahihi wa mtoto kuanza kujifunza kula.





Umbo lake lipo kama kibuyu ,butternut ni chakula chepesi na laini kwa mtoto anaenza kufunzwa kula solid food ,lina lainisha tumbo na kumfanya mtoto kupata choo kwa urahisi kwa wale watoto wenye matatizo ya choo (constipation )linafaa zaidi.






Jinsi ya kupikwa
Butternut squash linanjia nyingi za kupikwa hapa nitakupa baadhi ya recipes unaweza mwandalia mtoto ,ukampumzisha kula viazi kila siku


  • Chemsha kwa dakika 10-15 likiiva mwaga maji weka maziwa ya baby formula (kopo) au maziwa ya mama nusu kikombe baada ya kukamua (pump) saga pamoja tayari kuliwa.


  • Butternut squash changanya na carroti 1 chemsha pamoja ikiiva saga na tayari kuliwa


  • Viazi vitamu changanya na butternut squash chemsha pamoja na kusaga


  • Zucchini chemsha pamoja na butternut ikiiva saga tayari kuliwa

HILI NDIO ZUCCHINI LINAUMBO LA TANGO

  • Butternut,kiazi ulaya,karoti na njegere kidogo pika pamoja weka butter au olive oil kidogo ikiiva saga tayari kuliwa.


Utakapo pika chakula cha mtoto tumia butter au olive oil kwa watoto walio chini ya mwaka 1
Hiyo butternut kwa kiswahili yaitwaje?
Nimependa hapo pa kuchanganya na maziwa ya mama
 
Wakuu mwanangu hapendi maji, sijui nitumie mbinu gani? Ana miezi 6...
Take it easy. We mnyweshe akikataa mwache ngojea muda kama lisaa ama nusu saa mpe akikataa mwache tena masaa kadhaa. Unajua wazazi wakati mwingine huwa tunawalazimisha watoto kula ama kuwapa vyakula tukijua ni watoto hapo tunakosea inabidi kumpangia mtoto ratiba ya kula ni sawa na wewe mtu akulazimishe kunywa maji au kula kipindi huna kiu au njaa utafanyaje?. Mie wangu akikataa naweka pembeni namwacha aende zake mwenyewe akiniona baadae nakunywa maji au nakula anajileta mwenyewe anapata vyake anasepa tena. Tumia ratiba yako ya kunywa maji kwa mwanao ikiwa hana tatizo lolote.
 
Farkhina aksante mno kwa uzi mzuri. Utatusaidia wengi.

Wangu ana miezi 5 soon tunaanza mchakato wa chakula. Maziwa ya mama ananyonya usiku tu. Mchana formula sababu kwanza alikuwa hashibi na pia ratiba za ajira.

Naomba kuuliza, tunashauriwa chakula cha mtoto kiwe fresh yaani kipikwe ale. Siyo unapika asubuhi ale jioni. Sasa wenzangu mnafanyaje? H/gs ndo wanapika mchana wakati mpo makazini au?

At least cha jioni mama unaweza andaa as ukiwahi kurudi...including weekends.

Maana hawa H/gs nao umakini unahitajika.
 
Take it easy. We mnyweshe akikataa mwache ngojea muda kama lisaa ama nusu saa mpe akikataa mwache tena masaa kadhaa. Unajua wazazi wakati mwingine huwa tunawalazimisha watoto kula ama kuwapa vyakula tukijua ni watoto hapo tunakosea inabidi kumpangia mtoto ratiba ya kula ni sawa na wewe mtu akulazimishe kunywa maji au kula kipindi huna kiu au njaa utafanyaje?. Mie wangu akikataa naweka pembeni namwacha aende zake mwenyewe akiniona baadae nakunywa maji au nakula anajileta mwenyewe anapata vyake anasepa tena. Tumia ratiba yako ya kunywa maji kwa mwanao ikiwa hana tatizo lolote.
ngoja nijaribu huu utaratibu
 
zingatia ucje ukaweka chumv nyingi kwenye cchakula cha mtot figo zake hazina uwezo mkubwa wakuiondoa Huyo chumvi mwilin inatakiwa use unaihic kwa mbal xana
 
Back
Top Bottom