Lishe kwa mtoto - Unampikia nini mtoto wako (miezi 6-12)

Mihogo ya sukari na nazi....nimepika jana so sweet
Namna ya kuandaa
. Menya mihogo, ikate katikati kutoa ule uzi
. Ichemshe na maji tu hadi iive ilainike
. Maji yakikauka katia kitunguu nusu, hoho kipande kidogo, mafuta kijiko kimoja cha chakula, kwangulia carrot, weka sukari na tui la nazi acha ichemke
. Nazi ikibaki kidogo, koroga koroga ili iwe rojo
Msosi upo tayari kwa kuliwa. Ni tamu hiyo bad luck mwanangu aligoma kula nikala mwenyewe chote nikamaliza
Hahahaaaa! Vyakula vya watoto huwa ni vitamu sijui kwanini wao huwa hawavipendi.
 
Ngoja nikioa ntafuata,Maelekezo yote hayo Ahsante wandugu na Wanachama Wa JF-Members.Nimependa comment zenu imekaa safi sana.
 
Jaman mimi naomba msaada wanangu ana miezi 5 na nusu ila alipata toka jtano alikua anakataa kunyonya mpaka namlazimisha. Ijumaa jikaendabkumpima kwani alikaa anachemka. Nilimuanishia quinini kwaninalikua na maralia , kuanzia hapo anatapika tuu akiona nikimpa dawa, nikimpa uji au maziwa nikutapika tuu. Kinacho nisumbia sana nikutonyonya kabisaaaaa yaani hataki kuona nikilio utazani umemlambisha limao. Mpaka leo tokea jmosi . msaada jaman.
 
mi wangu anapenda ugali maharagwe ana miezi mi 8 sasa cjui kurithi au? hata niandae nn yeye nguna na ndondo tu,
hahahahaaa.....umenifanya nicheke. Hiyo ya kurithi aisee ipo. Mama yangu aliniambia nikiwa mdogo toka nimeanza kukaa chakula changu kikuu kilikuwa maharage. Ndo chakula pekee nilichokuwa nakula kwa hiari. Kabla hayajarojeka yanawekwa kwenye sahani naokota moja moja kama karanga. Huyu wa kwangu nae hivyo hivyo. Ana miaka 8 lakini maharage ndo mboga pendwa.
 
Ulishaji watoto wa miezi 6-59.
ni muhimu kumwanzishia mtoto chakula kikamilifu akifika miezi 6 maana kabla ya hapo mtoto anatakiwa anyonyeshwe tuu. chakula kamili ni kile chenye makundi yote na chakula kwa viwango vya kufaa kulingana na mahitaji ya mtoto.
Kuna aina ya boga ambalo ni zuri sana kwa chakula cha mtoto na bei yake ni nafuu na lina virutubishi kwa wingi linaitwa butter nut.
sijui kiswahili chake ila unalichemsha kama boga la kawaida na kuliponda na cream kidogo na maziwa kidogo halafu unamlisha mtoto.
 
Habari wanajukwaa... Nimekutana na hii nikaona ni vyema kushare nanyi. Sijui kama ipo humu tayari kama ipo naomba mniwie radhi.

KARANGA NI SUMU KWA MTOTO:KUCHANGANYA KARANGA KWENYE NAFAKA(UNGA WA LISHE) NI SUMU HATARI
Posted on AUGUST 3, 2015 9:30 PM by AFYABORAKWAMTOTO
Matumizi ya karanga kwa uji wa mtoto ni vizuri sababu inamwongezea virutubisho ,mafuta na kumsaidia kulainisha choo ila karanga haitakiwi kukaa kwa mda mrefu baada ya kusagwa.



Karanga inatabia ya kutengeneza fangasi hivyo utakapo andaa nafaka(mfano -ulezi,mahindi,mchele,ngano….) za kutengeneza unga wa lishe haipaswi kuchanga’nya na karanga ,iwapo utasaga nafaka usichanganye na karanga,karanga saga pembeni na isiwe nyingi saga ya kutosha itakayo tumika wiki moja (siku 7) na unatakiwa uhifadhi sehemu kavu na safi kwenye chombo cha plastik chenye mfuniko.






Utakapo pika uji baada ya dakika 10 ongezea karanga vijiko 2-3 vikubwa ,koroga na acha karanga iive vizuri ndio uepue tayari kumpa mtoto,uji wa lishe unatakiwa kupikwa kwa mda mrefu sichini ya dakika 35-45 moto usiwe mkali ,sababu huo mchanganyiko wa nafaka na karanga uive vizuri lasivyo mtoto ataharisha.
[paste:font size="6"]JINSI YA KUANDAA KARANGA



Chambua karanga vizuri ondoa zile mbovu na pepeta kwenye ungo,andaa moto usiwe mkali mdogo tu, bandika sufuria na kukaanga bila mafuta zikibadili rangi kidogo epua. Anika juani zikikauka toa maganda yake na kuchambua tena kutoa zilizoungua au mbovu ,tayari kusagwa kwa blender au kutwanga na kinu au peleka mashine ila hakikisha unafanya kwa hali ya usafi. Baada ya kusagwa hifadhi kwenye chombo cha plastik na kufunika hakikisha isikae zaidi ya siku 7.[/paste:font]





[paste:font size="6"]MADHARA YA KUCHANG’ANYA KARANGA NA NAFAKA ZA(UNGA WA LISHE) WAKATI WA KUSAGA!
Karanga inatabia ya kuotesha fungus na kutengenza sumu ya toxin inakuja kuadhiri ini la mtoto na kumpelekea kupata saratani ya ini daktari bingwa wa watoto hospital ya muhimbili Dr Masawe anashauri karanga iandaliwe kidogo na itumike wakati wa kupika uji , karanga inatabia ya kuungua / kunata kwenye sufuria mapema kabla uji haujaiva, hapo unakuwa unapoteza vitutubisho vyote vilivyomo hivyo ni vizuri ukafatilia maelezo nilio toa hapo juu jinsi ya kutumia karanga kwa njia sahihi.[/paste:font]






Ushauri wa afyaborakwamtoto


Unaponunua / tengeneza unga wa lishe usinunue / kutengeneza wenye mchanganyiko wa

1:Nafaka zaidi ya mbili yani kama ni (mahindi,soya,uwele,mtama na nyinginezo) badala yake nunua wenye nafaka 1-2 tu ,kwani mchang’ayiko mkubwa sio mzuri kwa mtoto unahatarisha afya yake sababu utumbo(mfumo wa mmeng’nyo) wake hauna uwezo wa kumeng’enya vyote hivyo kwa wakati 1bado ni mdogo na utamfunga choo



2:Usinunue unga wa lishe wenye soya ndani kwa watoto chini ya miaka 2


3:Usinunue uji wa lishe wenye mchanganyiko wa karanga
 
Habari za asubuhi wadau. Poleni kwa janga la sukari. Naombeni kujua namna ya kuandaa mchanganyiko sahihi wa uji wa lishe kwa ajili ya matumizi ya watoto nyumbani. Mfana, kilo ngapi za mahindi, soya, ulezi n.k.
 
mahindi ya njano kilo mbili ngano ambayo haijakobolewa kg moja soya kg moja mchele kg moja karanga kg moja ulezi nusu nadhani nimemaliza
 
mahindi ya njano kilo mbili ngano ambayo haijakobolewa kg moja soya kg moja mchele kg moja karanga kg moja ulezi nusu nadhani nimemaliza
Sijaona mahindi ya njano miaka sasa. Wapi yanapatikana? Au ni yale ya bisi?
 
Habari za asubuhi wadau. Poleni kwa janga sukari. Naombeni kujua namna ya kuandaa mchanganyiko sahihi wa uji wa lishe kwa ajili ya matumizi ya watoto nyumbani. Mfana, kilo ngapi za mahindi, soya, ulezi n.k.
Achana na habari za uji huo mnaouita wa "lishe", kiukweli hauna lishe yoyote!! Wataalamu wa magonjwa ya watoto, na wataalamu wa lishe hawashauri kabisa matumizi ya hiyo kitu kwa sababu zifuatazo,
1.Contents za huo uji mnaoita wa "lishe" ni kama 6 hivi (mahindi,soya,ulezi,karanga,n.k.) ambapo hivyo vitu kila kimoja kinaiva katika temperatures tofauti. Kwa hiyo ukichanganya huo mchanganyiko unakuwa katika hatari ya kumlisha mtoto baadhi ya content ambazo eidha zinakuwa zimeiva kupitiliza na hivyo kuharibu virutubisho, au kumlisha contents ambazo hazijaiva.
2.Mchanganyiko wa hivyo vitu pia mara nyingi zinakuwa na virutubisho vile vile (mara nyingi ni wanga, na protini kwa kiasi, hivyo basi hakuna haja ya kuchanganya vitu vingi ambavyo vinakaribiana au kulingana aina ya virutubisho)
3.Pia ukichanganya mseto huo, contents za huo mseto pia zinakuwa na different shelf lives (muda wa kuweza kukaa bila kuharibika), hivyo basi unaweza kuwa unamlisha mtoto vitu vilivyooza. Mfano, karanga huwa zinaoza ndani ya wiki 1-2 tuu; hivyo component ya karanga ndani ya mseto huo, within 2 weeks tuu zinakuwa zimeshaoza tayari!!

Je, kitu gani cha kumlisha mtoto ambae tayari amefikisha umri wa miezi 6 na kuendelea?
Wataalamu wa lishe huwa wanashauri kuwa mtoto apewe a variety of foods (sio kupewa huo uji wa "lishe" kila saa, kila siku,asubuhi hadi jioni). Pia, inashauriwa mtoto apewe chakula mabacho familia inakula, ila kiweze kuandaliwa katika hali ya ulaini ambayo itampelekea mtoto aweze kula vizuri bila kukabwa; Pamoja na kuongezewa "snacks" yaani, milo midogo katikati mara 3-4. Kwa mfano: asubuhi kabisa mtoto akiamka, say saa 1 asbh anaweza akapewa uji wa unga wa mahindi, halafu labda saa nne akanywa chai pamoja na familia (labda akapewa slesi ya mkate uliolainishwa kwa kuchovya kwenye chai ya rangi,kwa mfano), halafu saa saba akala chakula cha mchana ambacho familia inakula (mfano kama familia inakula ugali maharage,ugali ukapondwa pondwa na kulainishwa na mchuzi wa maharage), then saa kumi mtoto akapewa uji wa unga wa ulezi kwa mfano, na kwenye saa moja wakati familia inakula pia akala chakula cha familia (mfano kama familia inakula wali samaki, wali ukachanganywa kwenye mchuzi wa samaki hadi ulainike, na mtoto akapewa pamoja na vipande vya samaki pia).
Hivyo basi, kama una uwezo wa kuwa na unga wa aina tofauti tofauti, ni afadhali ukawa na unga wa aina hizo tofauti tofauti (e.g. unga wa ulezi,unga wa mahindi,unga wa soya separately), halafu ukawa unampa mtoto uji wa tofauti tofauti ili kumbadilishia ladha; kuliko kuchanganya mseto wote huo na kumlazimisha mtoto kunywa uji huo huo, kila saa, kila siku; ndio maana watoto wengi muda wa kunywa huo mseto mnaouita "lishe" inakuwa ni kama vita kwa sababu na wao pia wanachoka ladha hiyo hiyo kila saa. Kama hauna uwezo wa kuwa na unga wa aina hizo tofauti tofauti pia, sio ishu kabisa mtoto wako anaweza kukua vizuri tuu kwa kula chakula cha familia ambacho kiko modified kidogo ili kilainike, na uji mmojawapo kati ya wa mahindi/ulezi au pia hata maziwa kama mtoto wako ni moenzi wa maziwa!!
Ni hayo tuu, mnisamehe kwa maelezo marefu.
chifu77
Peace92
 
Back
Top Bottom