BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,792
- 287,994
Lipumba: Tumkumbuke Mwalimu Nyerere Siku ya Kuzaliwa
Mwandishi Wetu Oktoba 15, 2008
Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo
Asema aliowaamini ndio waliovuruga nchi
MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba anasema kwamba inasikitisha kwamba taifa limeshindwa kumuenzi Mwalimu Nyerere kupiga vita rushwa, uozo ambao alisimama kidete kuupiga vita katika kipindi chake chote cha uongozi.
Ameiambia Raia Mwema katika mahojiano kwamba anamkumbuka Mwalimu kama mtu aliyekuwa anachukia mno rushwa akifuata kwa dhati moja ya ahadi za Mwana TANU iliyokuwa ikisema kwamba "rushwa ni adui wa haki, sitapokea, wala kutoa rushwa".
Anasema kwamba suala la kupiga vita rushwa sasa limeachwa huku Taifa likionekana wazi kwenda kombo katika vita hiyo na hasa baada ya awamu ya tatu iliyokuwa ikiongozwa na watu ambao Mwalimu Nyerere mwenyewe alidhani ni waadilifu.
Kwa mujibu wa Profesa Lipumba, maovu mengi yanayohusiana na rushwa na ufisadi yalijitokeza katika kipindi cha mwisho cha awamu ya tatu chini ya aliyekuwa Raism, Benjamin Mkapa na kwamba awamu ya nne ya sasa inayoongozwa na Rais Jakaya Kikwete imeshindwa kutatua uozo huo ulioanzia wakati wa Mkapa.
Anasema mwaka 1999 wakati Mwalimu anafariki ndio wakati ambao ilisajiliwa kampuni ya Anben, inayodaiwa kuwa ya watu walioko karibu na Mkapa, iliyokopa dola milioni 500,000 na kuzilipa bila ya mapato yake kujulikana yanatoka wapi.
Anasema pia kwamba ndani ya awamu ya tatu ndimo mwaka 2002 lililopozuka sakata la rada ambalo gazeti la Guardian la Uingereza liliripoti ya kuwa Kampuni ya BAE System lililipa dola milioni 12 kama rushwa.
Kashfa nyingi za ufisadi ukiwamo wa EPA (Akaunti ya Nje ya Benki Kuu) zilitokea wakati wa uongozi wa Rais Mkapa, mtu ambaye Mwalimu alikuwa na imani naye sana," alisema Prifesa Lipumba akiongeza kwamba uongozi wa awamu ya tatu ulishindwa kufuata maadili ya Mwalimu kuhusu rushwa hiyo ikionyesha kwamba " tumeshindwa kumuenzi kama inavyopaswa".
Je, anasemaje kuhusu maadhimisho ya siku ya kifo cha Mwalimu? Kwa maoni yake, ni makosa kumkumbuka siku aliyofia. Alisema ingekua bora Taifa lingekuwa linamkumbuka siku aliyozaliwa.
"Ingekuwa vizuri tungekuwa tunamkumbuka siku aliyozaliwa kwa sababu Mwalimu alikufa kwa kifo cha kawaida. Siku ya kuzaliwa kwake ingekuwa na maana zaidi," anasema.
Lakini alisema pia kwamba binafsi anamkumbuka Mwalimu Nyerere kwa mengi na kumbukumbu ya Mwalimu isiyofutika katika kichwa chake ni ya mwaka 1962 alipokuwa mdogo Mwalimu alipohutubia mkutano wa TANU.
Alisema kwamba Mwalimu alikuwa na mvuto mkubwa mno na anakumgbuka jinsi alivyoubadilisha wimbo wa Kinyamwezi wa "Ohoo sase zabela mitwe" (Ohoo risasi zavunja kichwa) kuwa "Ohoo TANU yajenga nchi".
Mwandishi Wetu Oktoba 15, 2008
Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo
Asema aliowaamini ndio waliovuruga nchi
MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba anasema kwamba inasikitisha kwamba taifa limeshindwa kumuenzi Mwalimu Nyerere kupiga vita rushwa, uozo ambao alisimama kidete kuupiga vita katika kipindi chake chote cha uongozi.
Ameiambia Raia Mwema katika mahojiano kwamba anamkumbuka Mwalimu kama mtu aliyekuwa anachukia mno rushwa akifuata kwa dhati moja ya ahadi za Mwana TANU iliyokuwa ikisema kwamba "rushwa ni adui wa haki, sitapokea, wala kutoa rushwa".
Anasema kwamba suala la kupiga vita rushwa sasa limeachwa huku Taifa likionekana wazi kwenda kombo katika vita hiyo na hasa baada ya awamu ya tatu iliyokuwa ikiongozwa na watu ambao Mwalimu Nyerere mwenyewe alidhani ni waadilifu.
Kwa mujibu wa Profesa Lipumba, maovu mengi yanayohusiana na rushwa na ufisadi yalijitokeza katika kipindi cha mwisho cha awamu ya tatu chini ya aliyekuwa Raism, Benjamin Mkapa na kwamba awamu ya nne ya sasa inayoongozwa na Rais Jakaya Kikwete imeshindwa kutatua uozo huo ulioanzia wakati wa Mkapa.
Anasema mwaka 1999 wakati Mwalimu anafariki ndio wakati ambao ilisajiliwa kampuni ya Anben, inayodaiwa kuwa ya watu walioko karibu na Mkapa, iliyokopa dola milioni 500,000 na kuzilipa bila ya mapato yake kujulikana yanatoka wapi.
Anasema pia kwamba ndani ya awamu ya tatu ndimo mwaka 2002 lililopozuka sakata la rada ambalo gazeti la Guardian la Uingereza liliripoti ya kuwa Kampuni ya BAE System lililipa dola milioni 12 kama rushwa.
Kashfa nyingi za ufisadi ukiwamo wa EPA (Akaunti ya Nje ya Benki Kuu) zilitokea wakati wa uongozi wa Rais Mkapa, mtu ambaye Mwalimu alikuwa na imani naye sana," alisema Prifesa Lipumba akiongeza kwamba uongozi wa awamu ya tatu ulishindwa kufuata maadili ya Mwalimu kuhusu rushwa hiyo ikionyesha kwamba " tumeshindwa kumuenzi kama inavyopaswa".
Je, anasemaje kuhusu maadhimisho ya siku ya kifo cha Mwalimu? Kwa maoni yake, ni makosa kumkumbuka siku aliyofia. Alisema ingekua bora Taifa lingekuwa linamkumbuka siku aliyozaliwa.
"Ingekuwa vizuri tungekuwa tunamkumbuka siku aliyozaliwa kwa sababu Mwalimu alikufa kwa kifo cha kawaida. Siku ya kuzaliwa kwake ingekuwa na maana zaidi," anasema.
Lakini alisema pia kwamba binafsi anamkumbuka Mwalimu Nyerere kwa mengi na kumbukumbu ya Mwalimu isiyofutika katika kichwa chake ni ya mwaka 1962 alipokuwa mdogo Mwalimu alipohutubia mkutano wa TANU.
Alisema kwamba Mwalimu alikuwa na mvuto mkubwa mno na anakumgbuka jinsi alivyoubadilisha wimbo wa Kinyamwezi wa "Ohoo sase zabela mitwe" (Ohoo risasi zavunja kichwa) kuwa "Ohoo TANU yajenga nchi".