Lipumba: Sikubaliani na baadhi ya maamuzi yaliyofanyika ndani ya CUF!

Dr Matola PhD

JF-Expert Member
Oct 18, 2010
56,492
92,970
Jamani wakuu mwenye kujuwa maana haambiwi maana, hapa Lipumba anaonesha wazi kwamba yeye ni mwenyekiti jina tu hana mamlaka yote ndani yya Cuf isipokuwa Maalim Seif. ebu jisomee mwenyewe.

Lipumba ammaliza Hamad

na Nasra Abdallah | Tanzania Daima

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, ameunga mkono uamuzi wa kumvua uanachama Mbunge wa Wawi Hamad Rashidi Mohamed.

Akizungumza na waandishi habari jana ofisi za makao makuu ya chama hicho, Buguruni Dar es Salaam, Profesa Lipumba, alisema analazimika kuunga mkono maamuzi hayo kutokana na ukweli kwamba yalitolewa Mkutano wa Halmashauri Kuu.

Hata hivyo Lipumba ambaye kauli yake ilikuwa ikisubiriwa kwa hamu kubwa na wanachama kuhusiana na suala hilo, alikiri kutopendezwa na kukubaliana na baadhi ya maamuzi yanayofanyika ndani ya chama, lakini kwa kuwa yameafikiwa na wengi yeye hana budi kuungana nao.

Japokuwa mwenyekiti huyo hakuwa wazi kutaja ni maamuzi gani ambayo hayakumpendeza alisema anawajibika kuyaheshimu kwa kuwa yalifuata katiba.

Alisisitiza kwamba ndani ya chama lazima kuwe na nidhamu hivyo ambaye anaona hawezi kufuata yale yaliyokubaliwa na chama ni vyema akajiondoa mwenyewe.

Alisema jambo la msingi kwao ni kujenga chama imara na chenye nidhamu na kuongeza kwamba siasa haiko makao makuu ya CUF ila iko katika maeneo ambayo watu wanatoka.

Alipoulizwa swali kama haoni chama chake kimekataa mabadiliko kama yale ambayo yalijaribu kufanywa na vijana wa chama cha Kikoministi cha China mwaka 1989 cha kutaka vijana kushika uongozi ambapo walitishwa kutokana na jaribio hilo.

Profesa huyo anasema kwa CUF mabadiliko hayo ni tofauti na hayo ya China kwa madai kwamba hao wanaotaka kugombea uongozi ndani ya chama hicho wana umri sawa na yeye na sio vijana.

Katika hili alisisitiza kwamba ni vyema wanaotaka kugombea wasubiri muda ukifika wa kufanya hivyo kujitokeza kwani uongozi uliopo sasa bado haujamaliza muda wake.

“Jamani muda ukifika wa kufanya hivyo hakuna mtu atakayekataliwa kwani ni haki ya kikatiba, mbona katika kuelekea uchaguzi mkuu uliopita kuna baadhi ya wanachama walijitokeza kugombea nafasi ya urais kwenye kura za maoni na hakuna aliyepingwa?” alihoji Profesa Lipumba.

Kuhusu kujiengua kwa baadhi ya wanachama katika chama hicho na kuanzishwa kwa chama kipya cha Alliance Democratic for Change (ADC), Lipumba alisema jambo hilo halimpi wasiwasi kwa kuwa kila mtu ana uhuru wake na wananchi ndiyo watakaoweza kupima chama kipi wanachoona kina uwezo wa kuwaongoza.

Safari yake nchini Marekani
Akizungumzia safari yake ya Washington nchini Marekani, ambayo alikaa huko kwa takriban miezi mitano, alikokwenda kwa ajili ya kufanya utafiti kuhusu demokrasia na maendeleo, utafiti ambao ulilenga kuleta demokrasia itakayoleta maendeleo na ajira katika nchi za Afrika, alisema katika utafiti alipata nafasi ya kutoa mjadala kuhusu miaka 50 ya Uhuru Tanzania na hatua ya maendeleo ambayo nchi imeifikia.

Kwa mujibu wa profesa huyo, miaka 200 ndiyo miaka ya maendeleo ya kisiasa, lakini cha kushangaza sasa hivi nchi iko katika robo ya miaka hiyo 200 ya maendeleo lakini asilimia 70 ya wananchi wake wanatumia chini ya dola moja huku mkazi wa Dar es Salaam ambaye anahesabiwa ndiye tajiri ana uwezo wa kupata sh 650 kwa siku.

Alisema suala la kuendelea uchumi na demokrasia linaenda pamoja hii ikiwa ni pamoja na wananchi kupata fursa ya kuikosoa serikali, kuchagua viongozi wanaowataka na kuwawajibisha.

Mapendekezo yaliyofikiwa katika utafiti huo wa uchumi duniani, Profesa Lipumba alisema aliona kuna haja ya kuwa na asasi muhimu zitakazowezesha uhuru wa wananchi kujieleza na kuikosoa serikali.

Pia mapendekezo mengine ni kuwepo kwa Tume Huru ya Uchaguzi na asasi huru ya kupambana na rushwa kwa kuwa Takukuru haina uwezo ikizingatiwa kwamba haiwezi kumpeleka mtuhumiwa wa rushwa mahakamani mpaka Mkurugenzi wa Mashtaka ya Jinai atie saini jambo linalorudisha nyuma juhudi za kupambana na rushwa.

Vilevile utafiti huo ulitaka kuwepo kwa asasi huru ya kukusanya fedha itakayofanya kazi kwa uwezo na uwazi zaidi na kuwa na matumizi mazuri ya fedha zitakazopatikana katika makusanyo hayo.

“Katika hili wananchi wa Tanzania wanaweza kufunguliwa kila mmoja akaunti yake bila kujali ni mtoto au mkubwa ambapo rasilimali zote kama gesi, mafuta na madini kiasi cha mapato yake kinagawiwa kwa kuweka katika kila akaunti ya mwananchi na makato ya kodi yanatolewa humohumo hali itakayofanya kila Mtanzania kufaidika na rasilimali zilizopo badala ya sasa hivi rasilimali hizo kufaidiwa na wachache.
 
Hongera mwenyekiti, wasio na nidhamu wana haki ya kutimka wanaweza kwenda chadem au cdc whetever...
 
Hongera mwenyekiti wenye wivu mapofu yanawatoka..

Endelea kurekebisha chama wasio na nidhamu wanaweza kwenda chadema (bingwa wa kupokea makapi, shibuda, lwakatere safari etc..

Jenga chama prof.
 
Hongera mwenyekiti wenye wivu mapofu yanawatoka..

Endelea kurekebisha chama wasio na nidhamu wanaweza kwenda chadema (bingwa wa kupokea makapi, shibuda, lwakatere safari etc..

Jenga chama prof.
Tambwe Hiza, Aman Walid Kaborou, Fatma Maghimbi & co.
 
Hongera mwenyekiti wenye wivu mapofu yanawatoka..

Endelea kurekebisha chama wasio na nidhamu wanaweza kwenda chadema (bingwa wa kupokea makapi, shibuda, lwakatere safari etc..

Jenga chama prof.
Hivi... Kuhama chama ni ukapi? Au kufikiri kuwa wanaohama chama ni makapi, NI UKAPI? Unaposikia wanachama kadhaa wamerudisha kadi na kuhamia chama kingine maana yake wametumia uhuru wao wa kujiunga na kundi lolote bila kuvunja sheria
 
Lipumba(34).jpg


Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, akifungua mkutano wa Baraza Kuu la Uongozi wa chama hicho jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Katibu Mkuu wa chama hicho ambaye pia ni Makamu wa

Kwanza wa Rais Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad. (PICHA: OMAR FUNGO)



Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, amesema maamuzi ya Baraza Kuu la Uongozi wa CUF kumvua uanachama Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed, na wenzake, yalikuwa ni mepesi kwa sababu chama hicho kimekwishafanya maamuzi magumu zaidi kuliko hilo.

Alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akifungua kikao cha siku mbili cha kawaida cha Baraza Kuu la Uongozi la CUF Taifa, jijini Dar es Salaam.

“Hili lilikuwa jepesi kulinganisha na maamuzi magumu ambayo tuliyafanya mwaka 2001 wakati Katibu Mkuu alipokuwa nje ya nchi. Maamuzi ya kufanya maandamano ya kudai katiba mpya, kudai tume huru ya uchaguzi, kudai utawala

bora na uchaguzi wa Zanzibar wa mwaka 2000 urejewe,” alisema na kuongeza: “Yalifanywa chini ya uongozi wangu wakati Katibu Mkuu hakuwapo.”

Alisema maandamano hayo ya mwaka 2001, pamoja na kuwapoteza wahanga wa demokrasia, ndiyo yaliyoanza kujenga misingi mpaka hatimaye wakaweza kufikia maridhiano ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Mwenyekiti wa CUF, Machano Khamisi, alisema CUF imejipanga kuhakikisha inawashinda maadui wa chama hicho.
Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, alimhakikishia Profesa Lipumba kuwa CUF iko imara na kwamba bado

iko ngangari kinoma kama alivyoiacha kabla ya kuondoka nchini au zaidi ya hapo.
Hata hivyo, Maalim Seif alisema changamoto inayoikabili CUF hivi sasa, ni kuendeleza moto uliowashwa ili wafike

mwaka 2015 katika joto lile lile ambalo hivi karibuni lilianzishwa na ujio wa Profesa Lipumba kutoka nje ya nchi.
Mapema, Profesa Lipumba alisema CUF inazingatia na kutetea maslahi ya wanyonge, na kwamba itaendelea kufanya hivyo bila kujali maslahi ya mtu binafsi.

Profesa Lipumba alisema Tanzania imebarikiwa kuwa na rasilimali nyingi, ikiwamo ardhi yenye rutuba, madini, gesi asilia, bandari na jiografia yake kwa ujumla ambavyo alisema iwapo vitatumika vizuri, wananchi wanaweza kunufaika na kupunguza tatizo la umaskini linalowakabili.

Alikemea siasa za udini ambazo alisema hazina mustakbali mwema katika kuwaunganisha Watanzania na kuwaletea maendeleo.




CHANZO: NIPASHE
 
Mimi ninavyofikiri kuwa kuna kiwango Fulani cha elimu MTU akifikia kwanza haongopi, pili anasimamia Yale ambayo anayaamini sasa basi ni Lipumba huyu huyu aliyefanya Press na waandishi akasema maamuzi mengine yanakera?!
 
Mimi ninavyofikiri kuwa kuna kiwango Fulani cha elimu MTU akifikia kwanza haongopi, pili anasimamia Yale ambayo anayaamini sasa basi ni Lipumba huyu huyu aliyefanya Press na waandishi akasema maamuzi mengine yanakera?!

Yaani angebaki kwenye fani yake asingekuwa muongo kama alivyo leo.. Halafu jamani wameona raisi gani duniani Profesa..? Au mwenyekiti wa chama cha siasa..?
 
Huyu Lipumba ananifurahisha sana. Anamsema sana Kikwete kwa kusafiri lakini yeye kama mwenyekiti wa chama (tena kilicho madarakani huko Zanzibar) anapotea kimoja kwa miezi! Ukiangalia sana ni afadhali Kikwete anayeenda kwa siku 5 -8 anarudi, Lipumba yeye ni miezi!

Tukumbuke huyu ni mwenyekiti wa chama, sio mwanachama wa kawaida. Kwanini asiamue moja, siasa au kazi zake za nje! Kwa mtaji huo nani anaweza kusema angekuwa rais huyu Lipumba ataacha kutokomea huko majuu wananchi watamuona mara moja kila baada ya miezi minne? Mwenyekiti wa msimu = rais wa msimu!
 
Yaani angebaki kwenye fani yake asingekuwa muongo kama alivyo leo.. Halafu jamani wameona raisi gani duniani Profesa..? Au mwenyekiti wa chama cha siasa..?

Dogo una umri gani na elimu gani? Fanya utafiti kabla hujaropka! Bingu wa Mutharika ni Prof, Rais wa Malawi na Mwenyekiti wa Chama.
 
Mimi ninavyofikiri kuwa kuna kiwango Fulani cha elimu MTU akifikia kwanza haongopi, pili anasimamia Yale ambayo anayaamini sasa basi ni Lipumba huyu huyu aliyefanya Press na waandishi akasema maamuzi mengine yanakera?!
Masikini HR umechinjiwa baharini!!!!!!!!!! Na media hazikutaki tena! Kashitaki kwa Pinda!
 
Dogo una umri gani na elimu gani? Fanya utafiti kabla hujaropka! Bingu wa Mutharika ni Prof, Rais wa Malawi na Mwenyekiti wa Chama.

Umeona huo upuuzi alioufanya malawi..? ilifikia wakati Malawi kwa karibu wiki mbili ilikuwa haina baraza la mawaziri..! Ungeshirikisha uzee na usomi wako kwenye kufikiri ungegundua Hilo.. My point ni kwamba ukishakuwa Profesa huwezi kuwa kiongozi wa nchi au chama cha siasa.. umenipata msomi mtu mzima..?
 
Back
Top Bottom