Lipumba: CCM inaendesha nchi kibabe

Luteni

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
2,274
301
Tanzania Daima

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba amesema Chama cha Mapinduzi (CCM) kinaendesha nchi kibabe bila kuheshimu uhuru wa mahakama.
Akihutubia mkutano wa hadhara juzi katika viwanja vya Kiwalani, Dar es Salaam, baada ya kuwashukuru wananchi wa eneo hilo kwa kuwachagua Wenyeviti wa Serikali za Mitaa kupitia CUF, Profesa alisema CCM imeshindwa kuonyesha demokrasia kwa vile imekuwa ikiingilia mambo mengi ya kisheria.
Lipumba alisema Mahakama Kuu iliamua kuwepo na mgombea binafsi lakini kutokana na uoga CCM imekataa kwa vile inahofia kupoteza madaraka.
“Kama kungekuwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) huru na yenye haki hata chaguzi ndogo sita zilizowahi kufanyika ilitakiwa mgombea binafsi aruhusiwa kugombea!” alisema Lipumba.
Kuhusu suala la ufisadi, alisema anashangazwa na jinsi wabunge wachache waliojiita wapambanaji walivyoshindwa kumaliza suala la kampuni ya kuzalisha umeme wa dharura ya Richmond hadi Bunge kuamua kufunga mjadala huo.
Kuhusu sakata la rada, Profesa Lipumba alisema aliyekuwa Waziri wa Miundombinu Andrew Chenge ndiye anayehusika lakini katika hali ya kushangaza ameendelea kushika madaraka ndani ya CCM badala ya kufikishwa mahakamani.
 
MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba amesema Chama cha Mapinduzi (CCM) kinaendesha nchi kibabe bila kuheshimu uhuru wa mahakama.
Sahihisho:MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF),anaetambuliwa na Msajili, Profesa Ibrahim Lipumba amesema ............
Profesa alisema CCM imeshindwa kuonyesha demokrasia kwa vile imekuwa ikiingilia mambo mengi ya kisheria
Hivi kuvamia ofisi za CUF na kuvunja kufuli ndio njia sahihi za Profesa kuonyesha demokrasia kwa vile amekuwa hakuingilia mambo ya kisheria
hali ya kushangaza ameendelea kushika madaraka ndani ya CCM badala ya kufikishwa mahakamani.
Hali ya kushangaza Profesa Lipumba ameendelea kushika madaraka ndani ya CUF licha ya kujiuzulu na kuufukuzwa, badala ya kujiunga na chama kinachomfadhili?
 
Tanzania Daima

MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba amesema Chama cha Mapinduzi (CCM) kinaendesha nchi kibabe bila kuheshimu uhuru wa mahakama.
Akihutubia mkutano wa hadhara juzi katika viwanja vya Kiwalani, Dar es Salaam, baada ya kuwashukuru wananchi wa eneo hilo kwa kuwachagua Wenyeviti wa Serikali za Mitaa kupitia CUF, Profesa alisema CCM imeshindwa kuonyesha demokrasia kwa vile imekuwa ikiingilia mambo mengi ya kisheria.
Lipumba alisema Mahakama Kuu iliamua kuwepo na mgombea binafsi lakini kutokana na uoga CCM imekataa kwa vile inahofia kupoteza madaraka.
“Kama kungekuwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) huru na yenye haki hata chaguzi ndogo sita zilizowahi kufanyika ilitakiwa mgombea binafsi aruhusiwa kugombea!” alisema Lipumba.
Kuhusu suala la ufisadi, alisema anashangazwa na jinsi wabunge wachache waliojiita wapambanaji walivyoshindwa kumaliza suala la kampuni ya kuzalisha umeme wa dharura ya Richmond hadi Bunge kuamua kufunga mjadala huo.
Kuhusu sakata la rada, Profesa Lipumba alisema aliyekuwa Waziri wa Miundombinu Andrew Chenge ndiye anayehusika lakini katika hali ya kushangaza ameendelea kushika madaraka ndani ya CCM badala ya kufikishwa mahakamani.
Ahhhhhhhhhh nikajua habar ya leo kumbe toka 2010 basi sawa
 
Nilitaka kushangaa,maana ubabe wa CCM ndio umempa chama ikiwemo kumsaidia kuvunja ofisi,kulala ndani ya ofisi,ruzuku na hata kwenda ikulu kuteta na Magu kila akijisikia!!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom