MWENYEKITI wa Tume ya Uchaguzi Nchini Jaji Mstaafu Lewis Makame amesema iwapo Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF Profesa Ibrahim Lipumba anamtaka yeye ajiuzulu wadhifa wake ni vema akaanza yeye kufanya hivyo.
Kauli hiyo ya Jaji Makame inakuja kutokana na Mwenyekiti huyo wa CUF kumtaka ajiuzulu kwa madai kuwa hana jipya la kusaidia vyama vya siasa na wananchi wanaotaka mageuzi tofauti na kulinda maslahi ya Chama Tawala cha CCM.
Jaji Makame alisema hajaona sababu ya yeye kujiuzulu kwani anaamini kuwa yeye ni mwadilifu na anatekeleza kazi zake kwa mujibu wa katiba na sheria zilizipo.
Mwenyekiti huyo wa Tume ya Uchaguzi alisema suala la mtu kukosea lipo kwa binadamu yoyote lakini kwa upande wake haamini kwamba amefanya makosa ya kumlazimu ajiuzulu wazifa wake.
Alisema Lipumba anapaswa kuonyesha mfano yeye kutokana na ukweli kwamba ameshiriki katika chaguzi mbalimbali zaidi ya mara tatu bila kushinda hivyo hana jipya lolote kwa chama chake.
Mwenyekiti huyo alisema Profesa Lipumba amekuwa akitumia hoja hiyo ya kumtaka kujiuzulu kwa kuwahadaa wanachama wa chama hicho ambao wameshindwa kubaini udhaifu wa kiongozi wao.
Source: Nifahamishe.com
Kauli hiyo ya Jaji Makame inakuja kutokana na Mwenyekiti huyo wa CUF kumtaka ajiuzulu kwa madai kuwa hana jipya la kusaidia vyama vya siasa na wananchi wanaotaka mageuzi tofauti na kulinda maslahi ya Chama Tawala cha CCM.
Jaji Makame alisema hajaona sababu ya yeye kujiuzulu kwani anaamini kuwa yeye ni mwadilifu na anatekeleza kazi zake kwa mujibu wa katiba na sheria zilizipo.
Mwenyekiti huyo wa Tume ya Uchaguzi alisema suala la mtu kukosea lipo kwa binadamu yoyote lakini kwa upande wake haamini kwamba amefanya makosa ya kumlazimu ajiuzulu wazifa wake.
Alisema Lipumba anapaswa kuonyesha mfano yeye kutokana na ukweli kwamba ameshiriki katika chaguzi mbalimbali zaidi ya mara tatu bila kushinda hivyo hana jipya lolote kwa chama chake.
Mwenyekiti huyo alisema Profesa Lipumba amekuwa akitumia hoja hiyo ya kumtaka kujiuzulu kwa kuwahadaa wanachama wa chama hicho ambao wameshindwa kubaini udhaifu wa kiongozi wao.
Source: Nifahamishe.com