Lipi ni lengo la speaker kutimua wapinzani bungeni?

sindano butu

JF-Expert Member
Aug 20, 2012
503
157
Mbunge wa jimbo ni mtu mkubwa sana na ameenda bungeni kuwakilisha na kutetea masilahi ya wananchi wake. Lakini mbunge akifika bungeni kwenye kutetea maslahi ya wananchi anapata kikwazo cha kutokuwa huru na dikteta spika ndugai hapa tanzania.

Labda niulize wadau spika anakuwa na lengo gani kutokuheshimu wapinzani na kutoa sana vitisho utazania yeye ndo alimleta mbunge bungeni. Mi nafikiri spika analenga kuwanyima wananchi haki zao wa jimbo fulani wa mbunge aliyefukuzwa kwani yeye amejiona ndo mwenye madaraka kumleta bungeni mbunge.

Kwakweli hili haliko sawa maana inaharibu demokrasia na kuwafanya wabunge wajione hawathaminiki kwenye kutoa michango. NATAKA NIMUAMBIE SPEAKER IPO SIKU ATALIPA HAKI ZA WABUNGE ZINAZOPOTEA HATA KWA NJIA MBAYA IKISHINDIKANA. Na kama ndugai anataka ccm itawale nchi milele sio fare kabisa kwani ushindani wowote duniani huwa kuna kurithishana ushindi kama fareness ipo.

Speaker lazima aelewe kuwa kwenye kutoa hoja lazima ubishi na ugomvi utokehe kama maneno yakitolewa ni makali na si busara kutumia ubavu kwani huaribu utamu wa hoja zinazozungumzwa. Lazima aelewe kuwa vijana hawawezi kuongea kama wazehe na wazehe hawawezi kuongea kama vijana kwani hawako sawa kimtazamo na ikitokea ugomvi ni jukumu la speaker kusululisha na sikwa kufukuza wapinzani.

Nataka speaker ajitambue NA AJIELEWE KUWA CHEO SI CHA KUDUMU NI MPITO NA KUNA MAISHA BAADA YA CHEO NA NI VIZURI SANA KUONGEZA MARAFIKI NA NI UPUMBAVU SANA KUONGEZA MAADUI.
 
mada nzuri ,tatizo tunarudi pale pale katiba ipo ila watawala wanaitumia tu pale inapokidhi matakwa yao,spika anaongozwa na sheria anapokuwa anaendesha vikao hivi na tunamtegemea kuwa always he must apply his mind anapotoa uamuzi sio jaziba au kupendelea chama chako,angalia bunge la pale SA sheria zao hazitofautiani sana na za kwetu ila spika wao hakurupuki kutoa uamuzi wa kuwafukuza nje ya kikao wabunge au mbunge asiyefuata sheria za bunge,na elewa hii sheria ya kumsimamisha mbunge kwa muda mrefu sijui anatoa wapi,ni vema spika WETU akatembelea bunge la Namibia na SA aone wenzake wana kabiliana vipi na changamoto za mabunge ya vyama vingi.I can put my head on the block spika wetu huyu wa sasa hata bunge la chama kimoja lingemshinda.
 
"Anawatoa nje ili wakose kinga halafu boss atawashughulikia nje " kama alivosema mwenyewe
 
mada nzuri ,tatizo tunarudi pale pale katiba ipo ila watawala wanaitumia tu pale inapokidhi matakwa yao,spika anaongozwa na sheria anapokuwa anaendesha vikao hivi na tunamtegemea kuwa always he must apply his mind anapotoa uamuzi sio jaziba au kupendelea chama chako,angalia bunge la pale SA sheria zao hazitofautiani sana na za kwetu ila spika wao hakurupuki kutoa uamuzi wa kuwafukuza nje ya kikao wabunge au mbunge asiyefuata sheria za bunge,na elewa hii sheria ya kumsimamisha mbunge kwa muda mrefu sijui anatoa wapi,ni vema spika WETU akatembelea bunge la Namibia na SA aone wenzake wana kabiliana vipi na changamoto za mabunge ya vyama vingi.I can put my head on the block spika wetu huyu wa sasa hata bunge la chama kimoja lingemshinda.
Ndugai hashauliki yule
 
Hongera spika kubadirika watu watakupenda kwa kurinda demokrasia na kuachana na uchwara dikteta.
 
Back
Top Bottom