Lipi jema, kuanzisha chama kipya cha siasa au kujiunga na chama cha siasa kilichopo?

Onambali

Member
Mar 11, 2011
67
10
Wana JF,
Nawasalimu.

Baada ya kutangaza nia yangu ya kuomba ridhaa ya kuwa rais wa nchi yetu mwaka 2030, nimeulizwa maswali mengi sana mojawapo nilitakiwa nitaje chama changu cha siasa.
Kusema kweli kabisa, mimi bado sijawa mwanachama wa chama chochote cha siasa.
Mheshimiwa rais wa kwanza wa Tz, Dr JK Nyerere, aliwahi kusema ‘kama ukichota maji kwa kikombe kutoka kwenye dimbwi halafu uyafanyia utafiti wa kichambuzi, maji yale yatakuwa sawa na yale yaliyobaki kwenye dimbwi’ . Kama kauli hii ni ya kweli, basi fananisha viongozi wetu wa siasa na maji ndani ya kikombe yaliyochotwa kutoka kwenye dimbwi (jamii). Ukifananisha hivyo utaona kwamba, tatizo kubwa nchini kwetu ni kukosekana kwa utu, utashi, uzalendo, ubunifu, maono, maadili, ukweli na haki ndani ya jamii nzima. Matokeo yake ni kwamba sampuri (kiongozi) anayetokana na jamii husika huwa na mawazo ya kisanii maana jamii imejitwika usanii katika ngazi zote za kiutawala kuanzia kwa baadhi ya wakuu wa kaya mbalimbali kuwa wasanii hata kwa wenzi wao, watoto wao, nk.
Nina mengi ya kutengenza nchini kwetu. Lazima tujenge jamii inayojitambua, inayojithamini, inayojiamulia, inayojiheshimu, isiyojisanii, inayolinda utaifa wao kuwa urithi wa vizazi vya leo na vile vijavyo, na inayofahamu uhuhimu wa kila raia wake.
Baada ya kusema haya, nafikiri sasa kujiunga au kuanzisha chama cha siasa ili nianze rasmi mbio za kudai uhuru wa kweli wa mtanzania kutoka kwa wakoloni wakuu yaani umaskini wa kufikiri, magonjwa ya kufikiri na ujinga ulioganda vichwani kwa watu bila kujali nyadhifa , shahada walizo nazo hata kama ziwe za heshima au za kusoma, nk.

Naomba ushauri wenu great thinkers, lipi jema, kuanzisha chama cha siasa kipya au kujiunga na chama cha siasa ambacho tayari kimesajiliwa tayari? Kama ukinishauri nijiunge na chama cha siasa naomba pia uniambie kipi na kwanini.
Asanteni sana wana JF.
Onambali, rais mtarajiwa 2030.
 
wana jf,
nawasalimu.

baada ya kutangaza nia yangu ya kuomba ridhaa ya kuwa rais wa nchi yetu mwaka 2030, nimeulizwa maswali mengi sana mojawapo nilitakiwa nitaje chama changu cha siasa.
kusema kweli kabisa, mimi bado sijawa mwanachama wa chama chochote cha siasa.
mheshimiwa rais wa kwanza wa tz, dr jk nyerere, aliwahi kusema ‘kama ukichota maji kwa kikombe kutoka kwenye dimbwi halafu uyafanyia utafiti wa kichambuzi, maji yale yatakuwa sawa na yale yaliyobaki kwenye dimbwi’ . Kama kauli hii ni ya kweli, basi fananisha viongozi wetu wa siasa na maji ndani ya kikombe yaliyochotwa kutoka kwenye dimbwi (jamii). Ukifananisha hivyo utaona kwamba, tatizo kubwa nchini kwetu ni kukosekana kwa utu, utashi, uzalendo, ubunifu, maono, maadili, ukweli na haki ndani ya jamii nzima. Matokeo yake ni kwamba sampuri (kiongozi) anayetokana na jamii husika huwa na mawazo ya kisanii maana jamii imejitwika usanii katika ngazi zote za kiutawala kuanzia kwa baadhi ya wakuu wa kaya mbalimbali kuwa wasanii hata kwa wenzi wao, watoto wao, nk.
nina mengi ya kutengenza nchini kwetu. Lazima tujenge jamii inayojitambua, inayojithamini, inayojiamulia, inayojiheshimu, isiyojisanii, inayolinda utaifa wao kuwa urithi wa vizazi vya leo na vile vijavyo, na inayofahamu uhuhimu wa kila raia wake.
baada ya kusema haya, nafikiri sasa kujiunga au kuanzisha chama cha siasa ili nianze rasmi mbio za kudai uhuru wa kweli wa mtanzania kutoka kwa wakoloni wakuu yaani umaskini wa kufikiri, magonjwa ya kufikiri na ujinga ulioganda vichwani kwa watu bila kujali nyadhifa , shahada walizo nazo hata kama ziwe za heshima au za kusoma, nk.

naomba ushauri wenu great thinkers, lipi jema, kuanzisha chama cha siasa kipya au kujiunga na chama cha siasa ambacho tayari kimesajiliwa tayari? Kama ukinishauri nijiunge na chama cha siasa naomba pia uniambie kipi na kwanini.
asanteni sana wana jf.
onambali, rais mtarajiwa 2030.


achana na siasa
 
Utajinadi kama mgombea binafsi,tutakuwa tumeshabadilisha katiba na kuweka hicho kipengele,nitakuwa compaign manager wako
 
Una malengo huna mkakati, huna haja ya kuanzisha chama ukaenda kuongeza walaji wa ruzuku (kodi zetu)kwa kua tayari viko vyama vyenye mtazamo wakoa, jiunge na chama chochote kinachokufaa ni dalili ya ukomavu na uzoefu wa siasa, kutaka kuanzisha chama chako mwenyewe imekaa kibibafsi sana kana kwamba una maslahi fulani hivi!
 
inaonekana kijana ni mtu sana wa sound, angalia usije ukawa kama hawa wanasiasa wanaopopolewa mawe kwa sasa. Kama vp utapima mwenyewe kuanzisha chama au kujiunga na vyama viliopo, kila la heri kijana katika mbio zako za urais 2030.
 
Waheshimiwa, Lakini, Plawala, Revolutionary na mkuu wa chuo, nashukuruni, naheshimu maoni yenu, nasubiri maoni zaidi kutoka kwa great thinkers wengi.
 
jiunge na cuf au nccr ili uifufue, au jiunge na ccm ili uvae magamba na kujivua halafu wao ndio watabaki nayo maana yamekomaa. Una sound mpaka basi kijana
 
Jiunge na yule bwana anaevaa kofia km askari wa vietnam mwenye chama cha mfukoni au jiunge na Makaidi!
 
Hoja yako inakinzana sana na matamanio yako.Kama unakiri kuwa tatizo ni la jamii nzima(usanii,kukosa uadilifu,uzalendo nk...)basi na wewe ni sehemu ya jamii hiyo,au unadhani kuwa wewe nini kinakutofautisha na wengine wote? i doubt if you are a presidential material.
 
Back
Top Bottom