Debby the FEMINIST
Member
- May 4, 2020
- 32
- 37
Mkuu wa wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi Hashim Komba ameitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU wilayani humo kufanya uchunguzi wa matumizi mabaya ya fedha kiasi cha shilingi milioni 18 zilizotumika kwenye mradi wa Usafi na Mazingira (WASH) wilayani humo ambapo ni Ununuzi wa pikipiki 2 kwa shilingi milioni 11 na Ununuzi wa Mafuta ya Milioni 7 yaliyotumika ndani ya siku 4
Komba ametoa agizo hilo baada ya ziara yake katika Zahanati ya Mkotokuyana, Ikungu, Tunduru ya Leo na hospitali ya wilaya ya Nachingwea ambapo pia amewataka watumishi wote waliochukua fedha kwa ajili ya kufuatilia utekelezaji wa mradi huo kuzirejesha mara moja sababu ikiwa ni kutoifanya kazi na kupelekea mradi kutokamilika kwa wakati.
Komba ametoa agizo hilo baada ya ziara yake katika Zahanati ya Mkotokuyana, Ikungu, Tunduru ya Leo na hospitali ya wilaya ya Nachingwea ambapo pia amewataka watumishi wote waliochukua fedha kwa ajili ya kufuatilia utekelezaji wa mradi huo kuzirejesha mara moja sababu ikiwa ni kutoifanya kazi na kupelekea mradi kutokamilika kwa wakati.