Mwanashheria njaa
JF-Expert Member
- Sep 24, 2018
- 1,791
- 2,320
Hivi Magdalena Sakaya alifiaga wapi
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Usiku saa 7. Mbona hawapo kituo chochote cha polisi? Jambo gani lingine unalolijua polisi wakafanikisha tofauti na kusimamia mwenge?Msiwe mnakimbilia upotoshaji wa habari muwe wakweli hao watakuwa na makosa yao husika na wamekamatwa kwa jinai.
CUF haina impact yoyote hadi kupelekea kutekwa wafuasi wake.
Usikute ndio baadhi ya watanzania waliokuwa msumbiji na wamechukuliwa na kikosi kazi.
umechanganya mambo mengi kwenye uzi mmojaMuendelezo wa awamu iliyopita, halafu yule jamaa mwingine anasema sasa hivi hatapinga kama mwanzo, siasa ikitumika kama kitega uchumi ni hatari sana kwa usalama wa taifa na watu wake.
Baada ya siku kadhaa kelele zikizidi utasikia wamefikishwa mahakamani, kama shida yao ni kuwapeleka mahakamani kwanini kutekana usiku na silaha nzito? naona hawa askari wetu wanatamani vita, vyema wapelekwe Msumbiji wakasaidie huko.
Yes, mambo mengi yenye uhusiano kwenye uzi mmoja, fungua akili yako vizuri utagundua.umechanganya mambo mengi kwenye uzi mmoja
Wewe ndio hufuatilii, kama kuna eneo CUF ilibaki intact basi ni kusini. Hakuna defection za maana Lindi,Mtwara na Ruvuma kwenda ACT ukiachana na Mhe.Bwege tu. Wabunge ama wagombea wengi wa 2015 Wengi walibaki CUF ama kurejea CCM so ACT bado kupata numbers za CUF kule kusini.Bro...asikudanganye mtu, hakuna CUF kusini labda kidogo ungesema ACT. Watu wa kusini na siasa zao ni tofauti na tunavyofikiri... hakuna kitisho cha CUF kusini labda asikudanganye mtu.
kesi ya mbowe 2020 amekuja kukamatwa 2021, labda hili litapata suluhu 2022.Waulizwe Sirro, Kingai na Mahita. Wanauelewa zaidi na genge hili.
kesi ya mbowe 2020 amekuja kukamatwa 2021, labda hili litapata suluhu 2022.
HakikaYes, mambo mengi yenye uhusiano kwenye uzi mmoja, fungua akili yako vizuri utagundua.
Ugonjwa wa magazeti ya siku hiziKaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, Foka Dinya amekiri kutokea kwa tukio hilo akisema kwamba Jeshi la Polisi linaendelea na uchaguzi.
"Jeshi la polisi linaendelea na uchaguzi ili kubaini chanzo cha tukio na kujua wapi waliko" amesema Kamanda Dinya
Chanzo: Mwananchi
Hivi hawa majambazi wanaovaa uniform wanataka kulipeleka wapi Taifa hili? Division 4 point 32 ndiyo tabu yakeNi huko mkoani Lindi inasemekana wanaCuf hao walivamiwa makwao na watu waliokuwa wamejihami kwa siraha nzito na kutokomea nao kusikojulikana.
---
Watu watano wakazi wa Kijiji cha Rutamba Halmashauri ya Mtama wanadaiwa kuwa ni wanachama wa Chama cha Wananchi (CUF), wamepotea tangu Oktoba 30, 2021.
Katibu wa CUF Wilaya ya Lindi, Shadhil Bosha amesema kuwa watu hao waliopotea ni wanachama wa chama hicho akidai kuwa walichukuliwa na watu wasiojulikana nyumbani kwao Oktoba 30, 2021 saa saba usiku.
"Tunaliomba Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa haraka ili familia na jamii iondolewe hofu," amesema Bosha.
Bosha aliwataja watu hao wanaodaiwa kupotea kuwa ni pamoja na Musa Fukutu, Hamisi Liendeka, Shaziri Chileu, Baraka Ali na Isumail Yahaya.
Mke wa Ismail Yahaya, Husna Litapwachi amesema Oktoba30, 2021 saa saba usiku walisikia mlango uikgongwa na watu watano huku akidai kuwa wawili wakiwa na silaha waliingia chumbani na kuwakuta wamelala kitandani na kuwaamuru washuke chini .
Litapwachi anasema baada ya hapo walikusanya simu na wakaondoka na mumewe.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, Foka Dinya amekiri kutokea kwa tukio hilo akisema kwamba Jeshi la Polisi linaendelea na uchaguzi.
"Jeshi la polisi linaendelea na uchaguzi ili kubaini chanzo cha tukio na kujua wapi waliko" amesema Kamanda Dinya
Chanzo: Mwananchi
Alipigwa na moshi mzito kichwaniLindi cuf ni threat, au umesahau hta JPM hakurudi kufanya kampeni huko!!
Si alishasema kuwa yeye na yule dhalim ni kitu kimojaNiliona kwenye taarifa ya habari. Nikajisemea moyoni kuwa bado wasijulikana wapoo eeennhhh.