Lindi: Wanachama watano wa CUF wadaiwa kutekwa na watu wenye silaha usiku wa manane

Donnie Charlie

JF-Expert Member
Sep 16, 2009
15,082
16,116
Lindi. Watu watano wakazi wa Kijiji cha Rutamba Halmashauri ya Mtama wanadaiwa kuwa ni wanachama wa Chama cha Wananchi (CUF), wamepotea tangu Oktoba 30, 2021.

Katibu wa CUF Wilaya ya Lindi, Shadhil Bosha amesema kuwa watu hao waliopotea ni wanachama wa chama hicho akidai kuwa walichukuliwa na watu wasiojulikana nyumbani kwao Oktoba 30, 2021 saa saba usiku.

"Tunaliomba Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa haraka ili familia na jamii iondolewe hofu," amesema Bosha.

Bosha aliwataja watu hao wanaodaiwa kupotea kuwa ni pamoja na Musa Fukutu, Hamisi Liendeka, Shaziri Chileu, Baraka Ali na Isumail Yahaya.

Mke wa Ismail Yahaya, Husna Litapwachi amesema Oktoba30, 2021 saa saba usiku walisikia mlango uikgongwa na watu watano huku akidai kuwa wawili wakiwa na silaha waliingia chumbani na kuwakuta wamelala kitandani na kuwaamuru washuke chini .

Litapwachi anasema baada ya hapo walikusanya simu na wakaondoka na mumewe.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, Foka Dinya amekiri kutokea kwa tukio hilo akisema kwamba Jeshi la Polisi linaendelea na uchaguzi.

"Jeshi la polisi linaendelea na uchaguzi ili kubaini chanzo cha tukio na kujua wapi waliko" amesema Kamanda Dinya

Mwananchi
 
SIO KWELI, mbona nasikia mambo hayo yalishakomeshwa na mama?

Msimchafue mama, watu kupotea hakuna tena, wasiojulikana hawapo tena, UHURU wa habari na kujieleza bwerereeee, Pesa nje nje, YALIYOWASHINDA WATANGULIZI wake kwa miaka dahali, yeye kayapiga kwa miezi kadhaa tu, korona imeisha kwa chanjo, madarasa 15,000 yanaenda kumea kwa trilioni 1.4, SMZ imepata ndege 2 zilizozidi bajeti yao ya nchi ya miaka miwili, kodi ya tiaraei kubaki kwao, tenesko bara kuwahudumia visiwani bure n.k

Acheni wivu jamani, msimchafue mama kisa yeye ni mwenye jinsia ya KIKE.
 
CUF ilishakufa na Lipumba na Magdalena Sakaya hivyo sio tishio tena kwa serikali au chama chochote.
 
Uyo katibu taarifa ya wenzake kupotea kaitoa lini mbn wadau wamepotea toka 30 okt na uyo mama baada ya mumewe kuchukuliwa alichukua hatua gani tuanzie hapo kwanza
 
Lindi. Watu watano wakazi wa Kijiji cha Rutamba Halmashauri ya Mtama wanadaiwa kuwa ni wanachama wa Chama cha Wananchi (CUF), wamepotea tangu Oktoba 30, 2021.

Katibu wa CUF Wilaya ya Lindi, Shadhil Bosha amesema kuwa watu hao waliopotea ni wanachama wa chama hicho akidai kuwa walichukuliwa na watu wasiojulikana nyumbani kwao Oktoba 30, 2021 saa saba usiku.

"Tunaliomba Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa haraka ili familia na jamii iondolewe hofu," amesema Bosha.

Bosha aliwataja watu hao wanaodaiwa kupotea kuwa ni pamoja na Musa Fukutu, Hamisi Liendeka, Shaziri Chileu, Baraka Ali na Isumail Yahaya.

Mke wa Ismail Yahaya, Husna Litapwachi amesema Oktoba30, 2021 saa saba usiku walisikia mlango uikgongwa na watu watano huku akidai kuwa wawili wakiwa na silaha waliingia chumbani na kuwakuta wamelala kitandani na kuwaamuru washuke chini .

Litapwachi anasema baada ya hapo walikusanya simu na wakaondoka na mumewe.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, Foka Dinya amekiri kutokea kwa tukio hilo akisema kwamba Jeshi la Polisi linaendelea na uchaguzi.

"Jeshi la polisi linaendelea na uchaguzi ili kubaini chanzo cha tukio na kujua wapi waliko" amesema Kamanda Dinya.

Waulizwe Sirro, Kingai na Mahita. Wanauelewa zaidi na genge hili.
 
Ni huko mkoani Lindi inasemekana wanaCuf hao walivamiwa makwao na watu waliokuwa wamejihami kwa siraha nzito na kutokomea nao kusikojulikana.

---
Watu watano wakazi wa Kijiji cha Rutamba Halmashauri ya Mtama wanadaiwa kuwa ni wanachama wa Chama cha Wananchi (CUF), wamepotea tangu Oktoba 30, 2021.

Katibu wa CUF Wilaya ya Lindi, Shadhil Bosha amesema kuwa watu hao waliopotea ni wanachama wa chama hicho akidai kuwa walichukuliwa na watu wasiojulikana nyumbani kwao Oktoba 30, 2021 saa saba usiku.

"Tunaliomba Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa haraka ili familia na jamii iondolewe hofu," amesema Bosha.

Bosha aliwataja watu hao wanaodaiwa kupotea kuwa ni pamoja na Musa Fukutu, Hamisi Liendeka, Shaziri Chileu, Baraka Ali na Isumail Yahaya.

Mke wa Ismail Yahaya, Husna Litapwachi amesema Oktoba30, 2021 saa saba usiku walisikia mlango uikgongwa na watu watano huku akidai kuwa wawili wakiwa na silaha waliingia chumbani na kuwakuta wamelala kitandani na kuwaamuru washuke chini .

Litapwachi anasema baada ya hapo walikusanya simu na wakaondoka na mumewe.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, Foka Dinya amekiri kutokea kwa tukio hilo akisema kwamba Jeshi la Polisi linaendelea na uchaguzi.

"Jeshi la polisi linaendelea na uchaguzi ili kubaini chanzo cha tukio na kujua wapi waliko" amesema Kamanda Dinya

Chanzo: Mwananchi
 
Muendelezo wa awamu iliyopita, halafu yule jamaa mwingine anasema sasa hivi hatapinga kama mwanzo, siasa ikitumika kama kitega uchumi ni hatari sana kwa usalama wa taifa na watu wake.

Baada ya siku kadhaa kelele zikizidi utasikia wamefikishwa mahakamani, kama shida yao ni kuwapeleka mahakamani kwanini kutekana usiku na silaha nzito? naona hawa askari wetu wanatamani vita, vyema wapelekwe Msumbiji wakasaidie huko.
 
Muendelezo wa awamu iliyopita, halafu yule jamaa mwingine anasema sasa hivi hatapinga kama mwanzo, siasa ikitumika kama kitega uchumi ni hatari sana kwa usalama wa taifa na watu wake...

Hivi unafikiri CUF ina madhara gani kisiasa Tanzania mpaka wanachama wake kutekwa?..

Tujaribu kutoliweka kila jambo kwenye mlengo wa kisiasa, ili fikra zetu ziende mbali kidogo..
 
Back
Top Bottom