Lindi: RC Zainabu Telack ameagiza kuteketezwa kwa tani 24 za Korosho zilizopo Mtama

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,806
11,968
Mkuu wa mkoa wa Lindi Zainabu Telack akiwa kwenye kikao cha utekelezaji wa mpango wa kuboresha usimamizi wa huduma za ugani kwa wakulima wa korosho katika mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma na Pwani, ameagiza kuteketezwa kwa korosho tani 24 zilizopo ghala kuu la Mtama, lililopo halmashauri ya Mtama wilayani Lindi.

Hayo yamejiri baada ya Korosho hizo kupelekwa kwenye ghala kuu la hazina zikiwa na Grade One na Grade Two na baadae zikapoteza ubora na kushindwa kuuzika kwenye minada.

Sambamba na hilo Telack amewataka wakurugenzi wa halmashauri zote mkoa wa Lindi kuwawezesha maafisa ugani ili weweze kuwasaidia wakulima kwenye zao la korosho.

Chanzo cha habari Mashujaa FM
 
Mmh bora wangezifanyia recycle kama inawezekan ikazalisha kituingine..
wakifanya hivyo,utapunguza nguvu ya kurudisha kangomba (jokes). Hata hivyo, majivu yatayopatikana baada ya kuunguza korosho hizo yanaweza kurudishwa shambani na recycling itakuwa tayari.
 
Dah kuteketeza? Kisa zimekosa wateja? Hilo nalo ni kosa kubwa sana. Kwani vile viwanda vya kubangua korosho vimekwenda wapi? Si waziprocess wenyewe ziuzwe zilizobanguliwa na kama zitakosa mteja tena hata mashuleni na majeshini zinaweza kugawiwa watu wakazila wakapata afya. Agizo la mh mkuu wa mkoa sio la kiungwana kwani korosho ni chakula nahaijasemwa kuwa zimeharibika au hazifai kwa matumizi ya binadamu.

Ukiprocess korosho unapata korosho yenyewe na mafuta pia ambayo ni material.nzuri kwa viwanda vya plastic kwani ndio hupolish vyombo vya plastic sasa ukiteketeza unapata nini?
 
Umezipokea zikiwa daraja la 1 na 2 uhifadhi wa hovyo wa maghala umepelekea uharibifu wa korosho hakuna hatua za kuchukua (hata elimu ya uhifadhi ) unakimbilia kuteketeza

Hata kuwaza kuzifanya chakula cha mifugo hapana wewe n kuharibu tu
 
Back
Top Bottom