Lindi imeandaliwa vyema kuupokea mradi mkubwa wa Liqufied Natural Gas?

Philipo Khan

Member
May 14, 2016
37
44
Ni jambo la furaha sana kwa mkoa wa Lindi moja ya mikoa ya zamani iliyobakia nyuma kimaendeleo huenda kuliko mikoa yote iliyoanzishwa zamani.

Uwepo wa mradi huu mkubwa ambao utakua ni kivutio kikubwa cha viwanda mkoani Lindi ambavyo vitakua chachu ya maendeleo mkoani Lindi.

Hoja kubwa kwa wananchi wa Lindi je, wamejiandaa kuupokea mradi huu kinguvu kazi na uwekezaji wa kijasiliamali?

Ujio wa mradi huu utaenda sambamba na mahitaji makubwa ya nyumba za kupanga, vyakula kama nyanya, kuku, viazi, matikiti nk

Maana kutofanya hivyo kutasababisha watu wa mikoa mingine kuja kuchukua hizo fursa nanyi muendelee kubakia watazamaji wa maendeleo ya wenzenu

Kwa upande wa serikali imeanza kuandaa muindombinu ya nishati itakayohakikisha uhai wa viwanda hivyo?

Je wameandaa miradi ya maji toka kwenye vyanzo vya maji vya kudumu na uhakika? Maana viwanda bila maji ni kazi bure, hali ya upatikanaji wa maji mjini Lindi bado siyo nzuri, kuna mitaa ina miaka miwili mabomba yao hayajawahi kutoa maji.

Naunga mkono jitihada za serikali kuuweka mradi huo mkoani Lindi, eneo la likong'o ili kupunguza tofauti za kimaendeleo kati ya mikoa yake au ukanda na ukanda

Hongera Rais Kikwete, muasisi wa mradi huu.

Hongera Rais Magufuli mtekelezaji mkuu wa mradi huu
 
Jamani Lindi Jamani.Nilifika Lindi Mara yangu ya kwanza mwaka jana mwezi May.Niliipenda sana ile Mandhari yake.Lindi Kwa nchi zingine ni mahali Matajiri tuu ndiyo wanapaswa kuishi hapo.Lindi Mwenyezi Mungu kaipendelea sana.Ila tuu Wenyeji wa hapo wanashindwa kutumia fursa kibao tuu hapo.Ila Gesi irakapo fika hapo itakuwa ndiyo Chachu haswa kimaendeleo.
 
Jamani Lindi Jamani.Nilifika Lindi Mara yangu ya kwanza mwaka jana mwezi May.Niliipenda sana ile Mandhari yake.Lindi Kwa nchi zingine ni mahali Matajiri tuu ndiyo wanapaswa kuishi hapo.Lindi Mwenyezi Mungu kaipendelea sana.Ila tuu Wenyeji wa hapo wanashindwa kutumia fursa kibao tuu hapo.Ila Gesi irakapo fika hapo itakuwa ndiyo Chachu haswa kimaendeleo.
Unaongelea lindi ipi mkuu, hii ninayoishi mimi au,think big,lindi iko nyuma sana mfano wilaya ya liwale
 
Wabia wa mradi huo inaaminika wamebadiri nia yao na kwamba wanaangalia fursa nyingine nchini na nje ya nchi!
Tunachelewa mno kuchukua hatua na huenda ndio sababu iliyofanya Wahisani watulie kwanza. Kwakweli sielewi status ya mradi huu, tunajivuta mno wakati majirani zetu wa Msumbiji wanaendelea na ujenzi wa LNG terminal. Nasikitika sana kwa kukwama kwa mradi mkubwa kama huu wenye thamani takribani usd 32 bilio na vilivile kukwama kwa mradi mkubwa wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo wenye thamani zaidi ya usd 12 bilion. Nchi inahitaji kuwa na mega projects kama hizo kwa ajiri ya sasa na baadae. Yeyote anayejua juu ya mwelekeo wa mradi huu tafadhali tujuze.
 
Unaongelea lindi ipi mkuu, hii ninayoishi mimi au,think big,lindi iko nyuma sana mfano wilaya ya liwale
Lindi hiyo hiyo kaka wewe unayoishi hapo.Mimi Naishi Arusha.Lakini Lindi nimepapenda sana kaka.Yaani Mandhari yake usiseme.Lindi Inauzika broo.Ngoja Gesi ikishaaanza kuja hapo itaniambia broo
 
Hii ni Habari njema si kwa wana Lindi peke yake bali Watanzania wote kwa ujumla ni vizuri tuchangamkie fursa zinapojitokeza nawaomba vijana wasome sana masomo ya sayansi.
 
Tunachelewa mno kuchukua hatua na huenda ndio sababu iliyofanya Wahisani watulie kwanza. Kwakweli sielewi status ya mradi huu, tunajivuta mno wakati majirani zetu wa Msumbiji wanaendelea na ujenzi wa LNG terminal. Nasikitika sana kwa kukwama kwa mradi mkubwa kama huu wenye thamani takribani usd 32 bilio na vilivile kukwama kwa mradi mkubwa wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo wenye thamani zaidi ya usd 12 bilion. Nchi inahitaji kuwa na mega projects kama hizo kwa ajiri ya sasa na baadae. Yeyote anayejua juu ya mwelekeo wa mradi huu tafadhali tujuze.

Usiniulize sources ya habari hizi lakini amini usiamini mradi wa gas wa Mtwara na Lindi unaweza kuwa mradi hewa katika utawala huu. Mradi wa Lindi uliwachefuwa wawekezaji baada ya serikali kuchukua eneo husika kwa mabavu ili kupisha ujenzi huo! Inavyoonekana waliona utawala huu ni risk kwao kufanya biashara. Kadhalika wawekezaji wa gas Mtwara wamefungasha virago kwenda Mozambique pasipo kutoa sababu.

Kuna tatizo mahala fulani kwenye utawala mpya wa nchi yetu katika mahusiano na wawekezaji. Imekuwa kana kwamba hawana imani tena nasi. Ukiachia uwapo wa tatizo ni ukweli kwamba gas ya Mtwara na Lindi sio "deal" tena kwasababu ugunduzi wa gas unafanyika sehemu mbalimbali za Tz na nchi jirani na hata kwenye maeneo ya bahari ambayo hayana mmiliki.
 
Usiniulize sources ya habari hizi lakini amini usiamini mradi wa gas wa Mtwara na Lindi unaweza kuwa mradi hewa katika utawala huu. Mradi wa Lindi uliwachefuwa wawekezaji baada ya serikali kuchukua eneo husika kwa mabavu ili kupisha ujenzi huo! Inavyoonekana waliona utawala huu ni risk kwao kufanya biashara. Kadhalika wawekezaji wa gas Mtwara wamefungasha virago kwenda Mozambique pasipo kutoa sababu.

Kuna tatizo mahala fulani kwenye utawala mpya wa nchi yetu katika mahusiano na wawekezaji. Imekuwa kana kwamba hawana imani tena nasi. Ukiachia uwapo wa tatizo ni ukweli kwamba gas ya Mtwara na Lindi sio "deal" tena kwasababu ugunduzi wa gas unafanyika sehemu mbalimbali za Tz na nchi jirani na hata kwenye maeneo ya bahari ambayo hayana mmiliki.[/QUOTE
Huu ni uzushi mkubwa ndio maana unasema tusikuulize umepata wapi habari hizi, mradi upo pale pale kama ulivyokuwa umepangwa, sasa hv kinachoendelea ni hatua za mwisho za maandalizi kwa ajili ya mradi kuanza. Kama huamini kaylize watu wa makampuni ya nje kama Statoil, Ophir na BG/Shell ambao ndiyo wawekezaji watakaojenga mradi huu.
Usiniulize sources ya habari hizi lakini amini usiamini mradi wa gas wa Mtwara na Lindi unaweza kuwa mradi hewa katika utawala huu. Mradi wa Lindi uliwachefuwa wawekezaji baada ya serikali kuchukua eneo husika kwa mabavu ili kupisha ujenzi huo! Inavyoonekana waliona utawala huu ni risk kwao kufanya biashara. Kadhalika wawekezaji wa gas Mtwara wamefungasha virago kwenda Mozambique pasipo kutoa sababu.

Kuna tatizo mahala fulani kwenye utawala mpya wa nchi yetu katika mahusiano na wawekezaji. Imekuwa kana kwamba hawana imani tena nasi. Ukiachia uwapo wa tatizo ni ukweli kwamba gas ya Mtwara na Lindi sio "deal" tena kwasababu ugunduzi wa gas unafanyika sehemu mbalimbali za Tz na nchi jirani na hata kwenye maeneo ya bahari ambayo hayana mmiliki.
 
Ni jambo la furaha sana kwa mkoa wa Lindi moja ya mikoa ya zamani iliyobakia nyuma kimaendeleo huenda kuliko mikoa yote iliyoanzishwa zamani.

Uwepo wa mradi huu mkubwa ambao utakua ni kivutio kikubwa cha viwanda mkoani Lindi ambavyo vitakua chachu ya maendeleo mkoani Lindi.

Hoja kubwa kwa wananchi wa Lindi je, wamejiandaa kuupokea mradi huu kinguvu kazi na uwekezaji wa kijasiliamali?

Ujio wa mradi huu utaenda sambamba na mahitaji makubwa ya nyumba za kupanga, vyakula kama nyanya, kuku, viazi, matikiti nk

Maana kutofanya hivyo kutasababisha watu wa mikoa mingine kuja kuchukua hizo fursa nanyi muendelee kubakia watazamaji wa maendeleo ya wenzenu

Kwa upande wa serikali imeanza kuandaa muindombinu ya nishati itakayohakikisha uhai wa viwanda hivyo?

Je wameandaa miradi ya maji toka kwenye vyanzo vya maji vya kudumu na uhakika? Maana viwanda bila maji ni kazi bure, hali ya upatikanaji wa maji mjini Lindi bado siyo nzuri, kuna mitaa ina miaka miwili mabomba yao hayajawahi kutoa maji.

Naunga mkono jitihada za serikali kuuweka mradi huo mkoani Lindi, eneo la likong'o ili kupunguza tofauti za kimaendeleo kati ya mikoa yake au ukanda na ukanda

Hongera Rais Kikwete, muasisi wa mradi huu.

Hongera Rais Magufuli mtekelezaji mkuu wa mradi huu
Nionavyo hoja kubwa hapo ni serikali kuandaa umeme wa uhakika pamoja na maji kwajili ya viwanda. Hao wanalindi kama hawatojiandalia mazingira ya kibiashara tutaenda kufanya watu wengine, siyo lazima biashara waifanye wao. Kwani ni nani alisema gesi ni ya watu wa Lindi tu? Watanzania wengine tunayo haki ya kunufaika nayo pia
 
Usiniulize sources ya habari hizi lakini amini usiamini mradi wa gas wa Mtwara na Lindi unaweza kuwa mradi hewa katika utawala huu. Mradi wa Lindi uliwachefuwa wawekezaji baada ya serikali kuchukua eneo husika kwa mabavu ili kupisha ujenzi huo! Inavyoonekana waliona utawala huu ni risk kwao kufanya biashara. Kadhalika wawekezaji wa gas Mtwara wamefungasha virago kwenda Mozambique pasipo kutoa sababu.

Kuna tatizo mahala fulani kwenye utawala mpya wa nchi yetu katika mahusiano na wawekezaji. Imekuwa kana kwamba hawana imani tena nasi. Ukiachia uwapo wa tatizo ni ukweli kwamba gas ya Mtwara na Lindi sio "deal" tena kwasababu ugunduzi wa gas unafanyika sehemu mbalimbali za Tz na nchi jirani na hata kwenye maeneo ya bahari ambayo hayana mmiliki.

Kwa uelewa wangu, wawekezaji kabla ya kuwekeza wanaangalia mambo makuu na miongoni mwa mambo hayo ni sheria inayosimamia uwekezaji na pili ni pilitical stability. Wakati ule walipokuwa tayari kuwekeza nchi hii haikuwa na sheria yeyote inayosimamia uwekezaji katika gesi na ndio maana Serikali ilipokuwa inakazania kupitisha sheria ile wapinzani wakawa wanapinga kuwa kuna haraka gani bila kujua kwamba inahitajika ili kuwapa nafasi wawekezaji waweza kuangalia kama sheria inalinda maslahi yao au la. Wapinzani walikuja na madai mengi sana juu ya suala hili kitu ambacho wawekezaji katika sekta hii wakawa wanaogopa kutokuwa na political stability. Fahamu kuwa sizungumzi siasa hapa, nazungumza facts zilizokuwa zinazungumzwa kwenye journals za Kimataifa za masuala ya energy. Kutokana na hilo wawekezaji wakasita kwakuwa hawakuwa na uhakika wa usalama katika uwekezaji wao wakihofia political unstability na kutokuwa na sheria. Tukio la kusitisha kwao lika coincides na kuporomoka kwa bei ya crude oil below usd 30 pb ambako kulifanya mafuta kuwa nafuu zadi kuliko kawaida na kutishia soko la gas na vilevile kufunguka na kuwa tayari kwa Msimbiji kuwekeza kwenye LNG termila facility. Haya yote yamechangia sana, ikumbukwe pia wawekezaji walihitaji zaidi hii terminal ijengwa in-shore na sio off-shore.
Lakini amini nakwambia ukisomba trend katika biashara ya mafuta, gas and alternative source of energy, statistics za matumizi ya nishati hadi 2050 inaonesha kuwa matumizi ya nishati ya gas inakuwa kwa kasi kuliko nishati ya mafuta ingawa bado matumizi ya mifuta ni kiwango kikubwa kuliko gas. Matumizi ya gas yanaendelea na yataendelea kuongezeka kwa sababu zifuatazo 1) ugunduzi wa LNG techonoly 2) Mitambo ya kisasa na yenye nguvu ya kuzalisha gas, fahamu kuwa mitambo ya gas inaanzia hata kwenye kiwango cha chini kabisa sio lazima uwe na machine ya megawatts kubwa sana, kwa mfano sisi tunaweza kununua mitambo midogomidogo na kuiunganisha, 3) Kutokana Dunia kuwa sensitive na suala la emission ya greenhouse na carbon dioxide ambazo zina negative impact kwenye climate change inayopelekea kuongezeka kwa joto la Dunia na kuleta mabadiliko ya hali ya hewa duniani, gas ndio muokozi kwakuwa ina very low carbon contents ukilinganisha na oil and coal which are largely used as a source of energy to drive economy and power the world. Tanzania na Msumbiji zipo kwenye very strategic locations to wards to the world markets of China, India and Asia as compared to West African countries hivyo uhitajikaji wa gas yake ni muhimu kwakuwa ni karibu na soko. Lazima ujue kwamba uwekezaji kwenye energy industry si kama katika sector zingine za uchumi na wala haifuati traditional corporate financing hii ni kwakuwa hii sector inahitaji very big capital investmnet na has huwa inahusisha project financing sytem ambapo kuna kuwa na wawekeaji zaidi ya moja ili kuweza kupata fund na vilevile this is very high risk business kwahiyo ku share capital inasaidia kutawanya risks, vilevile utekelezaji wake ni very complex unaweza kuchukua miaka2-4 toka umeanza kuwekeza hadi gas inaanza kutoka chini ya ardhi, sometime complexity ya geological characteristics za sedimentary rocks zinabadilika hivyo kuhitajika kwa technologia nyingine ambayo haikuzaniwa baadae, ni vigumu kujua hali halisi ya chini kabla hujafika pamoja na advance technology inayotumika wakati wa survey. Hivyo basi elewa kuwa business hii ni very complex and risks, hata sisi Watanzania tunaojiita Wazalendo tunaolilia kufanya biashara hii na kusema Serikali inatunyima, sina uhakika kama kweli tuneweza kutoka na source of fund ya ku finance hizi project, ukiangalia projects zote kubwa duniani na za kushirikiana miongoni mwa makampuni makubwa ya mafuta duniani na wals si kampuni moja tu. Ndio maana kuna umuhimu sana kuwekeza kwenye National Oil Company kama zilivyofanya nchi zote zenye mafuta duniani, kwakuwa TPDC kwakuwa inawakilisha nchi inauwezo mkubwa wakupata mtaji kwakuweka rehani gas yenyewe au mafuta kwakuwa oil/gs reserves belong to the state. Kutokana na sababu hizo Wawekezaji wanahitaji sheria zilizowazi kabisa zinakazowavutia wao kuwekeza bila kuwa na wasiwasi sheria zitakazolind vitega uchumi vyao kwakuwa uzoefu unaonesha kuwa gas au mafuta yanapoanza kuzalisha nchi huwa zinabadili sheria na has za kugawana mapato kitu ambacho ni hatari sana.
 
Kwa uelewa wangu, wawekezaji kabla ya kuwekeza wanaangalia mambo makuu na miongoni mwa mambo hayo ni sheria inayosimamia uwekezaji na pili ni pilitical stability. Wakati ule walipokuwa tayari kuwekeza nchi hii haikuwa na sheria yeyote inayosimamia uwekezaji katika gesi na ndio maana Serikali ilipokuwa inakazania kupitisha sheria ile wapinzani wakawa wanapinga kuwa kuna haraka gani bila kujua kwamba inahitajika ili kuwapa nafasi wawekezaji waweza kuangalia kama sheria inalinda maslahi yao au la. Wapinzani walikuja na madai mengi sana juu ya suala hili kitu ambacho wawekezaji katika sekta hii wakawa wanaogopa kutokuwa na political stability. Fahamu kuwa sizungumzi siasa hapa, nazungumza facts zilizokuwa zinazungumzwa kwenye journals za Kimataifa za masuala ya energy. Kutokana na hilo wawekezaji wakasita kwakuwa hawakuwa na uhakika wa usalama katika uwekezaji wao wakihofia political unstability na kutokuwa na sheria. Tukio la kusitisha kwao lika coincides na kuporomoka kwa bei ya crude oil below usd 30 pb ambako kulifanya mafuta kuwa nafuu zadi kuliko kawaida na kutishia soko la gas na vilevile kufunguka na kuwa tayari kwa Msimbiji kuwekeza kwenye LNG termila facility. Haya yote yamechangia sana, ikumbukwe pia wawekezaji walihitaji zaidi hii terminal ijengwa in-shore na sio off-shore.
Lakini amini nakwambia ukisomba trend katika biashara ya mafuta, gas and alternative source of energy, statistics za matumizi ya nishati hadi 2050 inaonesha kuwa matumizi ya nishati ya gas inakuwa kwa kasi kuliko nishati ya mafuta ingawa bado matumizi ya mifuta ni kiwango kikubwa kuliko gas. Matumizi ya gas yanaendelea na yataendelea kuongezeka kwa sababu zifuatazo 1) ugunduzi wa LNG techonoly 2) Mitambo ya kisasa na yenye nguvu ya kuzalisha gas, fahamu kuwa mitambo ya gas inaanzia hata kwenye kiwango cha chini kabisa sio lazima uwe na machine ya megawatts kubwa sana, kwa mfano sisi tunaweza kununua mitambo midogomidogo na kuiunganisha, 3) Kutokana Dunia kuwa sensitive na suala la emission ya greenhouse na carbon dioxide ambazo zina negative impact kwenye climate change inayopelekea kuongezeka kwa joto la Dunia na kuleta mabadiliko ya hali ya hewa duniani, gas ndio muokozi kwakuwa ina very low carbon contents ukilinganisha na oil and coal which are largely used as a source of energy to drive economy and power the world. Tanzania na Msumbiji zipo kwenye very strategic locations to wards to the world markets of China, India and Asia as compared to West African countries hivyo uhitajikaji wa gas yake ni muhimu kwakuwa ni karibu na soko. Lazima ujue kwamba uwekezaji kwenye energy industry si kama katika sector zingine za uchumi na wala haifuati traditional corporate financing hii ni kwakuwa hii sector inahitaji very big capital investmnet na has huwa inahusisha project financing sytem ambapo kuna kuwa na wawekeaji zaidi ya moja ili kuweza kupata fund na vilevile this is very high risk business kwahiyo ku share capital inasaidia kutawanya risks, vilevile utekelezaji wake ni very complex unaweza kuchukua miaka2-4 toka umeanza kuwekeza hadi gas inaanza kutoka chini ya ardhi, sometime complexity ya geological characteristics za sedimentary rocks zinabadilika hivyo kuhitajika kwa technologia nyingine ambayo haikuzaniwa baadae, ni vigumu kujua hali halisi ya chini kabla hujafika pamoja na advance technology inayotumika wakati wa survey. Hivyo basi elewa kuwa business hii ni very complex and risks, hata sisi Watanzania tunaojiita Wazalendo tunaolilia kufanya biashara hii na kusema Serikali inatunyima, sina uhakika kama kweli tuneweza kutoka na source of fund ya ku finance hizi project, ukiangalia projects zote kubwa duniani na za kushirikiana miongoni mwa makampuni makubwa ya mafuta duniani na wals si kampuni moja tu. Ndio maana kuna umuhimu sana kuwekeza kwenye National Oil Company kama zilivyofanya nchi zote zenye mafuta duniani, kwakuwa TPDC kwakuwa inawakilisha nchi inauwezo mkubwa wakupata mtaji kwakuweka rehani gas yenyewe au mafuta kwakuwa oil/gs reserves belong to the state. Kutokana na sababu hizo Wawekezaji wanahitaji sheria zilizowazi kabisa zinakazowavutia wao kuwekeza bila kuwa na wasiwasi sheria zitakazolind vitega uchumi vyao kwakuwa uzoefu unaonesha kuwa gas au mafuta yanapoanza kuzalisha nchi huwa zinabadili sheria na has za kugawana mapato kitu ambacho ni hatari sana.

Kwa mara ya kwanza 2016 nasoma uchambuzi mzuri uliotoka kwa mtu mwenye shule na asiyechanganya siasa na ushabiki. Kwa kweli sikuchoka kusoma uchambuzi huu na sina hata chembe ya kuupinga. Kumbe humu tunao great thinkers!

That said, mimi ni mwenyeji wa mikoa ya kusini na ni mionogni mwa watu tunaolia kwa kusita kwa wawekezaji wa miradi yote ya kusini ikiwamo mradi wa uranium. Tulidhani kwamba kusini tungeendelea kupitia miradi hii, tumepigwa kofi jingine upande mwingine.
 
Back
Top Bottom