SolarPower
JF-Expert Member
- Jan 17, 2011
- 223
- 27
Katika kikao cha Bunge kinachoendelea Dodoma kuna Mbunge mmoja alizungumzia tetesi kuwa Serikali imeamua kuanzia mwaka huu (2011) mtihani wa Hisabati wa Darasa la Saba utakuwa wa Multiple choice lakini Waziri wa Elimu na Naibu wake walipinga. Lakini ukweli ni kuwa hivyo ndiyo ilivyoamuliwa na ndivyo itakavyokuwa kwani watoto waliofanya mtihani wa Moko mwezi huu wa saba katika somo la Hisabati majibu yake yalikuwa ni Multiple Choice. Na matokeo ya uamuzi huu mbovu yameanza kujitokeza kwani katika shule moja kuna wanafunzi ni dhaifu sana katika Hisabati lakini wamepata maksi ambazo zimewashangaza hata walimu wao.