thamani yetu iwapi?,wanyonge wa duniani.
wanaotujali wangapi?,mbona hawaonekani?
haki zetu ni zipi?,mbona hazijulikani?
makosa yetu ni yepi?, hata tuwe adhabuni?
masuali yamenijaa , kichwani najiuliza
kitembea hujikwaa , nasubiri mliwaza.
nishaikata tamaaa , nasubiri miujiza
wanasiasa hadaa , wamo watuangamiza.
ni wengi watesekao , ni malaki kwa lukuki.
wamekimbia makwao , kuitafuta riziki.
mataifa watokayo , yamekana zao haki.
wakubwa ndio walao , wanyonge tunahiliki.
wengi barabarani ,usiku hujilalia
vyakula vya majalalani, ndio wao hujilia.
ya kinamama sisemi , heshima nawatunzia
watawala ni nani? , wasiotufikiriaa.
wanatunyima elimu , wanasema hatusomi
matibabu yalazimu , pesa iwe mfukoni.
maji nayo ni adimu , umeme hatuuoni.
tumemkosa hakimu ,twamuachia manani
kuna wanaojinyonga ,kwa kuchoshwa na dhuluma.
kuna tunaojitenga , na siasa za hujuma
msitufanye wajinga ,kutunyanyasa daima.
mwatudharau mwaringa ,mwatuchimbia nakama.
duniani tunaishi ,mithili ya nusu wafu.
matatizo hayaishi , si sasa wala halafu.
wakubwa haziwatoshi , wazitafuna sarafu.
wajifanya ni wacheshi , wakitubana mapafu.
watawala fikirini , nasi pia binadamu.
kile mnachotamani , nasi pia tuna hamu.
mwatibiwa ugenini , sie twafa majumbani.
haki yetu ni nini? , mbona mnatudhulumu?
roho zetu mwaziona , ni kama roho za mende.
miili yatuzizima , hatujui wapi twende.
twamuomba karima , atujalie tushinde.
atuepushe daima , na madhara atulinde.
hatujali utajiri , twaomba uadilifu.
muwajali mafakiri ,msiwe wabadhirifu.
hapo sisi tutakiri , serikali ni tukufu.
rushwa nayo ni hatari ,wekeni uaminifu.
maisha yenu ni mema , hayafanani na yetu.
daima mko salama , sie "hofu" jina letu.
kutwa kucha twalalama,hamjali vilio vyetu.
na tukiamua kusema , mwaziba midomo yetu.
"Taifa ni maskini" ,mwashindwa kuthibitisha.
nyuso zetu ziko duni , zenu nyie zang'arisha.
twawaona majiani , magari mwabadilisha.
wale tulo maskini , kijio chatuhangaisha.
kukumbushana wajibu , nami leo nakumbusha.
si lazima mnijibu , mkifahamu yatosha.
maisha ni majaribu , iko siku yatakwisha.
kwa mola kuna adhabu , kaburini kunatisha.
shairi nahitimisha , kwa mnasaba wa dua.
yarabbi tasahilisha , na kheri kutuletea.
dhuluma ataondosha ,atujaaliye sawiya .
zisitupate presha , atulinde na ghasiya.
tunamuomba muumba , atujaalie subira.
atulinde na kasumba ,za wanasiasa na sera.
awafedhehi watimba ,wanaodanganya kwa kura.
atubariki wa shamba , tusiamue kugura.
amiin.
ni mdogo wenu underage
wanaotujali wangapi?,mbona hawaonekani?
haki zetu ni zipi?,mbona hazijulikani?
makosa yetu ni yepi?, hata tuwe adhabuni?
masuali yamenijaa , kichwani najiuliza
kitembea hujikwaa , nasubiri mliwaza.
nishaikata tamaaa , nasubiri miujiza
wanasiasa hadaa , wamo watuangamiza.
ni wengi watesekao , ni malaki kwa lukuki.
wamekimbia makwao , kuitafuta riziki.
mataifa watokayo , yamekana zao haki.
wakubwa ndio walao , wanyonge tunahiliki.
wengi barabarani ,usiku hujilalia
vyakula vya majalalani, ndio wao hujilia.
ya kinamama sisemi , heshima nawatunzia
watawala ni nani? , wasiotufikiriaa.
wanatunyima elimu , wanasema hatusomi
matibabu yalazimu , pesa iwe mfukoni.
maji nayo ni adimu , umeme hatuuoni.
tumemkosa hakimu ,twamuachia manani
kuna wanaojinyonga ,kwa kuchoshwa na dhuluma.
kuna tunaojitenga , na siasa za hujuma
msitufanye wajinga ,kutunyanyasa daima.
mwatudharau mwaringa ,mwatuchimbia nakama.
duniani tunaishi ,mithili ya nusu wafu.
matatizo hayaishi , si sasa wala halafu.
wakubwa haziwatoshi , wazitafuna sarafu.
wajifanya ni wacheshi , wakitubana mapafu.
watawala fikirini , nasi pia binadamu.
kile mnachotamani , nasi pia tuna hamu.
mwatibiwa ugenini , sie twafa majumbani.
haki yetu ni nini? , mbona mnatudhulumu?
roho zetu mwaziona , ni kama roho za mende.
miili yatuzizima , hatujui wapi twende.
twamuomba karima , atujalie tushinde.
atuepushe daima , na madhara atulinde.
hatujali utajiri , twaomba uadilifu.
muwajali mafakiri ,msiwe wabadhirifu.
hapo sisi tutakiri , serikali ni tukufu.
rushwa nayo ni hatari ,wekeni uaminifu.
maisha yenu ni mema , hayafanani na yetu.
daima mko salama , sie "hofu" jina letu.
kutwa kucha twalalama,hamjali vilio vyetu.
na tukiamua kusema , mwaziba midomo yetu.
"Taifa ni maskini" ,mwashindwa kuthibitisha.
nyuso zetu ziko duni , zenu nyie zang'arisha.
twawaona majiani , magari mwabadilisha.
wale tulo maskini , kijio chatuhangaisha.
kukumbushana wajibu , nami leo nakumbusha.
si lazima mnijibu , mkifahamu yatosha.
maisha ni majaribu , iko siku yatakwisha.
kwa mola kuna adhabu , kaburini kunatisha.
shairi nahitimisha , kwa mnasaba wa dua.
yarabbi tasahilisha , na kheri kutuletea.
dhuluma ataondosha ,atujaaliye sawiya .
zisitupate presha , atulinde na ghasiya.
tunamuomba muumba , atujaalie subira.
atulinde na kasumba ,za wanasiasa na sera.
awafedhehi watimba ,wanaodanganya kwa kura.
atubariki wa shamba , tusiamue kugura.
amiin.
ni mdogo wenu underage