WAZEE WA KIMASAI WAMJADILI LOWASSA risasi mchanganyiko
Aidha, wazee hao wapatao 90 wamejadili pia kuhusu mkanganyiko uliopo ambao baadhi ya watu humchukulia waziri mkuu huyo aliyejiuzulu kuwa ni kutoka kabila la Kimasai wakati wao wanamfahamu kuwa ni Mmeru.Akizungumza na mwandishi wetu kwa simu kutoka kijiji cha Luburuko, Arumeru Mashariki mkoani Arusha mwanzoni mwa wiki hii, Katibu wa Mila za Kimasai, Amos Mollel alisema kuwa kikao hicho kilikaa Machi 8, mwaka huu.Mollel alisema kuwa, walilazimika kuitisha kikao cha wazee kutoka maeneo mbalimbali mkoani humo kufuatia watu wengi kusema kuwa tuhuma zilizomfanya Lowassa ajiuzulu uwaziri mkuu ni kubwa na ni kitendo cha aibu ambacho Mmasai hawezi kufanya.Aliendelea kusema kuwa kikao chao kilifikia uamuzi wa kuwaomba wananchi waelewe kuwa Lowassa si Mmasai, kwani kufanya hivyo ni kuwachokoza watu wa kabila hilo.Unajua mwandishi, madai yanayoelekezwa kwa Lowassa kuhusu ufisadi uliofanywa kupitia kampuni hewa ya kuzalisha umeme ya Richmond ni kitendo cha aibu kubwa kwa jamii.Hivyo, tulikaa ili kujisafisha kwakuwa wengi wanajua kuwa ni Mmasai mwenzetu kumbe ni Mmeru, alisema Mollel.Lowassa alijiuzulu hivi karibuni kwa kuhusishwa na sakata la Kampuni hewa ya Richmond ambayo hadi sasa inalipwa shilingi milioni 152 kwa mwezi.Mawaziri wengine waliojiuzulu kufuatia kashfa hiyo ni pamoja na waliowahi kuwa mawaziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi na Ibrahim Msabaha.
Aidha, wazee hao wapatao 90 wamejadili pia kuhusu mkanganyiko uliopo ambao baadhi ya watu humchukulia waziri mkuu huyo aliyejiuzulu kuwa ni kutoka kabila la Kimasai wakati wao wanamfahamu kuwa ni Mmeru.Akizungumza na mwandishi wetu kwa simu kutoka kijiji cha Luburuko, Arumeru Mashariki mkoani Arusha mwanzoni mwa wiki hii, Katibu wa Mila za Kimasai, Amos Mollel alisema kuwa kikao hicho kilikaa Machi 8, mwaka huu.Mollel alisema kuwa, walilazimika kuitisha kikao cha wazee kutoka maeneo mbalimbali mkoani humo kufuatia watu wengi kusema kuwa tuhuma zilizomfanya Lowassa ajiuzulu uwaziri mkuu ni kubwa na ni kitendo cha aibu ambacho Mmasai hawezi kufanya.Aliendelea kusema kuwa kikao chao kilifikia uamuzi wa kuwaomba wananchi waelewe kuwa Lowassa si Mmasai, kwani kufanya hivyo ni kuwachokoza watu wa kabila hilo.Unajua mwandishi, madai yanayoelekezwa kwa Lowassa kuhusu ufisadi uliofanywa kupitia kampuni hewa ya kuzalisha umeme ya Richmond ni kitendo cha aibu kubwa kwa jamii.Hivyo, tulikaa ili kujisafisha kwakuwa wengi wanajua kuwa ni Mmasai mwenzetu kumbe ni Mmeru, alisema Mollel.Lowassa alijiuzulu hivi karibuni kwa kuhusishwa na sakata la Kampuni hewa ya Richmond ambayo hadi sasa inalipwa shilingi milioni 152 kwa mwezi.Mawaziri wengine waliojiuzulu kufuatia kashfa hiyo ni pamoja na waliowahi kuwa mawaziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi na Ibrahim Msabaha.