Lijimama la kinaijeria

Waterlemon

Senior Member
Sep 2, 2016
137
178
Hili tukio lilitokea kipindi cha nyuma... nimeona nilieke hapa jukwaani myaone wenyewe wana JM.

Tulikuwa tupo ndani ya basi kwenye mizunguko ya kawaida... kila mtu na shughuli zake na mawazo yake kichwani. Mara tukaskia mzozo kwa sauti za juu na za jazba.

Lijimama la kinaijeria ambalo lilikuwa limwili limemjaa haswa alikuwa akumtuhumu abiria wa pembeni yake ambae alikuwa kijana mdogo tu kwa kufoka kama kamchomolea pochi yake ya pesa kutoka kwenye mkoba wake.... kijana wa pembeni alionyesha kupinga hiyo tuhuma... lakini lawama ziliendelea kumwelemea na kipigo kuanza kumuangukia. Mwanzo kuanzia kutoka lijimama la kinaijeria kwa vibao na makofi, na abiria wengine wakaanza kumsaidia...

Kijana akakung'utwa vya kutosha.... kuanzia ndani ya basi ambali lilikuwa limejaa ... mpaka basi likasimama na kipigo kuendelea nje.

Katika pirika pirika za kuendelea kumpiga kijana wa watu... lijimama la kinaijeria katika kuruka ruka kusambaza kipigo, kati kati ya matiti pochi lake likachomoka na kuanguka hadharani... watu wote wanashuhudia ...


"Ooooh, kumbe pochi yangu ilikuwa hapa?" ... akaiokota na huyooo taratiiiibu, akaanza kuondoka.

Wapigaji waliokuwa wakisaidia wote macho yamewatoka wakimwangalia kijana aliepigwa wasijue la kufanya.

Je muungwana... anapopigwa mwizi . Ni sahihi kuingilia kutoa adhabu?
 
Angetakiwa kulipiga vibao au hata mawe kama vipi na hao abiria wengine ningewambiwa wafanye kunisaidia kama walivyosaidia..si sahihi kufanya walichofanya nimeshashuhudia watu badala ya kumpiga mtu kwa kisingizio hicho tuliamua wote kwenda kituo cha police na ukaguzi ukaanza baada ya maelezo yetu
 
Angetakiwa kulipiga vibao au hata mawe kama vipi na hao abiria wengine ningewambiwa wafanye kunisaidia kama walivyosaidia..si sahihi kufanya walichofanya nimeshashuhudia watu badala ya kumpiga mtu kwa kisingizio hicho tuliamua wote kwenda kituo cha police na ukaguzi ukaanza baada ya maelezo yetu

Haswaaaa. Hilo ndio la kufanya. Lakini frustration za maisha watu huzimalizia hapo hapo.
 
tabia ya kupiga piga hovyo watu haikubaliki.

ni unyama kumbondabonda mtu, hata kama kweli ni mwizi.

mwizi akamatwe atiwe polisi, kisha mahakamani.

sio kutoboa toboa watu macho na vyuma.

mbaya sana hii.
 
yani Mimi najua umelitafuna jimama la kinaijeria nikupongeze mkuu kwa mafanikio makubwa kama hayo kumbe unatuletea vistori vyako vya kahawa bwege kabisa wewe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom