life style

rich gang

JF-Expert Member
Jun 9, 2016
1,552
908
nilizaliwa kwa mama peke yangu na sikujua kuwa ningekutana na wenzangu,sasa akili ilichachamaa na hio ni baada ya kukutana na marafiki kadhaa ambao wengi tuliishi kwa mtaa huku tukibadili mazingira na na jinsi ya kukaa ,utoto ulinitanda nikifanya kosa nakula viboko mixture na mkanda,nikichelewa home nilikuwa naweza pigwa hata na kiatu,sebure disco jirushe kwenye makochi ila ukikutwa utajuta kwa hayo makofi,tena beki 3 alivyo mnoko ukifanya soo yeye ndio anapewa jukumu la kusaka chocho zote..nyumbani zilishakuja nying kesi kwamba nimemtoa mtu ngeo,nilikuwa situlii akija mgeni labda uniwekee muvi ya bluce lee au jack chan majirani waliniona mtoto hatari usiku napiga kelele mithili ya popo,mwendo wa vurugu nalusha makopo juu ya bati,nikitulia ujue ni siku ya ndondo na wali,ikipita sana mda soda najifanya naumwa unaweza hisi nimelogwa,nakunja sura sitaki kupiga soga,nilikuwa mbishi sana linapokuja swala la kuoga mda mwingine nilikuwa nazuga hamna sabuni kumbe nimeficha ili nicheki cartoon...kila siku nilikuwa nambonji nikiwa hoi........unakumbuka nini utotoni mwako
 
Back
Top Bottom