Mshika Tester
Member
- May 3, 2020
- 38
- 35
Sijui ndiyo nimeanza kukata tamaa kwa kweli sijielewi! Zamani niliamini uwezekano wa kupata pesa kwa njia halali ni mkubwa sana, niliamini uchawi si chochote lakini sasa naanza kuingiwa na kaimani, watu tunataabika miaka mingi kutafuta mali kwa njia halali tunawahi kuamka daily, tunapiga kazi bila kuchagua, tunajibana kula na kuvaa, hatuna mademu wakali, hatuni nyumba, magari, tumechelewa kuzaa na kuoa.
Lakini tunaowaona wazembe kila siku wanapiga hatua tu wanaenjoy maisha vyote tunavyojizuia kufanya ili tufanikiwe wao wanafanya tena kwa speed kama yote hata hivyo mafanikio yanaendelea kuwafuata (sina maana sipendi wengine wafanikiwe ila ni mfano wa kulinganisha na sisi tunao hastle).
Naanza kuamini upepo wa pesa, nuksi, mikosi na chuma ulete nk, tunapata pesa haikai na ukiangalia hatuna majukumu mengi kama kusomesha, kutunza wazazi, kutunza familia cha ajabu zaidi hatuna matumizi ya anasa, lakini bado hela haikai kila siku umaskini unaongezeka makali.
Niliamini nitakuja kuwa tajiri siku moja lakini kadiri siku zinavyosonga mbele mambo yanachange, naamini pia vijana wengi wa kati ya 18-27 wanaamini watakuja kuwa matajiri pia.
Angalizo! Usiamini kama mimi inawezekana mimi nimenza kukata tamaa au kuna maarifa fulani sahihi nimekosa katika harakati zangu, hebu na wewe jipe muda kufanya utafiti kabla hujaanza kuwaza kama mimi.
Yesu mwokozi naomba nisaidie nisiingie kwenye ushirikina angalau nipe ishara za kwenda peponi niridhike kuwa sitakuwa tajiri lakini nitaenda peponi kuliko hivi sasa. Sijui nikifa nitaenda kuteseka katika moto wa milele au nitaenda peponi. Naogopa nisije nikawa nimeteseka duniani na mbinguni nikateseka pia nikiwa moja ya viumbe vilivyoumbwa kwa ajili ya kuteseka.
Lakini tunaowaona wazembe kila siku wanapiga hatua tu wanaenjoy maisha vyote tunavyojizuia kufanya ili tufanikiwe wao wanafanya tena kwa speed kama yote hata hivyo mafanikio yanaendelea kuwafuata (sina maana sipendi wengine wafanikiwe ila ni mfano wa kulinganisha na sisi tunao hastle).
Naanza kuamini upepo wa pesa, nuksi, mikosi na chuma ulete nk, tunapata pesa haikai na ukiangalia hatuna majukumu mengi kama kusomesha, kutunza wazazi, kutunza familia cha ajabu zaidi hatuna matumizi ya anasa, lakini bado hela haikai kila siku umaskini unaongezeka makali.
Niliamini nitakuja kuwa tajiri siku moja lakini kadiri siku zinavyosonga mbele mambo yanachange, naamini pia vijana wengi wa kati ya 18-27 wanaamini watakuja kuwa matajiri pia.
Angalizo! Usiamini kama mimi inawezekana mimi nimenza kukata tamaa au kuna maarifa fulani sahihi nimekosa katika harakati zangu, hebu na wewe jipe muda kufanya utafiti kabla hujaanza kuwaza kama mimi.
Yesu mwokozi naomba nisaidie nisiingie kwenye ushirikina angalau nipe ishara za kwenda peponi niridhike kuwa sitakuwa tajiri lakini nitaenda peponi kuliko hivi sasa. Sijui nikifa nitaenda kuteseka katika moto wa milele au nitaenda peponi. Naogopa nisije nikawa nimeteseka duniani na mbinguni nikateseka pia nikiwa moja ya viumbe vilivyoumbwa kwa ajili ya kuteseka.