T 1990 ELY
JF-Expert Member
- Sep 7, 2014
- 12,162
- 28,297
Umenikumbusha hiyo aibu/kisa chako namba mojaDah,wakati uzi huu unaletwa sikuwa online kwakwel
Nina visa vyangu viwili na kingine ni cha mwanafunzi mwenzangu
Kisa no 1
Miaka kadhaa ya nyuma nikiwa form one huko vijijini basi kulikuwepo na utaratbu kila terminal na annual walikuwa wanasoma top ten na wale kumi wa kutoka mwisho basi siku hyo ilikuwa ijumaa tukifunga kwenda likizo ya mwezi disemba siku hyo nilkuwepo period na kipindi hiko tulikuwa tunavaa matambala hata pedi nilkuwa sizijui basi mida ya sa nane tukaa skuli balaza mawaidha yakaendelea mara nasikia damu zinatiririka mithili ya maji yaani nasikia sehemu nilyokaa kama imejaa hivi najiuliza niombe ruhusa kabla sijajifikiria vizuri nasikia wanaanza kusoma majina ya top ten mara jina langu linaitwa ,wa kwanza darasani ni fulani(sasa inabidi ninyanyuke niende kupewa mkono na meza kuu na kupewa zawadi)aseee!nildata pale chini kwa sekunde kadhaa,theni nkasimama ,nilihisi damu zinachuruzika hadi miguuni(but haikuwa hivo ni hisia tu) bahati nzuri sketi ilikuwa nyeusi afu ndefu basi nkapata akili nkavua sweta nkajifunga kiunoni ikabid niende mbele kuchukua zawadi(unapoenda mbele wanafunzi unawapa mgongo )japo sijui sikugundulika lakini niliona aibu sana yaani kama wiki nzima nilkuwa nikifikiria hicho kitu
Kisa no 2
Hii ni miaka ya hivi karibuni,kawaida mimi pombe nakunywa,lakini ni zile za kureflesh na ni mara chache mno na mara nyingi huwa nakunywa wine na konyagi ikitokea basi bwana siku hyo nimejisikia kunywa nimeenda glossary nkaulizia wine hakuna,konyagi hakuna nkaambiwa imebaki k,vant tu sijawahi kunywa kivant ila uwa nasikia wanaisifia basi nkasema wacha nichukue kivant ndogo maana sina namna,nkabeba zangu nkaenda home nkanywa but naona radha yake siyo nzuri nkajikaza nkanywa nilivomaliza nkaenda kulala,nimelala usingizi mzuri mara kama naota hivi nasikia mme wangu ananiamsha anasema umekuwaje????aseee kumbe natapika mashuka yote na blanket yashakula matapishi fasta usingizini(ikumbukwe sijawahi tapika tangu nakunywa pombe)haraka niliamka nkaenda chooni tapika wee mpaka nyongo aseeee siku hiyo niliona aibu yaani kutapika kisa pombee??na mme wangu yeye hata hanywiii,naichukia k,vant
Kisa 3
Tukiwa form four miaka hyo wavulana kwa wasichana ilikuwa mida ya sa saba jua kali kipindi cha hesabu darasani kilikuwa kinaendelea,ikumbukwe hii mida ni mida ambayo wanafunzi wengi wanakuwa wamelala basi kuna binti mmoja alikuwa amekaa sehemu ambayo ni katikati ya darasa kama kawaida akauchapa usingizi wake kwenye dawati,mda kidogo akaanza kuota na kukojoa akakojoa mkojo unatiririka kwenye sakafu,hyo nayo ilikuwa aibu kwake hata sisi wasichana tuliona aibu but ni mambo ya kawaida
Nilivokoswa na aibu ambayo nilishaiona mbele yako
2016 nilkuwa natoka gongo la mboto naenda job,kumbe nilvotoka nkabeba mkoba mwingine wa jana ambao ulikuwa na hela nkauacha,tumefika sokota nakumbuka nimebeba mkoba hauna nauli dah nkaona hapa ni hatari,nkimuona konda ni wale micharuko akili akanijia kwamba itabid nimwambie hela yake namtumia m pesa kwani nashukia njiani,nkaanza kuwaza ntakavodhalilishwa nkasema eeh Mungu wangu sijafanya makusudi,huwezi amini konda alinipita wala hakuniuliza nauli nami nkasema hii ndo inaitwa miujiza
But all in all aibu zinakuja vyovote kikubwa ni kuzipotezea
Kuna madame moja alikuwa anatufundisha darasani ile anageuka kuandika ubaoni niliona/tuliona damu zimetiririka/zinatiririka mguuni
Kumbe madame aliingia kwenye siku zake bila yeye kujua
Wanafunzi tuliona tukio hilo laivu kabisa madame aliona aibu mno mpaka wiki mbili zilipita hakuja shuleni