Wateule
JF-Expert Member
- Sep 17, 2010
- 390
- 368
Katiba imezuia marais wastaafu wasishtakiwe, lakini sio wasijadiliwe. Tena majadiliano muhimu, ambayo yamejikita kuangalia uwezekano wa kuondoa kinga, ili wafikishwe mahakamani kutoa maelezo zaidi. Binafsi, sioni lazima wafungwe (kwani hili lina mazingira magumu sana), lakini wakikutwa na hatia watuombe msamaha watanzania kwa ubinafsi wao na tusonge mbele kama taifa.
Lakini, kinga ya rais kutoshtakiwa iondolewe kwenye hiyo katiba mpya, ili marais wajao (akiwemo na Magufuli wa sasa) wawe na hofu na heshima juu ya mali za Watanzania. Akisimamia hili, Magufuli atakuwa amefanya la maana sana kwa nchi yake, kwani atakuwa ametusafishia njia kwa siku za usoni na pia hatokuwa na mtihani mgumu wa kulazimika kuwashtaki na pengine kuwafunga marais waliomtangulia. Hata utawala wa Waafrika ulivyofanikiwa kushika dola kule South Afrika, hawakuhubiri kuwakamata wazungu waliowatesa nchini mwao na kuwafunga au kuwaua, bali waliunda tume ya "Maelewano na Mapatano" ili kusameheyana kwa yaliyopita na kusonga mbele.
Na sisi Watanzania tuwe wepesi wa kukubali kusamehe na kusonga mbele baada ya majadiliano kufanyika. Utaratibu wa sasa wa kuwatisha watu wasiwajadili marais wastaafu ambao ni dhahiri wamehusika kwa njia moja au nyingine katika ubadhirifu huu mkubwa wa mali za Watanzania, sio mzuri na hauna mwisho mwema. Kuendelea kutisha watu hakumpi sifa Magufuli ya u "hero" kama anavyotaka, na badala yake kunamfanya aonekane mtu aliyedandia basi bila kujua linapoelekea.
Lakini, kinga ya rais kutoshtakiwa iondolewe kwenye hiyo katiba mpya, ili marais wajao (akiwemo na Magufuli wa sasa) wawe na hofu na heshima juu ya mali za Watanzania. Akisimamia hili, Magufuli atakuwa amefanya la maana sana kwa nchi yake, kwani atakuwa ametusafishia njia kwa siku za usoni na pia hatokuwa na mtihani mgumu wa kulazimika kuwashtaki na pengine kuwafunga marais waliomtangulia. Hata utawala wa Waafrika ulivyofanikiwa kushika dola kule South Afrika, hawakuhubiri kuwakamata wazungu waliowatesa nchini mwao na kuwafunga au kuwaua, bali waliunda tume ya "Maelewano na Mapatano" ili kusameheyana kwa yaliyopita na kusonga mbele.
Na sisi Watanzania tuwe wepesi wa kukubali kusamehe na kusonga mbele baada ya majadiliano kufanyika. Utaratibu wa sasa wa kuwatisha watu wasiwajadili marais wastaafu ambao ni dhahiri wamehusika kwa njia moja au nyingine katika ubadhirifu huu mkubwa wa mali za Watanzania, sio mzuri na hauna mwisho mwema. Kuendelea kutisha watu hakumpi sifa Magufuli ya u "hero" kama anavyotaka, na badala yake kunamfanya aonekane mtu aliyedandia basi bila kujua linapoelekea.