Licha ya tofauti zao, kwa uwingi wetu Watanzania, watu hawa tuwalazimishe wafanye kwa niaba yetu

paul sylvester

JF-Expert Member
Mar 18, 2020
3,504
3,499
Hii hoja haijawalenga Sana wale wenzangu na mimi ambao Wao wamechanjwa chale za vyama vyao

Sasa karibu katika mjadara!

Najua kuna wale ambao liwe jua ama mvua Wao ni CCM Tu, lakini kuna wengine ambao hata ukimwamsha usiku wa manane Kutokea usingizini umuulize, wewe ni Chama gani, atakujibu huku akipiga miayo ya usingizini kuwa yeye ni CHADEMA tu

Siyo vibaya kuwa mwanachama wa kudumu, lakini nikutahadharishe kuwa, huwenda ndio sababu za Watanzania wengi kuwa masikini wa kutupwa ili Hali watu wachache wakineemeka na utajiri wa Taifa letu

Mawazo yangu ni ingelikuwa kheri iwe hivyo Kwa viongozi tu wa vyama kuwa wanachama wa kudumu Ila raia tukawa tuko katikati,

Nahisi kwamba, kuendekeza uvyama na kung'ang'ania mavyama badala ya kuchagua viongozi Bora tu Kutokea Chama chochote kile, ndio sababu pia ya umasikini tulionao wengi,

Yaani uchaguzi kama huu, tungelifanya upembuzi wa kuchagua mayai yote tokea Chama chochote na sio mayai viza eti tu Kwa sababu linatokea Chama chako,

Wagombea nafasi ya urais, ukiiruhusu nafsi yako itawale ukweli wa moyo wako, utakubaliana na mimi kwamba, wote ni vifaaa, mayai haswaa, majembe haswaa, wapambanaji na wasiokubali kushindwa kirahisi, wote ni majasiri na wapambanaji, wote wanakiu ya kutupeleka mahali, tofauti zao ni ndogo saana,

Ni ndogo Kwa sababu, watu hawawezi kufanana Kwa kila kitu,

Kuzidiana huko, ndio kunatufanya kila mmoja aseme, atampa furani Kura yake, nikiwemo na Mimi, na niseme wazi kuwa, Kura yangu nitampa Magufuli, ingawa msimamo wangu haupo katika Chama, napenda mtu Bora, Jasiri asiyeogopa, na hata Mungu Baada ya Musa kufa, alimwambia Joshua kuwa, awaongoze Israel kwenda Kanani, asigeuke nyuma Wala asiogope, Kwa kuwa Mtu Jasiri ndio sifa ya Ushindi,

Sasa basi, Kwa kuwa tuna watu mashuhuri hasa hao wawili pekee, Kwa maana ya Mh Lisu na Mh Magufuli, na ijapokuwa mmoja hasa Mh Lisu ndiye atakaye shindwa" na kushindwa kwake si Kwa sababu ni hatufai kutuongoza, hapana, anashindwa tu Kwa sababu ni lazima katika kushindana awepo mshindi na mshindwa

Sasa basi, hawa majemedari wa nyakati za leo, Sisi Watanzania, tuwalazimishe wafanye kazi pamoja,

Kama Magufuli akiwa ndiye Rais, Waziri Mkuu awe ni Mh Lisu, hiyo isiwe ombi kwao,

Kama ni kuandamana kama nchi ili kuwashinikiza wafanye kazi pamoja, basi tuwe na maandamano yasiyokoma,

Tanzania inamhitaji Magufuli na inamhitaji Lissu pia, na Mungu amewaleta Kwa wakati mmoja na wakati utufaao Sisi kama nchi

Toa maoni yako, Matusi ni kukosa hekima
 
Itakuwa dhambi kubwa Kama nchi, viongozi hawa tukashindwa kuwatumia kisa tu, wanatofautiana Vyama
 
Hivi tunamhitaji jiwe kwa lipi zuri? Amekuwa dikteta, mbaguzi na muuaji, mbona viwango vyetu watanzania ni vya chini kabisa jalalani? Inakuwaje mtu kuona kwamba jiwe ni kiongozi mzuri hata baada ya kuondoa uhuru, haki na demokrasia nchini? Lazima tatizo ni fikra finyu za watanzania. Itachukua muda sana kwa Tanzania kuendelea.
 
Hapa una hoja za msingi sina tatizo kabisa na mtazamo wako. Kimsingi kama uchaguzi ungekuwa unafanyika kwa uhalali sio lazima uwe mkubwa, lakini wangalau uhalali wa kuridhisha, tungeweza kupata viongozi bora bila kujali vyama vyao. Lakini kwa bahati mbaya sana mfumo mzima wa uchaguzi unatumikia chama kimoja, hii inapelekea kupata hata viongozi wasiostahili.

Unapoona nchi inafikia uchaguzi wote unanajisiwa na kutoa viongozi wa chama kimoja bila ridhaa ya umma, hapo tatizo ni kubwa kuliko unavyodhani.

Na kwa sasa, bila kuuma maneno, Magufuli ni mmoja kati ya watu wanaotumia udhaifu wa mifumo kuharibu mifumo ya utawala wa nchi. Na hii presidence anayotengeneza sasa italeta tatizo ndani ya nchi hii kwa miaka mingi, labda itokee machafuko ndio tutakaa meza ya kuweka mambo sawa. Bila machafuko sioni ushauri wako mzuri ukifanyiwa kazi.
 
Sasa magu wa nini ikiwa serikali yake ya miaka mitano haijaleta unafuu kwangu mimi na jirani zangu.

Bora atupishe kidogo tuone wengine watafanya nini, bora rungwe kuliko chakito
 
Hivi tunamhitaji jiwe kwa lipi zuri? Amekuwa dikteta, mbaguzi na muuaji, mbona viwango vyetu watanzania ni vya chini kabisa jalalani? Inakuwaje mtu kuona kwamba jiwe ni kiongozi mzuri hata baada ya kuondoa uhuru, haki na demokrasia nchini? Lazima tatizo ni fikra finyu za watanzania. Itachukua muda sana kwa Tanzania kuendelea.
Yule Mzee anamacho ya mwewe mkuu, anaona mbali Hadi miaka mitatu Mbele Tanzania itakuweje huko

Binadamu huwa tupo duniani Kwa ajiri ya wengine, na mtu akiishi tu Kwa ajiri yake peke yake, kawaida huyo mtu ni lazima tusimfiche kuwa, yeye ni hasara tupu kuwepo duniani

Unayemsema mkuu, Miradi mingi mikubwa aliyoianzisha, baada ya miaka mitano utaiona faida yake! Ndipo utauona umhimu wa huyo mtu

Je wewe utaacha legals ipi Kwa nchi yako, maana hili linamhusu kila mtu, najua unayo mengi ambayo umeyafanya, lakini pia usikatae kabisa eti huyu Magufuli hajafanya kitu, halafu sasa nikwambie ukweli kwamba, kitu alichofanya Magufuli pengine linaweza kuwa ndio kitu mhimu na kikubwa zaidi ya miaka 60 iliyopita,

Tatizo lililopo, hasa Africa hatuna neno linaloitwa Subra, na NDIYO Maana mtu akifungua mradi wake, Yuko radhi kuuufunga na kuacha abisa kufanya mradi wowote ule, kisa Jana alipata hasara, Inua macho mkuu, utazame Mbele
 
Unazungumzia siasa hata katiba hujui ?

Unazungumzia ubaguzi kamshauri Magufuli aache kulazimisha watu wachague wanaccm tu hata kama hawafai.

Magufuli ni mbaguzi hafai kuwa rais hata wa kundi la panya.
 
Haki za msingi za raia haziwezi kuwa substituted na miradi ya barabara tu.

Ni bora tusiwe na hizo barabara na midege ila haki na utu wetu viheshimiwe.
 
Kwa hili naweza kuandamana, ila sio mtu kashindwa eti niandamane Kwa ajiri huo ujinga, never ever
 
Zanzibar walikuwa na utaratibu wa kikatiba unaolazimisha mshindi wa kwanza na wa pili ktk kura za Urais kufanya kazi pamoja na kuunda serikali ya umoja wa kitaifa.

..Ndiyo maana kuna wakati Amani Karume wa CCM alikuwa Raisi na Maalim Seif Sharif Hamad wa CUF alikuwa Makamu wa Kwanza wa Raisi wa Serikali ya Zanzibar.

..Serikali ya Umoja wa kitaifa ya Zanzibar ilivurugika baada ya CCM kuamua kupora uchaguzi wa Znz mwaka 2015 baada ya kuonekana dhahiri kwamba Maalim Seif Sharif Hamad wa CUF ameshinda na anakwenda kuwa Raisi, na Dr.Mohamed Shein wa CCM anakwenda kuwa Makamu wa Kwanza wa Raisi.

..Kwa hiyo, pendekezo lako ni zuri, na linaweza kabisa kufanyiwa kazi kama ilivyokuwa kwa Zanzibar, ila tatizo ni wana CCM ambao siku zote hawakubaliani na dhana kwamba, penye ushindani pana kushinda na kushindwa. Kilichotokea Zanzibar kinathibitisha ukweli huo.
 
Hakuna MTU jasiri na mwerevu anaweza Fanya kazi na Jiwe.
Unahitaji kuwa mnafiki na mramba viatu ndio utamudu kufanya kazi na Stone.
Hata hivyo hafai na hatumtaki tena..
MTU mbaguzi na mwenye roho mbaya ya kikatili namna hii!!!
Kwa nchi zetu hizi zilizojaa watu wapenda misaada na wavivu wa Kufikiri, Magufuli ndiye anafaaa mno mkuu!

Kuna watu wavivu kiasi cha kuogopa hata kuoa akiogopa eti ataitunzaje familia yake mwenyewe hata kama lijamaa limeshafikisha umri wa kujitegemea, linajibanza banza Kwa wazazi Tu

Tanzania inamhitaji Magufuli kuliko inavyodhaniwa
 
Magufuli ame prove kwamba hajui chochote kwenye uongozi zaidi ya mabavu, vitisho, kufoka kukamata watu,kufunga watu, kufilisi watu.

Muda umefika aondoke, na ataondoka tu mwaka huu.

Iwe mvua like jua anaondoka, ni ujinga kuendelea kutawaliwa badala ya kuongozwa.

October 28, ondoa Pombe, ondoa makufuli.
 
Magufuli ame prove kwamba hajui chochote kwenye uongozi zaidi ya mabavu, vitisho, kufoka kukamata watu,kufunga watu, kufilisi watu.

Muda umefika aondoke, na ataondoka tu mwaka huu.

Iwe mvua like jua anaondoka, ni ujinga kuendelea kutawaliwa badala ya kuongozwa.

October 28, ondoa Pombe, ondoa makufuli.
Daa!! Mkuu mbona unatoa jibu la kigaidi aisee!!

Ujue ataondolewa Kwa Kura eeeh!!

Na wapiga Kura, wewe ni mmoja tu Kati ya wapigakura 29M+
Inakuwa vipi mkuu unakuwa na jibu Hilo kana kwamba wewe ndio idadi ya wapiga Kura wote

Mfano, wewe ni mmoja tu utayempa Kura Lisu, lakini na Mimi nitampa Magufuli, huoni hapo tayari Magufuli na Lisu wako Sawa Kati wapiga Kura wawili Mimi na wewe?

Kwa nini sasa useme kirahis Tu ni lazima aondolewe mkuu?
 
Ok, Kama wewe kura yako umeamua ikaharibikie kwake, fanya hivyo lakini usimatemate hoja kulazmisha na wengine wafikiri unavyofikiri wewe!

Mtu aliyebomolewa bila fidia nyumba yake aliyojenga kwa kiinua mgongo hawezi kukuelewa maana ukizunguzia Magufuli tena maana yake fidia ya nyumba yake ipotee moja kwa moja!

Mfanyakazi wa selekali, ukimwambia habari ya Magufuli tena, manake aendelee kuteseka na mshahara usiopanda daraja, malengo ya ujenzi au kusomesha watoto kwake yaendelee kuwa ndoto!

Mnufaika wa HESLB na yeye manake aendelee kuumia na makato ya 15%! Wakulima, Wavuvi, Wafanya biashara na wasio naajira nao wana machungu wasiyopenda yaendelee, Wanataka nafuu ya maisha! Hivyo kama wewe ni mnufaika wa utawala huu ni wewe na wenzako wachache mnaovaa kijani, lakinini massive ni wahanga wa utawala huu!
 
Daa!! Mkuu mbona unatoa jibu la kigaidi aisee!!

Ujue ataondolewa Kwa Kura eeeh!!

Na wapiga Kura, wewe ni mmoja tu Kati ya wapigakura 29M+
Inakuwa vipi mkuu unakuwa na jibu Hilo kana kwamba wewe ndio idadi ya wapiga Kura wote
Tuko wengi sana tusiopenda kufokewa, tusiopenda kutawaliwa, tusiopenda kuona watu wanafungwa na kuwekwa mahabusu bila makosa, tuko wengi zaidi ya milioni 30 tusiopenda kunyanyaswa na kuimizwa kwa amri zake.

Magufuli Ataondoka tu kwa kura zetu, October 28 ndio mwisho kudhulumu na kuwaonea wananchi.
 
Back
Top Bottom