Licha ya CCM kutufikisha hapa tulipo, Magufuli analeta tumaini jipya

konda msafi

JF-Expert Member
Sep 5, 2018
1,666
8,582
Kwa kweli nimejikuta nampenda Magufuli ghafla. CCM ndio imetufikisha hapa tulipo lakini kwa jinsi alivyowachana hawa mafisadi wa hela za wafanyakazi amenifanya nipate imani juu ya utendaji wake.

Kama ningekuwa na uwezo wa kumuomba Mwenyezi Mungu na akatekeleza maombi yangu, ningemuomba wapinzani wote wa Tanzania wamsamehe rais chochote kile ambacho wanadhani anahusika.

Na yeye rais awasamehe kwa yote waliyomkosea na ningemuomba kesi zote zilizopo mahakamani dhidi ya wapinzani zisizokuwa na kichwa wala miguu azifute (kama anayo hayo mamlaka). Pia ningeomba ushirikano kati ya Tanzania na jumuia ya kimataifa uimarishwe kwa ajili ya maslahi mapama ya nchi. Tuungane tujenge Tanzania moja. Hakuna sababu ya kupingana ilihali wote tunajenga taifa moja.

Ningeomba viongozi wote wa upinzani wafanye kazi pamoja na serikali kwa manufaa ya taifa. Kama inawezekana wakina Tundu Lisu, Freeman Mbowe, John Mnyika, Godbless Lema na wapinzani wengine wenye uwezo na wawajibikaji wapewa nyadhifa serikalini. Wasameheane, wajenge Tanzania moja. Umoja wa kitaifa uanzie kwa viongozi wetu wa vyama na serikali ushuke hadi huku chini kwa raia wa kawaida.

Kwa kweli Magufuli ameongea ukweli kabisa tena kwa kupiga mulemule. Tunahitaji rais wa namna hii, anayejua kero na matakwa ya raia wake. Kila mtu anajua hakuna mkamilifu chini ya jua.

Hivyo rais ni binadamu kama mimi na wewe, anaweza kukosea pia. Hivyo tuangalie mazuri yake. Leo kawasemea wafanyakazi vizuri sana.
 
Kwa kweli nimejikuta nampenda Magufuli ghafla. CCM ndio imetufikisha hapa tulipo lakini kwa jinsi alivyowachana hawa mafisadi wa hela za wafanyakazi amenifanya nipate imani juu ya utendaji wake. Kama ningekuwa na uwezo wa kumuomba Mwenyezi Mungu na akatekeleza maombi yangu, ningemuomba wapinzani wote wa Tanzania wamsamehe rais chochote kile ambacho wanadhani anahusika. Na yeye rais awasamehe kwa yote waliyomkosea na ningemuomba kesi zote zilizopo mahakamani dhidi ya wapinzani zisizokuwa na kichwa wala miguu azifute (kama anayo hayo mamlaka). Pia ningeomba ushirikano kati ya Tanzania na jumuia ya kimataifa uimarishwe kwa ajili ya maslahi mapama ya nchi. Tuungane tujenge Tanzania moja. Hakuna sababu ya kupingana ilihali wote tunajenga taifa moja. Ningeomba viongozi wote wa upinzani wafanye kazi pamoja na serikali kwa manufaa ya taifa. Kama inawezekana wakina Tundu Lisu, Freeman Mbowe, John Mnyika, Godbless Lema na wapinzani wengine wenye uwezo na wawajibikaji wapewa nyadhifa serikalini. Wasameheane, wajenge Tanzania moja. Umoja wa kitaifa uanzie kwa viongozi wetu wa vyama na serikali ushuke hadi huku chini kwa raia wa kawaida. Kwa kweli Magufuli ameongea ukweli kabisa tena kwa kupiga mulemule. Tunahitaji rais wa namna hii, anayejua kero na matakwa ya raia wake. Kila mtu anajua hakuna mkamilifu chini ya jua. Hivyo rais ni binadamu kama mimi na wewe, anaweza kukosea pia. Hivyo tuangalie mazuri yake. Leo kawasemea wafanyakazi vizuri sana.
Kumbeeee
IMG_20181228_122642.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza Mungu mwenyewe hapatani na kila mtu sasa unatakaje Rais apatane na kilamtu?
Pili,kukosoana ndio kunamfanya aboreke maana hata kuhusu mafao amekosolewa sana yeye na serikali take.
Tatu,aliyoyasema sio mageni hata wapinzani wamekwisha kuyasema hayo na mengine mengi sana pasi na kusikilizwa.
Nne,hakuna hatua inayopigwa pale unaporudi nyuma hatua moja kisha ukarudi mbele ulipokuwa kwa hatua hiyo moja,wenye akili watakushangaa unasifia nini hasa.
Tano,kupingana ni afya kwa wenye akili,swala la kujenga nyumba moja tusigombee fito ni ujinga maana yawezekana mwenye fito hajui kujenga na anaiba fito zenyewe!! Mengine fikiria mwenyewe nje ya box
 
Yeye ndiye aliyesaini huo muswada wa hiyo sheria ya kikokotowo halafu leo anajifanya anamshangaa waziri kwa kupeleka huo muswada bungeni!, anajifanya eti sasa anawatetea wafanyakazi ambao ni miezi michache tu iliyopita yeye ndiye aliyeweka saini hiyo sheria ya kikokotowo!

Kweli Wadanganyika ni rahisi kweli kuwadanganya, wewe wape pipi na maneno mataaaamu umeshawaroga!
 
Magufuli ni rais mzuri sana.
Na angekuwa best Rais ever ever.

Kama angekuwa hachukii wapinzani.
Basi.
Kweli kabisa mkuu. Huyu jamaa angekuwa hana tatizo na wapinzani HAKI YA MUNGU ANGEKUWA THE BEST PRESIDENT EVER. Natamani ningekuwa mshauri wake nikamuonyesha sehemu ile ndogo tu anayokosea. Huyu jamaa angepiga hatua kubwa sana. Anavyosema hii nchi ingekuwa kweli donor country. Angepata uungwaji wa kila mtu.
 
Kweli kabisa mkuu. Huyu jamaa angekuwa hana tatizo na wapinzani HAKI YA MUNGU ANGEKUWA THE BEST PRESIDENT EVER. Natamani ningekuwa mshauri wake nikamuonyesha sehemu ile ndogo tu anayokosea. Huyu jamaa angepiga hatua kubwa sana. Anavyosema hii nchi ingekuwa kweli donor country. Angepata uungwaji wa kila mtu.
Hivi nyie mnaomsifia,mnajitambua,na akili zenu zipo sawasawa kweli?.Ni mashaka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yeye ndiye aliyesaini huo muswada wa hiyo sheria ya kikokotowo halafu leo anajifanya anamshangaa waziri kwa kupeleka huo muswada bungeni!, anajifanya eti sasa anawatetea wafanyakazi ambao ni miezi michache tu iliyopita yeye ndiye aliyeweka saini hiyo sheria ya kikokotowo!

Kweli Wadanganyika ni rahisi kweli kuwadanganya, wewe wape pipi na maneno mataaaamu umeshawaroga!
Kwanini atatue hilo swala jamani, sasa sisi UFIPA tutamponda wapi Raisi wetu Mpendwa Magufuli kwa utendaji wake kikazi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa kweli nimejikuta nampenda Magufuli ghafla. CCM ndio imetufikisha hapa tulipo lakini kwa jinsi alivyowachana hawa mafisadi wa hela za wafanyakazi amenifanya nipate imani juu ya utendaji wake. Kama ningekuwa na uwezo wa kumuomba Mwenyezi Mungu na akatekeleza maombi yangu, ningemuomba wapinzani wote wa Tanzania wamsamehe rais chochote kile ambacho wanadhani anahusika. Na yeye rais awasamehe kwa yote waliyomkosea na ningemuomba kesi zote zilizopo mahakamani dhidi ya wapinzani zisizokuwa na kichwa wala miguu azifute (kama anayo hayo mamlaka). Pia ningeomba ushirikano kati ya Tanzania na jumuia ya kimataifa uimarishwe kwa ajili ya maslahi mapama ya nchi. Tuungane tujenge Tanzania moja. Hakuna sababu ya kupingana ilihali wote tunajenga taifa moja. Ningeomba viongozi wote wa upinzani wafanye kazi pamoja na serikali kwa manufaa ya taifa. Kama inawezekana wakina Tundu Lisu, Freeman Mbowe, John Mnyika, Godbless Lema na wapinzani wengine wenye uwezo na wawajibikaji wapewa nyadhifa serikalini. Wasameheane, wajenge Tanzania moja. Umoja wa kitaifa uanzie kwa viongozi wetu wa vyama na serikali ushuke hadi huku chini kwa raia wa kawaida. Kwa kweli Magufuli ameongea ukweli kabisa tena kwa kupiga mulemule. Tunahitaji rais wa namna hii, anayejua kero na matakwa ya raia wake. Kila mtu anajua hakuna mkamilifu chini ya jua. Hivyo rais ni binadamu kama mimi na wewe, anaweza kukosea pia. Hivyo tuangalie mazuri yake. Leo kawasemea wafanyakazi vizuri sana.

habari ndiyo hii hapa.......
20181228_135344.jpg
 
Kweli kabisa mkuu. Huyu jamaa angekuwa hana tatizo na wapinzani HAKI YA MUNGU ANGEKUWA THE BEST PRESIDENT EVER. Natamani ningekuwa mshauri wake nikamuonyesha sehemu ile ndogo tu anayokosea. Huyu jamaa angepiga hatua kubwa sana. Anavyosema hii nchi ingekuwa kweli donor country. Angepata uungwaji wa kila mtu.
Wapinzani ndio wanajifanya kumchukia, sasa unataka awabembeleze? Sahau.
 
Magufuli ni rais mzuri sana.
Na angekuwa best Rais ever ever.

Kama angekuwa hachukii wapinzani.
Basi.
Mimi siamini kama Rais anachukia wapinzani isipokuwa vyama vya upinzani vya kiafrica na uarabuni ni aina ya vyama vipo kwaajili ya kukwamishana ili ukikwama waje mbele ya wananchi waseme wao watafanya! hapa ndipo chance inapotkea kwa mabeberu kutuchonganisha na mwisho wa siku kuingiza siraha zao kusababisha machafuko.
 
Mimi siamini kama Rais anachukia wapinzani isipokuwa vyama vya upinzani vya kiafrica na uarabuni ni aina ya vyama vipo kwaajili ya kukwamishana ili ukikwama waje mbele ya wananchi waseme wao watafanya! hapa ndipo chance inapotkea kwa mabeberu kutuchonganisha na mwisho wa siku kuingiza siraha zao kusababisha machafuko.
Ukweli ndio huo. Tatizo vyama tawala huko nyuma vilijisahau sana, hivyo wapinzani wana legitimacy reason ya kuviondoa hivi vyama tawala. So kungekuwa vyama tawala vipo kwa ajili ya manufaa ya wananchi kusingekuwa na haja ya upinzani wa namna hii. Ungekuwepo upinzani "constructive" kama ilivyo Marekani na Ulaya. Ufisadi wa vyama vya ukombozi ndio umepelekea bara la africa kutoendelea kiuchumi. Hivyo vyama vya upinzani vina sababu ya msingi kuvipinga vyama vya ukombozi ambavyo ndio vyama tawala.
 
Ukweli ndio huo. Tatizo vyama tawala huko nyuma vilijisahau sana, hivyo wapinzani wana legitimacy reason ya kuviondoa hivi vyama tawala. So kungekuwa vyama tawala vipo kwa ajili ya manufaa ya wananchi kusingekuwa na haja ya upinzani wa namna hii. Ungekuwepo upinzani "constructive".
Sidhani ujue lengo la chama chochote ni kushika dola sasa hapa ujue kwa siasa zetu za kiafrica sidhani kama chama cha upinzani kitakuwa tayari kukipa ushirikiano wa kweli chama tawala ili kiendelee kubaki madarakani!

Chukulia mfano ingekuwa bunge letu lina 60% ya wabunge wa upinzani, Je! wapinzani wangekubali kupitisha bajeti ya SGR? Ununuzi ndege? Ujenzi wa bwawa la umeme kule Rufiji? Mwisho wa siku ile ripoti ya mazingira ndiyo ingekutumika kutukwamisha kama wakivyosema Choo kijengwe km 10 toka eneo la project sa sijui wanataka wafanyakazi washinde njiani kwenda kuchimba dawa.
 
Sidhani ujue lengo la chama chochote ni kushika dola sasa hapa ujue kwa siasa zetu za kiafrica sidhani kama chama cha upinzani kitakuwa tayari kukipa ushirikiano wa kweli chama tawala ili kiendelee kubaki madarakani!

Chukulia mfano ingekuwa bunge letu lina 60% ya wabunge wa upinzani, Je! wapinzani wangekubali kupitisha bajeti ya SGR? Ununuzi ndege? Ujenzi wa bwawa la umeme kule Rufiji? Mwisho wa siku ile ripoti ya mazingira ndiyo ingekutumika kutukwamisha kama wakivyosema Choo kijengwe km 10 toka eneo la project sa sijui wanataka wafanyakazi washinde njiani kwenda kuchimba dawa.
You have point my brother. Honestly you have a point. Binafsi siipendi ccm simply because ya huu umaskini iliyowasababishia watanzania. Lakini kusema kweli Magufuli anajitahidi. Na kama ulivyosema kama 60% ya wabunge wangekuwa wapinzani hii miradi isingeungwa mkono bungeni. Ila tungekuwa na chama kinachojali maslahi ya wananchi tokea uhuru hii miradi ingeungwa mkono tu hata kama asilimia kubwa bungeni ingekuwa wapinzani maana tungekuwa matured enough na tuliostaarabika kuunga mkono chochote chenye tija kwa taifa kama ilivyo marekani na ulaya. Marekani na ulaya hata upinzani huunga mkono pale kwenye maslahi hata kwa miswada inayoletwa na chama tawala.
 
Back
Top Bottom