Chagu wa Malunde
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 8,708
- 5,711
Hichi kituo cha kutetea haki za binadamu hakina msaada wowote kwa raia wa kawaida na inaonekana wao wapo kisiasa tu na kujaza matumbo yao kwa misaada ya pesa wanayopata toka huko nje.
Wapo tayari kupiga kelele na kulaani pale wanasiasa wa upinzani wanapokamatwa au alipokamatwa mfanyakazi wao Tito Magoti wameenda mbali mpaka kufungua kesi Mahakama Kuu. Lakini raia wa kawaida na wanyonge hawasaidiwi kabisa na hawa jamaa.
Mfano, kuna mama kule Mwanza mume wake aliteswa na migambo na wanajeshi mpaka kufa. Alivyowafuata hakuna msaada waliompa. Mwakilishi wao kule Mwanza anasema eti kesi ngumu kisa Mwanajeshi na migambo walitesa na kuua.
Je, Mgambo au mwanajeshi ana kinga ya kuua?
Kwa ujumla LHRC ni ajili ya propaganda tu.
Wapo tayari kupiga kelele na kulaani pale wanasiasa wa upinzani wanapokamatwa au alipokamatwa mfanyakazi wao Tito Magoti wameenda mbali mpaka kufungua kesi Mahakama Kuu. Lakini raia wa kawaida na wanyonge hawasaidiwi kabisa na hawa jamaa.
Mfano, kuna mama kule Mwanza mume wake aliteswa na migambo na wanajeshi mpaka kufa. Alivyowafuata hakuna msaada waliompa. Mwakilishi wao kule Mwanza anasema eti kesi ngumu kisa Mwanajeshi na migambo walitesa na kuua.
Je, Mgambo au mwanajeshi ana kinga ya kuua?
Kwa ujumla LHRC ni ajili ya propaganda tu.