LHRC kuna viongozi Watanzania?

Mudawote

JF-Expert Member
Jul 10, 2013
10,003
12,466
Na David Maphone

Niko bize kwa siku kadhaa sasa nikijipa kibarua cha kusaka taarifa za mashirika ya kutetea haki za binadamu nchini Tanzania ili kuona wametekeleza kwa kiwango gani jukumu lao la msingi kwenye kipindi hiki kigumu cha ugojwa hatari wa Corona ( COVID 19).

Watanzania walio wengi nikiwemo na mimi nilitegemea kusikia matamko ya kuwatetea watu masikini kutokana na Wafanyabiashara kupandisha bei za vifaa kinga vya kupambana na maambukizi ya Virusi vya Corona (Coronavirus)

Kwa uhodari ule ule mliokuwa mkitumia kuwatetea CHADEMA mpaka baadhi ya watanzani kufikia kuamini kwamba mashirika ya kutetea haki nchini Tanzania ni matawi rasmi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)

MNATIA SHAKA SANA
Liko wapi tamko la Legal and Human Rights Center (LHRC) kwenye sakata hili? Mbona sioni povu la kituo hiki ilihali Watanzania wa kawaida wanapokwa uhai wao na wafanyabiasha wenye tamaa za mali kuliko utu.

Pengine nimeharakia sana labda mnajipanga kwa ajili ya kufanya utetezi wa sakata hili kwa muda mtakaona muafaka kwenu au suala hili limekosa umuhimu katika mashirika yenu.

USHAURI WANGU
Wakati mwingine mjikite kwenye kutetea utu na maisha ya watu kuliko kuelekeza nguvu zenu kwenye masuala ya kisiasa. Mnapoteza imani kubwa sana kwa Watanzania.

MTANZANIA CHUKUA HATUA JIKINGE NA CORONA.

Narudi tena hapa hapa!


Mwandishi: David Maphone.
0653246600
Dar es Salaam, Tanzania.
 
LHRC haifanyi kazi kwa kukurupuka kama mnavyodhani!

Ninachokiona hapa ni kwamba una chuki na taasisi hiyo kiasi kwamba ulikuwa unatafuta sababu ya kuwasema vibaya!

Taasisi hiyo inadeal na haki za binadamu, its so obvious mara nyingi wataonekana kuwa tofauti na serikali maana matokeo ya aina ya utawala ndio huweka mstari wa haki za binadamu!

Hata CHADEMA wakishika nchi leo, kesho unaweza kuhisi LHRC waki chama cha upinzani CCM!
 
Hiyo siyo kazi ya LHRC!

Kama bidhaa zinapanda bei ni wajibu wa serikali kudhibiti. Na bahati nzuri serikali imeshakemea!

Ulitakaje kwani?
 
Ukiambiwa umevurugwa unalia lia hapa jamvini, nani kakwambia kuwa hao wana husika na kuwatetea wagonjwa? Mudawote,

In God we Trust
 
Mmawia kuwa na roho ya ubinaadamu rafiki.
We jamaa umepata ubinadamu lini?Mbonanunajionesha upuuzi wako hapa.hiyo taasisi inajihusisha nini na mambo ya korona ?Halafu unakurupuka tu unataka likitokea jambo wao watoe tamko wenzako wanakaa wanatulia wanaandika.Hicho sio kama chama cha ccm ambacho Bashiru analopoka lolote au polepole.Wao wakitoa tamko wanatoa kama taasisi sio kama mtu mmoja.Kwa hiyo kama unatamani kuona tamko lao subiri.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na David Maphone

Niko bize kwa siku kadhaa sasa nikijipa kibarua cha kusaka taarifa za mashirika ya kutetea haki za binadamu nchini Tanzania ili kuona wametekeleza kwa kiwango gani jukumu lao la msingi kwenye kipindi hiki kigumu cha ugojwa hatari wa Corona ( COVID 19).

Watanzania walio wengi nikiwemo na mimi nilitegemea kusikia matamko ya kuwatetea watu masikini kutokana na Wafanyabiashara kupandisha bei za vifaa kinga vya kupambana na maambukizi ya Virusi vya Corona (Coronavirus)

Kwa uhodari ule ule mliokuwa mkitumia kuwatetea CHADEMA mpaka baadhi ya watanzani kufikia kuamini kwamba mashirika ya kutetea haki nchini Tanzania ni matawi rasmi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)

MNATIA SHAKA SANA
Liko wapi tamko la Legal and Human Rights Center (LHRC) kwenye sakata hili? Mbona sioni povu la kituo hiki ilihali Watanzania wa kawaida wanapokwa uhai wao na wafanyabiasha wenye tamaa za mali kuliko utu.

Pengine nimeharakia sana labda mnajipanga kwa ajili ya kufanya utetezi wa sakata hili kwa muda mtakaona muafaka kwenu au suala hili limekosa umuhimu katika mashirika yenu.

USHAURI WANGU
Wakati mwingine mjikite kwenye kutetea utu na maisha ya watu kuliko kuelekeza nguvu zenu kwenye masuala ya kisiasa. Mnapoteza imani kubwa sana kwa Watanzania.

MTANZANIA CHUKUA HATUA JIKINGE NA CORONA.

Narudi tena hapa hapa!


Mwandishi: David Maphone.
0653246600
Dar es Salaam, Tanzania.
Hiki ndicho ninachokiona hapa.
IMG_20200320_113338.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom