LHRC: Gari la CCM liliwatangazia wananchi Igunga kuwa Kashindye kajitoa

EasyFit

JF-Expert Member
Jul 4, 2011
1,269
1,082
Mtandao wa uangalizi wa uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Igunga mkoani Tabora, umetoa tathmini yao na kusema kuwa zoezi hilo liligubikwa na kasoro nyingi zikiwemo za wapiga kura kuhongwa pombe, kuahidiwa kupewa nyama, kuuza shahada zao baadhi ya Mawaziri kuingilia mchakato huo pamoja na wananchi kurubuniwa kuwa mgombea wa Chadema kajitoa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaa jana, Mkuu wa kitengo cha uchaguzi kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Merick Luvinga, alisema walibaini kasoro hizo kabla ya upigaji kura na siku ya kupiga kura Jumapili iliyopita.

Uangalizi wa uchaguzi huo ulifanywa na Mtandao unaojumuisha mashirika 17 yasiyokuwa ya kiserikali ikiwemo LHRC ambapo wamesema maeneo mbalimali wanasiasa walihonga pombe, nyama na mawaziri kufanya shughuli zisizowahusu.

Mtandao huo ulipeleka waangalizi 243 na kila kata ikiwa na waangalizi 26.

Luvinga alisema siku ya kupiga kura, walishuhudia watu wakiwa wamenunuliwa pombe na wagombea na kunywa jirani na kituo cha kupigia kura pamoja na kupewa nyama ili kuwashawishi kuwachagua watu waliowahonga.

Aidha, alisema siku ya kupiga kura, gari la Mbunge mmoja wa mkoani Tabora lilipita mitaani na kuwatangazia wananchi kuwa mgombea wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Joseph Kashindye, alikuwa amejitoa katika kugombea nafasi ya ubunge hivyo wamchague mgombea wa CCM, Dk. Peter Kafumu.

Alieleza kasoro nyingine zilizojitokeza katika uchaguzi huo kuwa ni pamoja na watendaji wa vijiji kugawa mahindi kwa wapiga kura kwa lengo la kuwashawishi wamchague mgombea kutoka chama fulani.

Luvinga alisema waangalizi hao baada ya kuona matukio hayo, walipiga simu Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), lakini hawakupata msaada wowote.


Source: Nipashe
 
pamoja na kufanya yote hayo kununua pombe, nyama, kugawa Pesa n.k, lakini wamekula kwata la kutosha kutoka kwa Makamanda wa CDM na sidhani kama Kafumu atakubali kurudi tena ulingoni 2015 au kama kuna kiongozi wa CCM atakayerudi Igunga kukampeni...
 
Nimesoma gazeti moja leo eti watu walipewa nyama ya Mbuni wakadanganywa ni ya ng'ombe wakaichagua ccm. Kiukweli ccm imewadhalilisha wananchi wa Igunga yaani kumhonga mtu nyama kilo 1 ni dharau ya hali ya juu, sasa hiyo nyama atakula miaka mingapi. Na hao wanaharakati walikuwa wapi kuwaeleza wanaigunga hayo ndo wajitokeze saiv?
 
Nimesoma gazeti moja leo eti watu walipewa nyama ya Mbuni wakadanganywa ni ya ng'ombe wakaichagua ccm. Kiukweli ccm imewadhalilisha wananchi wa Igunga yaani kumhonga mtu nyama kilo 1 ni dharau ya hali ya juu, sasa hiyo nyama atakula miaka mingapi. Na hao wanaharakati walikuwa wapi kuwaeleza wanaigunga hayo ndo wajitokeze saiv?
Safari bado ni ndefu lakini inshallah tutafika.
 
pamoja na kufanya yote hayo kununua pombe, nyama, kugawa Pesa n.k, lakini wamekula kwata la kutosha kutoka kwa Makamanda wa CDM na sidhani kama Kafumu atakubali kurudi tena ulingoni 2015 au kama kuna kiongozi wa CCM atakayerudi Igunga kukampeni...
We fikiri tofauti ya kura na mbinu chafu walizotumia.
 
Jamani jama, inamaana uwezo wa mtz mwenzetu wa kufikiria na kufanya maamuzi unanunuliwa kwa Shs 4,500 (kilo moja ya nyama). Ndo maana na wawakilishi wanauza rasilimali ovyo ovyo (wanyamapori, madini, nk).
 
pamoja na kufanya yote hayo kununua pombe, nyama, kugawa Pesa n.k, lakini wamekula kwata la kutosha kutoka kwa Makamanda wa CDM na sidhani kama Kafumu atakubali kurudi tena ulingoni 2015 au kama kuna kiongozi wa CCM atakayerudi Igunga kukampeni...

Mpira ni magoli na sio changa.
 
pamoja na kufanya yote hayo kununua pombe, nyama, kugawa Pesa n.k, lakini wamekula kwata la kutosha kutoka kwa Makamanda wa CDM na sidhani kama Kafumu atakubali kurudi tena ulingoni 2015 au kama kuna kiongozi wa CCM atakayerudi Igunga kukampeni...

Siongezi lolote kijana nisije haaribu uliyo mwaga hapa .Ila kama kesi inaenda Mahakamani CCM itaanguka chali maana ushahidi kila kona na muuza nyama atasema kwa nini aliua mifugo 3 kwa hasara na furaha gani .
 
We fikiri tofauti ya kura na mbinu chafu walizotumia.
Kama jimbo moja wametumia Bil.3 fikiria majimbo zaidi ya 200 ongeza na urais watatumia sh. ngapi halafu at the end of the day waambulie 50.3% ya kura zote, and for how long will this keep on happening?
 
pamoja na kufanya yote hayo kununua pombe, nyama, kugawa Pesa n.k, lakini wamekula kwata la kutosha kutoka kwa Makamanda wa CDM na sidhani kama Kafumu atakubali kurudi tena ulingoni 2015 au kama kuna kiongozi wa CCM atakayerudi Igunga kukampeni...

Ukizungumzia kurudi 2015 ni mbali sana kwani kwa ushahidi uliopo sijui kama atanusurika kesi ya uchaguzi. kumbuka pia Magufuli aliwaambia wana Igunga wakimchagua Kafumu hawatajengewa lile daraja la Mbutu; sidhani kama hii ni sawa
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom