Let's share: Uliwahi kusaidiwa na mtu usiyemfahamu kabla (msamaria mwema)? Kipi kilitokea?

Infantry Soldier

JF-Expert Member
Feb 18, 2012
15,893
16,317
Good evening members.

Mimi niliwahi kusaidiwa na mtu niliyekuwa simjui au mtu baki mwaka 2003.

Huyu dada alikuwa ni askari police. Hata mimi nilishangaa sana kusaidiwa na police.

Nilikuwa ninatoka Kigoma sasa narudi dar. Baada ya kushuka kutoka katika bus pale Ubungo nikaenda moja kwa moja kwenye kituo cha daladala kusubiri gari za kunipeleka Kariakoo ili nipande tena gari za kuelekea Tandika.

Kwa bahati mbaya kabla hata sijapanda gari nikakuta pochi yangu pamoja na simu vyote havipo. Nikaenda straight mpaka kituo kidogo cha police mule ubungo bus terminal kutoa taarifa.

Nikaandikisha kila kitu mpaka vitambulisho vyote vilivyopotea kasoro pesa ambazo walisema kuwa hawawezi kuandika kwa maana huwa hazipatikanagi.

Nikamwambia yule dada wa mapokezi kuwa kwa kuwa nimeibiwa pochi yangu yote pamoja na pesa sikuwa hata na nauli ya kunifikisha tandika, yule dada kwa huruma yake akaingia mfukoni mwake akatoa shillings 5,000 akanipa kama nauli.

Nilimshukuru sana kwa maana bila vile nilikuwa ninadhalilika sana that night. Thanks to God I met that good Samaritan. Hayo ndio yalinikita mimi na mengine mengi tu.

Jamani tusidharau watu baki huwezi kujua kesho nani atakuja kukubeba akupeleke kwa hospital.

Kama na wewe uliwahi kusaidiwa na mtu baki kama ilivyonikuta mimi naomba tu shee hapa wakuu.

Ninawasilisha.

Karibuni sana.
 
Speaking of nauli dahhh nimetoa sana nauli kwa watu, watoto wa shule ndo usiseme.. Wakubwa ndo kbs nashindwa kukataa Nampa fasta mana naona huruma kweli unakuta mtu ana mvi kbs anakwambia mwanangu sina nauli hapa...
Ss sijui wengine huwaga ni chuma ulete..Mungu nilinde wema usije niponza
 
Aprili 2008, Maputo Msumbiji
Kuna hoteli inaitwa Rovuma ipo katikati ya jiji tulivamiwa usiku saa tisa tukaporwa kila kitu. Kuna dada mmoja raia wa Kenya aliposikia mimi ni mtz alinichukua kwake na nikaishi mwezi mzima na kila kitu alinisaidia. Nililia sana mwaka jana nilipopata smsn kutoka kwa mumewe kwamba kafariki kwa ajali akiwa Afrika Kusini. Alinichukulia kama kaka yake alisaidia sana, maana niliibiwa kila kitu hadi nguo. Mungu amlaze mahali pema.
 
Sitamsahau kaka Fulani nilikutana nae Arusha pale mianzini wakati nasoma chuo,,nlikua naeleke hospitali ile ya ENT ipo tanki la maji,nikasimama katika bar ile barabarani nile nlikua na njaa..
Nkakaa meza moja na mkaka hvi simjui,chakula kilivokuja nkamwambia waiter aisee chps zenu ndogo bora ningekula ndizi,yule kaka baada ya mda baada ya kuniskia nalalamika akamwita waiter akamwambia aniletew "rosti" aniongezee na chps...akaniuliza nlipokua naelekea,akampgia simu rafiki yake daktari nikaongea nae akanielekeza hospitali aliopo..bill ilivokuja akanilipa chakula na vinywaji jumla 18,000/=..(bill hii kwa kipindi nasoma chuo ni kubwa mno)
Baadae akaniaga akaondoka,,,hakuniomba namba ya simu wala kuniuliza jina...nlimshangaa ila alinisaidia maana nlikua na njaa na budget ilikua ef 5000 tu..

Namuombea kwa Mungu amfungulie milango ya rizki yule kaka..!!
Kuna watu wana mioyo ya ajabu sana,nataman nimuone tena ila ndo siwezi mkumbuka kabisa,ila natumai dua zangu zinamfikia.
 
Aprili 2008, Maputo Msumbiji
Kuna hoteli inaitwa Rovuma ipo katikati ya jiji tulivamiwa usiku saa tisa tukaporwa kila kitu. Kuna dada mmoja raia wa Kenya aliposikia mimi ni mtz alinichukua kwake na nikaishi mwezi mzima na kila kitu alinisaidia. Nililia sana mwaka jana nilipopata smsn kutoka kwa mumewe kwamba kafariki kwa ajali akiwa Afrika Kusini. Alinichukulia kama kaka yake alisaidia sana, maana niliibiwa kila kitu hadi nguo. Mungu amlaze mahali pema.
Inahuzunisha sana kaka
 
Sitamsahau kaka Fulani nilikutana nae Arusha pale mianzini wakati nasoma chuo,,nlikua naeleke hospitali ile ya ENT ipo tanki la maji,nikasimama katika bar ile barabarani nile nlikua na njaa..
Nkakaa meza moja na mkaka hvi simjui,chakula kilivokuja nkamwambia waiter aisee chps zenu ndogo bora ningekula ndizi,yule kaka baada ya mda baada ya kuniskia nalalamika akamwita waiter akamwambia aniletew "rosti" aniongezee na chps...akaniuliza nlipokua naelekea,akampgia simu rafiki yake daktari nikaongea nae akanielekeza hospitali aliopo..bill ilivokuja akanilipa chakula na vinywaji jumla 18,000/=..(bill hii kwa kipindi nasoma chuo ni kubwa mno)
Baadae akaniaga akaondoka,,,hakuniomba namba ya simu wala kuniuliza jina...nlimshangaa ila alinisaidia maana nlikua na njaa na budget ilikua ef 5000 tu..

Namuombea kwa Mungu amfungulie milango ya rizki yule kaka..!!
Kuna watu wana mioyo ya ajabu sana,nataman nimuone tena ila ndo siwezi mkumbuka kabisa,ila natumai dua zangu zinamfikia.
Amen. Kuna baadhi wanaguswa sana na matatizo ya watu.
 
Back
Top Bottom