Lets privatize Ikulu, Bunge na Mahakama

Kitila nyie sie ndio huwa mnalalamika kwamba ni hatari kubinafsishaji hata wa kiwanja cha Ndege.Haya ya kufikirika yanatoka wapi,I said No and i will stand on my Point.Cha msingi ni kuangalia jinsi ya kubadili Mfumo wa serikali zetu,hili ndilo tatizo per say.Tatizo siyo wanasiasa,Ni hawa watendaji ambao wanapenda kujilimbikizia Mali na mambo ya kazi zao za Ku Copy na Kupaste,Tutawaumbua wakti wa Bajeti ya Mwaka huu kama hawatajiandaa vizuri kukabiliana na Watanzania Majasiri kama sisi.,

Yes, sawa kabisa ni sisi. Lakini sidhani kwamba hoja ya Rev Kishoka ni rahisi kiasi unachokionyesha hapa. I think hoja yake humo ni kubwa na pana zaidi ya kubinafisisha serikali. At the very minimum, as I understood it, Rev Kishoka is simply venting out his frustrations over our failing government and the apparent lack of a credible alternative. I also share his frustrations, don't you?
 
Yes, sawa kabisa ni sisi. Lakini sidhani kwamba hoja ya Rev Kishoka ni rahisi kiasi unachokionyesha hapa. I think hoja yake humo ni kubwa na pana zaidi ya kubinafisisha serikali. At the very minimum, as I understood it, Rev Kishoka is simply venting out his frustrations over our failing government and the apparent lack of a credible alternative. I also share his frustrations, don't you?
It is not the first time for Rev. kishoka to express what he think should be chaged,But what has he done once again in different style.Nakushauri Rev. kishoka,Andika Barua kuelekeza kwa Rais,kama nifanyavyo mimi na najua watatelekeza..na matokeo mie nayaona.Mie namuunga Mkono,Mie nilishakata tamaa zamani sana,na sasa nimeamua kujiunga nao ili serikali ibadilike.Nachoamini na naamini kinawezekana ni vision 2010 tuhakikishe Vijana (hapa bila kuingalia itikadi)wanaingia madarakani na kuwang'oa hawa wazee waliolewa madaraka...mathalani Chenge@Natamani watu kama kitila,tuwemo katika Serikali na naamini Mabadiliko ya kweli yanalwtea na vijana makini wanoipenda Nchi yao.Yes I am and I need some changes.Lets Stand as one to make the better life for our fellow Tanzania.
 
Amani iwe kwako Rev.
Nakukumbusha yale mahubiri yetu ya 1954-1977.

KATIKA moja ya ahadi kumi za mwana-TANU kuna moja isemayo kila mwana-TANU alilazimika kuapa kuwa atakuwa tayari kwa namna yoyote ile kupambana na hatimaye kuwashinda adui.


Dhambi kubwa watawala waliyotenda ni kusahau miiko yao ya uongozi (ahadi za mwana TANU), wakaziona za kizamani zimepitwa na wakati, kwamba zama hizi ni zama mpya, Ni kwenda na wakati.

Tupambane na adui mpaka mwisho
 
It is not the first time for Rev. kishoka to express what he think should be chaged,But what has he done once again in different style.Nakushauri Rev. kishoka,Andika Barua kuelekeza kwa Rais,kama nifanyavyo mimi na najua watatelekeza..na matokeo mie nayaona.Mie namuunga Mkono,Mie nilishakata tamaa zamani sana,na sasa nimeamua kujiunga nao ili serikali ibadilike.Nachoamini na naamini kinawezekana ni vision 2010 tuhakikishe Vijana (hapa bila kuingalia itikadi)wanaingia madarakani na kuwang'oa hawa wazee waliolewa madaraka...mathalani Chenge@Natamani watu kama kitila,tuwemo katika Serikali na naamini Mabadiliko ya kweli yanalwtea na vijana makini wanoipenda Nchi yao.Yes I am and I need some changes.Lets Stand as one to make the better life for our fellow Tanzania.

Mhh Gembe,

Umeamua kujiunga nao leo ili serikali ibadilike? Na umesema kuwa kikwete akiandikiwa barua anatekeleza?
 
Rev, I understand your message; kweli tumechoka, mie kwa hii nakuunga mkono. Inatia uchungu sana hawa watu wanaopewa madaraka na wananchi wenye matumaini makubwa nao, kumbe ndiyo wezi. Vile vile you have a point here; think; Sumaye was a Prime minister for 10 solid years; but he confessed that before his post graduation at Havard Uni he didn't know why Tanzania was still poor, only after graduating from there then he got an answer! This man was a prime minister for 10 years and knew nothing! Simply he didn't know what he was doing! Kishoka I got you on this!!
 
Rev Kishoka umenikuna mahali. Mada yako inaonyesha namna umetumia muda kutafakari hatima ya Tz na kukuta hakuna mwanga mwisho wa reli. Hii ndio hali halisi. Inakatisha tamaa hata kuongelea ufisadi wa nchi yetu. Ni mwingi na umetapakaa kila kona kiasi kwamba hujui wapi pamezidi uchafu.
Kubinafsisha ikulu kwa hali ya kawaida ni kitu cha kushangaza. Ila kwa hali ya Tz vya kushangaza vilishaisha. Raisi mwingimne aliuza hata tausi wa ikulu; mwingine akahamia kabisa huko na extended family yake, akafungua na makampuni akiwa huko.
Aliyefuatia kaingiza uswahili, yaani baraza lake anzia juu akaweka mabingwa wa ufisadi; sasa cha kushangaza kimebaki kipi Tanzania hii?
Ikulu ikishakuwa mahali pa kunywa kahawa na kuandika mikataba binafsi basi ni kampuni kama kampuni nyingine, na ibinafsishwe tujue moja
 
The question is where do we go from here? Individually and JF as a group. We have identified the problem, now how do we go about bringing the solution? The CCM government is tired and overloaded with excess baggage, including corruption, lack of direction and lack of philosophy. Recently in my village I was talking to my older sister who had been for a long time a chairperson of CCM in the area. She has seen all the deception within her party and she surprised me by announcing she is joining CHADEMA. That to me is one way of dealing with the problem of leadership at a personal level. At a national level we need to strive to strengthen the opposition. Without the opposition haya makelele yote ya
Richmond na ufisadi yangefunikwa chini ya zulia.
 
Kwa system tuliyonayo sasa, hakuna matumaini ya Tanzania kubadilika na kuendelea na watanzania kuwa na maisha bora na raha. Tutaendelea tu kusema aaah Ulaya wameendelea sisi "maskini", tutaendelea kuwa na more Chenges, Karamagis, Mrambas, Vikwete and list goes on.
Kama wezi na mafisadi ndio wataendelea kuwa madarakani na kulindwa, a vibaka ndio watajaa segerea,
na kama inefficiency, corruption, porojo na fooling tricks zitandelea itafika siku watanzania tutachagua kubinafsisha ikulu yetu! Actually Mkapa is clever, dawa ya poor perfomace na inefficiency ni ubinafsishaji tu.
 
Bongolander,
Usikate tamaa ndugu yangu. Tanzania bila mafisadi inawezekana kabisa. Uwezo wa kubadilisha system umo mikononi mwetu. Tuutumie.
 
kuna mambo kadhaa ninayaona huko mbeleni

1:Zama za mipaka ya Kisiasa zitakwisha

kutokana na global warming athari zitakuwepo dunia nzima lakini zitatofautiana kati ya sehemu na sehemu moja ya sababu itakuwa ni geographic position kati ya sehemu na sehemu, katika sehemu kadhaa za ulimwengu hali itakuwa afadhali kuliko sehemu nyingine. kwa hiyo hali hiyo itasababisha wanadamu wahamie katika sehemu zenye afadhali. miongoni mwa sehemu zitakazokuwa na afadhali kwa mujibu wa hali ya kijiografia ni Tanzania, kwa hiyo nchi zenye nguvu lakini zilizoathirika na pollution na global warming zitaweka vikwazo vya kisera kuzilazimisha nchi zetu zifungue mipaka kwa watu wao ili wahamie huku kwetu kwenye hali ya hewa yenye afadhali kidogo, miongoni mwa vikwazo itakuwa ni kuwa ili upate misaada ya kiuchumi lazima ulegeze sheria za uhamiaji kwa watu wao.

Pointi nyingine itakayo sababisha wageni kuhamia katika nchi zetu ni kwamba kutokana na global warming kuyeyusha mabarafu katika actica na antactica baadhi ya visiwa vitazama, na watu katika visiwa hivyo itabidi wahamie katika nchi nyingine, nchi ambazo ni likely kuhamia itakuwa ni katika nchi zetu. kwa hiyo itaundwa sera ya dhahiri au siri kuhakikisha hawa watu wanakuwa accomodated katika nchi zetu.

Sera ya biofuel nayo itachangia wageni kurudi katika nchi zetu, mazao kwa ajili ya kuzalisha biofuel yatahitaji ardhi kubwa mno, na ili isiwepo conflict kati ya mazao yatakayotumika katika chakula na yale yatakayo tumika kwa ajili ya kuzalisha biofuel zitawekwa sera nzito kwa ajili ya kufanikisha ufanisi wa upatikananji wake wakubwa watatunga sera za kulazimisha serikali zetu kuwalinda wakulima wakubwa na hofu yangu ni kwamba serikali zetu zinaweza kulazimishwa kulegeza masharti ya uendeshaji wake kwa maana kwamba wageni wenye uwezo waruhusiwe kushika baadhi ya nyadhifa serikalini, na hapo ndo utakapokuwa mwanzo wa kubinafsisha serikali, na hii haitakuwa Tanzania tu bali itakuwa dunia nzima.

2:Masuala ya Majeshi(ya kivita) yataonekana kama mambo ya kizamani
na yataachwa.

kutokana na kwamba mipaka ya kisiasa itakosa nguvu , na binadamu wataingiliana, na kwamba mtu yeyote mwenye uwezo bila kujali rangi wala kbila wala jinsia wala ametoka wapi ndiye atakayetakiwa kuongoza basi ni dhahiri muda utafika Mtanzania mwenye uwezo ataajiriwa awe raisi wa marekani au popote pale, na mmarekani mwenye uwezo ataajiriwa awe raisi wa tanzania au popote pale, na kwa maana hiyo majeshi kwa ajili ya vita na nchi nyingine yatakosa umuhimu,kwa kuwa msamiati wa uzalendo wa kinchi utapungua nguvu , kwa sababu mtu atakuwa royal na pale alipo, akihamia sehemu nyingine atakuwa royal na pale, bali yatakuwepo majeshi ya polisi kwa ajili ya kulinda usalama wa ndani.
lakini hii ya kuhusu majeshi kuja kuachwa na wanadamu inaweza kutokea kutokana na kutokana na janga zito linaloweza kuletwa na vita, mfano vita vya nyuklia, baada ya vita kuisha na binadamu kufanya review ya majanga basi convetion wisdom itakuwa ni kwamba nchi ziache kuwa na majeshi kwa ajili ya vita,kwa sababu kuwa na majeshi ni sababu mojawapo ya kupigana vita hence cycle ya majanga tena
 
Kwanza nashukuru wote kwa kuchangia.

Swali kwenu, ikiwa kila kitu tulichonacho Serikali ikishindwa kukiendesha au kusimamia utendaji, inakimbilia kutafuta Wawekezaji au Wabia, kwa nini basi tusitafute Wawekezaji au Wabia kutoka nje ya nchi ili waongoze nchi yetu?

Tuna Katiba, Sheria na kanunu elfu zinazoongozwa na miongozo, itikadi, falsafa na ilaniza Chama/Vyama. Lakini kila siku tunashindwa kazi. tunashindwa kuwa wabunifu, wafanisi, wadadisi, wachapa kazi, waadilifu, wawajibikaji na kuishiwa kuwa wazembe, wahujumu, mafisadi, wavivu, wategaji na omba omba.

Ikiwa Serikali ambayo ndiyo inapaswa kutoa mwongozo na kuhamasisha uzalishaji mali inainua mikono juu na kusema tunatafuta wabia na wawekezaji kuokoa uzalishaji mali wa mashirika, viwanda, biashara na hata sasa kwenye kilimo, kutokana na kushindwa kuwa wabunifu na wenye kutumia juhudi na maarifa kuleta maendeleo ya kweli, je kuna faida gani kuwa ni Serikali ya watu wale wale ambao hata akija Rais mpya, hakuna litakalo badilijka?

Nyerere alikaa madarakani miaka 23. Mwinyi, Mkapa na Kikwete wamekalia kiti hicho hicho kwa miaka karibu 23. Katika miaka hiyo 46, Kikwete, Wasira, Msekwa, Malecela, Salim, Chenge, Sitta, Mzindakaya na wengine wengi, wameendelea kuwa viongozi (na wabunge) ndani ya Serikali na Chama na hata kuwa na sauti kubwa.

Sasa kama kwa miaka 46, wameshindwa kuwa na msukumo wa kweli wa kuleta maendeleo kwa Taifa na kupiga vita Ujinga, Maradhi na Umasikini na sasa kila mtu anakimbilia kutafuta "Panadol" ya kuuza kila kitu kwa Wageni wabia na wawekezaji si kauli jificho kuwa hatuwezi kujiongoza?

If that is the case, why not privatize the damn government? Let Mkoloni or Mwekezaji aje tuanze kupeta.

Interestingly, kila mahali alipo Mwekezaji na Mbia, kuna nidhamu ya hali ya juu, watu wanachapa kazi kwa bidii, ufanisi na ushindani. Inakuwaje sisi wenyewe tunashindwa kujitawala?

Je ni kosa letu wananchi au ni wale tunaowachagua na kuwapa dhamana ya kutuongoza wamekosa mwamko na kushindwa kutumia ipaswavyo sheria, kanuni na mipango ili kuhakikisha kuwa ama nidhamu ya kazi ina kuwa ni hiari na si mambo ya nidhamu ya woga, juhudi za maendeleo zinakuwa ni nia thabiti ya kila Mtanzania ili kuondokana na maadui watatu na si kujaza mifuko na hazina za wawekezaji?

Ni mpaka lini tutaendelea kusuasua katika hii safari ya kutokujijua? Hata tukimpa ndugu yangu Kitila au Zitto urais, je tunaamini tutabadilika na kuwa wachapakazi na watendaji mahiri, wafanisi, bunifu, adilifu na wawajibikaji? au tutadumisha Mizengwe kama kawaida?

Please someone go and search for Sir Richard Turnbull, lets privatise the damn country! and we can enjoy masufuria ya Misri!
 
Kwanza nashukuru wote kwa kuchangia.

Interestingly, kila mahali alipo Mwekezaji na Mbia, kuna nidhamu ya hali ya juu, watu wanachapa kazi kwa bidii, ufanisi na ushindani. Inakuwaje sisi wenyewe tunashindwa kujitawala?

Ni ushahidi tosha kuwa sisi ni watumwa tulio kamilika na hakuna wa kutuamsha toka hapo. Bora yule anayejua hivyo na kuchagua awe mtumwa wa namna gani kuliko kung'ag'ania kuwa tunaweza kuwa huru...Kuwa huru kivipi? Nasema sisi tumzaliwa kutawaliwa ambaye anaoana tofauti atufafanulie! Panga pagua sisi ni wafagizi, vijakazi, muflisi kifikra na kimtazamo..nani haoni hivyo? Bora kukubali yaishe..ushahidi? Huoni yanayoedelea miaka 46 ya madai ya uhuru etc..sisi ni viumbe destined for kutawaliwa...!
 
Kwanza nashukuru wote kwa kuchangia.



Ni ushahidi tosha kuwa sisi ni watumwa tulio kamilika na hakuna wa kutuamsha toka hapo. Bora yule anayejua hivyo na kuchagua awe mtumwa wa namna gani kuliko kung'ag'ania kuwa tunaweza kuwa huru...Kuwa huru kivipi? Nasema sisi tumzaliwa kutawaliwa ambaye anaoana tofauti atufafanulie! Panga pagua sisi ni wafagizi, vijakazi, muflisi kifikra na kimtazamo..nani haoni hivyo? Bora kukubali yaishe..ushahidi? Huoni yanayoedelea miaka 46 ya madai ya uhuru etc..sisi ni viumbe destined for kutawaliwa...!

AZIMIO
Huu ni ukweli kwanza ni lazima wote tutambue kuwa tunaumwa, kama tukitambua kuwa tunaumwa ndio tunaweza kutafuta dawa ya kututibu. Mimi leo mzungu akija ukiniambia you "niggers" can not even manage yourselves nanywea tu, na sio dharau wala ubaguzi ni kweli kabisa. Mpaka leo ukiangalia kazi aliyofanya mkoloni (shule, hospitali, barabara), ni nzuri kuliko waliyofanya viongozi wetu kwa miaka zaidi ya 40, sanasana tumerudi nyuma hatua nyingi tu, lakini ukweli huu kuutambua au kuukubali, hasa kwa watu walioko madarakani ni vigumu sana!
 
Azimio, Bongo,

Cha kusikitisha zaidi ni kuwa si unyonge wa wananchi kujisalimisha kwa "wageni" tuu, bali ni kubwa kwa watendaji na viongozi wetu.

Wasomi wetu wamekuwa mstari wa mbele, wakiungana na viongozi kutudhalilisha kwa kuona ya Mwekezaji ni mfalme wa mbingu ya saba.

Mnakumbuka jinsi gani tulivyohangaishwa kusafisha nchi, kupaka rangi na hata kuchapa Kanga na Vitenge vyenye taswira ya aliyetuletea mshiko wa MDC? Ilikuwaje serikali ikaamka ikawa makini kwa kila kitu, ulinzi, usalama, usafi, umeme, maji, uwajibikaji na kutunza saa ili kumfurahisha Bush, lakini michango ya muhimu kwa jamii na hata pale mambo ya dharura yanapotokea, kuna kujivutavuta kwa hali ya juu?

Njoo wawekezaji na wabia. Wao wanapewa zulia jekundu na vijiko vya dhahabu kama zawadi huku wakipewa misamaha ya kodi, ushuru na kuruhusiwa kufanya mambo wanavyotaka, mpaka sheria kupindishwa ili kukidhi matakwa ya wawekezaji! Mikataba yao na hata majina yao yanafichwa eti kumlinda mwekezaji na maslahi yake, hata pale inapodhihirika wazi kuwa mkataba unahujumu na unaweza kuliangamiza Taifa!

Tunauza uhuru na wajibu wetu kwa kumkingia kifua Mwekezaji na kulinda maslahi yake? Huko Buzwagi askari walivyopelekwa haraka kuvunja maandamano ya amani kudai haki, ndio kulinda maslahi ya Taifa?

Mimi nilitarajia waalimu wa mahali kama UDSM, wangekuwa wa kwanza kuleta mapinduzi ya kifikra ili kuondokana na uzezeta na zile nia za kuwa asimilated kwa wabia na wawekezaji, lakini kila mtu anapalilia tuta lake, huku tukishangaa Wanafunzi wanapofanya fujo?

Kama hatuwezi kuleta mbia na mwekezaji, basi millitarize the damn country!
 
Kishoka huku ni kukata tamaa na hakuna jambo baya kwa binadamu mwenye akili timamu kama kukata tamaa kwani anaweza kufikiri, kushawishi na hata kufanya lolote.

Watanzania wasikate tamaa kiasi hicho ambacho umefikia kwani ni hatari kwetu sote,
 
Kishoka huku ni kukata tamaa na hakuna jambo baya kwa binadamu mwenye akili timamu kama kukata tamaa kwani anaweza kufikiri, kushawishi na hata kufanya lolote.

Watanzania wasikate tamaa kiasi hicho ambacho umefikia kwani ni hatari kwetu sote,

I do not see any solutions in near future. 2010 and 2015 are still going to give us rotten products!

Tulichobakia ni kupiga kelele, kulalamika na kutoa maoni. Wanaopigiwa kelele hawasikilizi, masikio ya na nta tani mbili kama zile headphones za Bose!

Nilipoandika Thank God for giving us Kikwete, nilikuwa najipa tumaini, kuwa tunakoelekea kunaweza kuwa kwema.

Lakini kama kuzomewa kwa Mkapa kunasababisha vyombo vya Usalama na Serikali usakanye wazomeaji, huku mafisadi wanapeta, basi ni dhahiri bora arudi mkoloni tujue moja kuwa kamwe machoni pa Serikali hatuna haki na utu wetu hauthaminiwi.

Hapendwi mtu, ila Pochi!
 
Kishoka huku ni kukata tamaa na hakuna jambo baya kwa binadamu mwenye akili timamu kama kukata tamaa kwani anaweza kufikiri, kushawishi na hata kufanya lolote.

Watanzania wasikate tamaa kiasi hicho ambacho umefikia kwani ni hatari kwetu sote,

Mkuu, hali hii (ya kukata tamaa)unayoiona hapa JF-sehemu ya wasomi,wachambuzi, waelewa na wenye access na internet.

Huko vijijini watu walishakata tamaa long time !!! Kibaya zaidi na wa mijini nao sasa ndio wametambua machungu ambao wenzao wa vijijini wamekuwa nayo kwa muda mrefu sana.

Watanzania tumekata tamaa kwa sababu yooooote yameshasemwa lakini hakuna kinachofanyika.

Hiyo hatari unayosema si ya kufikirika, ipo tayari.Labda kinachosubiriwa ni wapi kutakuwa "point of rupture" ?
 
Kishoka huku ni kukata tamaa na hakuna jambo baya kwa binadamu mwenye akili timamu kama kukata tamaa kwani anaweza kufikiri, kushawishi na hata kufanya lolote.

Watanzania wasikate tamaa kiasi hicho ambacho umefikia kwani ni hatari kwetu sote,

Kugoma kuona ukweli ili kujiaminisha kuwa hajakata tamaa ni kosa kubwa. Infact ni kukata tamaa kusikopimika.

Kuona kosa na udhaifu sio kosa wala sio kukata tamaa! Kujipofua dhidi ya makosa na madhaifu muhimu ya kibnafsi kifamilia au Kitaifa ni zaidi ya kukata tamaa!

Kuwa Hard and bold to see and oberve what should be seen and honestly be observed bila kujali hata consquencies ... Ni ukomavu. Hapo kuna uwezekano wa kupiga hatua ya kwenda mbele! Kwani hata Dr akitokea anayeweza kuutibu ugonjwa ..unaweza kujitokeza na kusonga mbele kumfuata kwa msaada kwani Unajitambua fika, tena wewe mwnyewe bila hata kusukumwa....huko sio kukata tamaa!! Ni kuwa na charecter! Kujiheshimu.

Ni muda muafaka kwa WaTz kutambua ukweli halisi unaotuzunguka...na hili lifanyike kikamilifu tena bila hata ya kupepesa macho!!
 
Back
Top Bottom