Let's face it: Bongo Flava ni rubbish

Game Theory

Platinum Member
Sep 5, 2006
8,545
835
I know its gonna be unpopular opinion lakini potelea mbali. I have tried kusikiliza bongo flava lakini i can confess kuwa nimegive up!

Kama ingekuwa 1980's NINGEKUBALI kuwa hatuna vifaa wala exposure

Mara mia nisikilize KWAITO au hata ORIGINAL TAARAB na siyo MODERN TAARABA kuliko kusikiliza this rubbish so called BONGO FLAVA

Production zao ni poor hii nazungumzia akina DULLY SKYKES mpaka NAKAAYA SUMARI

Wasanii ni kila mtu in short wengi wao ni rubbish

Music video zao zinafanya barbeque video zangu zionekane zimetengenezwa na SPIKE LEE

Sasa hebu niambie how can i love this genre ya BONGO FLAVA?

Sikatai ni nzuri for local market lakini kwa sababu watu hawana much choice lakini kama ni venture capitalist i cannot thubutu kuinvest hata centi tano yangu kwenye hii takataka

BTW
the same applies to:

ZE COMEDY (ambao wanajaribu kuwaiga wale wakenya wanaoiga akina Moi)

MADIZAINA wakibongo (Akina Khadija Mwanamboka na wale wadosi ambao wanafanya shows kila kukicha)

The day hawa wapuuzi watakapo achana kuiga akian RODNEY JENKINS, DALLAS AUTIN, DR DRE, na na wengineo nitawaunga mkono in the mean time nitawasikiliza WANAJENJE for their originality, DARA J from WEST AFRICA for their originality na KWAITO from south Africa for their Originality

end of rant sasa nakaribisha watetezi wa huu upuuzi
 
end of rant sasa nakaribisha watetezi wa huu upuuzi

BM you may have a point katika hizi rants zako and I thought this would have been a very good discussion lakini kwa hiyo conclusion hapo juu naona kama hii thread 'umeifunga'. There is no argument you are forcing people to accept what you are saying hapa na it indicates kwamba asiyekubaliana na usemayo ni 'mpuuzi'.Atakayetetea 'upuuzi' ataonekana kwako ni mpuuzi. Its an utter disrespect of others thoughts and opinions. I have my opinions on this but I'll withhold them hadi utakapo edit hiyo statement hapo juu.
 
DOWN.....DOWN....BONGO FLAVA....!

Hapa sasa you are talking.... this has made TZ as one of our naigbouring country.What people talk,do,walk,travel,think,etc BONGO FLAVA...!

TALK TO 10 YOUNG MEN & KIDS OF WHAT THEY WANT TO BE OR WHAT THEY ARE GOING TO DO IN FUTURE....! OBVIOUS 60%(unresearched but proved)yaan^ WILL TELL YOU THE WANT TO BE RUBBISH.......!

INGIA MADARASANI, STUDENTS ARE BUSY WITH (not home works or something) RUBBISH 'MISTARI'...NATAKA KUTOA SINGO! WHAT FUTURE ARE WE CREATING NOW!!!!! THE COUNTRY OF WACHAPAKAZI OR THE COUNTRY OF WABURUDISHAJI....? (samahani sina maana ya VIBURUDISHO anavyozungumzia MKANDAMIZAJI)

SIKU HIZO NILIWAHI SOMA KITABU KIMOJA KIKIMZUNGUMZIA MHUSIKA ALIYEITWA
OKONKWO,HUYU ALIKUWA NA BABA YAKE AMBAYE KUANZIA MSIMU WA KUANDAA SHAMBA,KULIMA,KUPANDA,KUPALIA,KUVUNA NA HATA KU-STORE! THE ONLY THING BABA YAKE ALIWEZA KUFANYA NI KUWABURUDISHA WATU KWA FILIMBI NA MUZIKI MTAMU( actually was a great singer)bBUT AT THE END HE ENDED UP BEGGING AND GIVEN SOME GULPS( sina maana ya mwanamuziki anayepita baa akiimba na kuomba anunuliwe bia simply ni maarufu)OKONKWO ALIUMIA SANA KUWA NA BABA OF SUCH TYPE! LAKINI BADO NI BABA YAKE!
MY POINT IS: TUSIJENGE (FUTURE) JAMII YA WANAMUZIKI PEKEE!!!!! TUJENGE NA KUANDAA JAMII YA WAPENDA KAZIII!!!!!!(misunderstoo
d....?)
 
Unajua katika hii industry ya bongo Flava hakuna hata mmoja aliye na uhakika na anachokifanya. Kuanzia wale wanaoandika hizo lyrics, maproducer na waimbaji. wote wako hapa kutengeneza pesa ya haraka huku wakionyesha upuuzi wao.

Kwa mfano Bongo star search what a waste of time. kwa nini hizo fedha zisitumike kuwapa hao vijana elimu ya muziki au elimu nyingine yeyote ile something that will last na waweze kuwa nacho for the rest of thier lives
 
As young as i mayb i would have to say i kinda agree with the views and opinions expressed above..I used to have a friend who was busy na 'mistari' 'kutoa singo' lol..now he in the street smoking weed on the daily basis (wazazi wamemchoka but pia wazazi are to blame by not showing an example of what can be achieved through education (wasanii wengi wa bongo flava wanatoka familia maskini kwaiyo wanataka kutajirika haraka haraka)..i really dont knw where bongo flava is going.first they dont make real money off the album, concert money doesnt last, royalties and copyrights are an issue around the world, the only way we can see any delevelopment through music is if our government took a hard stance in support of it..BUT WAIT!! This is the same government (BOT.RICHMOND ETC) kuzuia ukimwi ,malaria kumewashinda etc...I think their hands are full...kutafika kweli!!
 
Kwa mtu anayejua historia ya muziki wa Tanzania, na haswa miziki iliyowahi kuvuma kama Orchestra,Rumba, Taarabu na mingine mingi utaweza kuelewa ni kwa kiasi gani miziki hii ya zamani ilivyoweza saidia kutoa taswira mpya kwenye muziki huu wa sasa Bongo flava. Kwa ninavyoelewa mimi Bongo flava ni kama copy ya RNB na HIPHOP combined, muziki kama chombo kina madhumuni yake na kwa watanzania Bongo Flava ni muziki ambao umejitahidi kwa kiasi kikubwa sana kufikia malengo au madhumini ya muziki, na inawezekana kabisa ukawa ndio muziki ulifanikiwa zaidi kuliko miziki yote Tanzania tukiondoa muziki wa Orchestra ambao kwa sasa sijui mwelekeo wake upo wapi. Pamoja na mafanikio yake yote hayo Muziki wa Bongo Flava pia una mapungufua yake ambayo watu kama wewe(ninyi) mumeweza kuyaona na pengine kusaidia kutia nguvu mpya ili kuufikisha kileleni au mahali ambapo tutaweza kujivunia nao, hata nje ya mipaka ya Tanzania na africa kwa ujumla.

Hip Hop ni muziki ulifanikiwa sana duniani, lakini pamoja na uzuri na mafanikio yake, nadhani ni mziki wenye kulalamikiwa zaidi kuliko miziki yote duniani sembuse Bongo flava?

Nivi matatizo vichache tu ambavyo ni "production" in terms of audio,Video,stage performance,stage apperance and decoration na mengineyo mengi yamekuwa na mapungufu sana lakini kwa upande wangu naona ni matokeo ya upungufu au ufinyu wa kipato cha wasanii na uchache wa kujitolea kwa washika dau wa sector na labda hati miliki ingewezesha hali kuwa njema. Ukiangalia kenya wana production zilizo nzuri kuzidi Tanzania lakini nadhani ni tools wanazotumia na pia wanchukulia muziki kama kazi (full time job) na si kama wafanyavyo wengi wa wasanii wetu. Msanii wa Tanzania anaishi Bar na akipata vidakika vichache katika siku ndio anaandika vi mistari viwili basi siku imekwisha, hana muda wa hata kutafuta shule ya muziki au shule ya chombo chochote cha muziki au any related course kama "records mastering,records marketing and distribution" na nyingine nyingi ili kila siku azidi kukua kimuziki. Na watu tukiambiwa ni full time job wanafikiri maana yake ni kuishi kwa kutegemea muziki tu, kwa hiyo hata akitumia visaa vyake vitatu kwa siku powa. La hasha, kama mwenzako ni mwajiriwa na nafanya kazi jtatu mpaka ijumaa, masaa nane kwa siku (masaa 40 kwa wiki) basi na wewe mwanamuziki unatakiwa ufanye hivyo hiyvo ili upate muda wa kutosha kujifunza mambo mengi yanayohusiana na muziki, uweze kufanya kazi nzuri kwa kuwa na muda wa kutosha kurekebisha makosa katika kazi zako ili kupata matunda mazuri na mwisho kupunguza matusi toka kwa watu kuwa muziki wa Bongo Flava ni Rubbish.

Na matatizo haya ndio yanawakumba wasanii wengine kama wa maigizo n.k.

Naomba nisijisafishe, mimi sii msanii ila ni mpenzi wa muziki na sanaa nyingine, na swala la RUBBISH au ubora wa sanaa zetu ni jukumu letu sote wapenzi na wasanii kuhakikisha kuwa sanaa nchini unakuwa ili tuweze kupata vitu vyenye ubora mkubwa. Na je? wewe kama mtanzania umefanya nini kusaidia usanii nchini au kuleta mabadfiliko katika sanaa yetu nchini?

Asante.
 
Ukitaka kulalamikia genre kama genre usichukue mifano yake mibovu kabisa, chukua mifano yake mizuri kabisa ili ukimuua Elvis uwe hubakizi kitu katika Rock and Roll, au ukimuua Bob unakuwa hujabakisha kitu katika reggae.

Umeshawahi kusikiliza metaphors na similes za "Professor J"? Umeshawahi kusikiliza satire, sarcasm na wit za Wagosi? Umeshawahi kusikiliza delivery ya Saigon? Umeshawahi kusikiliza the almost cacophonic artful composition of that word smith and lyrics weaver known as Halfani? Umeshamsikiliza Solo Thang akikwambia "kuna marepa na marapper", ulimuelewa? Wewe unasikiliza "marepa" au "marapper"?

Nakubali kuna utumbo mwingi sana kwenye bongo flava (as in hip hop in general by the way) lakini huwezi kui-judge genre nzima kwa Dully Sykes ambaye yeye mwenyewe kashakwambia ni "mzee wa misifa" na siyo authentic hip hopper.Unasikiliza production za "Soundcrafters" unategemea vipi kusikia authentic Tanzanian hip hop.Sikiliza mitwango ya Mika Mwamba na Majani iliyoenda na watu wanaoeleweka kwenye mic, utaelewa kwa nini watu wanashabikia bongoflava.Tatizo ni kuwa kwa kila msanii mmoja wa kweli kuna wengine tisa wana jump on the bandwagon bila talent wala drive, wanatafuta fame na money.

Hayo matatizo unayoyaona kwenye bongoflava yapo mpaka kwenye hip hop na ukiikomalia bongoflava unaweza kuwa self hater au unasikiliza the wrong kind of bongoflava.
 
Ukitaka kulalamikia genre kama genre usichukue mifano yake mibovu kabisa, chukua mifano yake mizuri kabisa ili ukimuua Elvis uwe hubakizi kitu katika Rock and Roll, au ukimuua Bob unakuwa hujabakisha kitu katika reggae.

Umeshawahi kusikiliza metaphors na similes za "Professor J"? Umeshawahi kusikiliza satire, sarcasm na wit za Wagosi? Umeshawahi kusikiliza delivery ya Saigon? Umeshawahi kusikiliza the almost cacophonic artful composition of that word smith and lyrics weaver known as Halfani? Umeshamsikiliza Solo Thang akikwambia "kuna marepa na marapper", ulimuelewa? Wewe unasikiliza "marepa" au "marapper"?

Nakubali kuna utumbo mwingi sana kwenye bongo flava (as in hip hop in general by the way) lakini huwezi kui-judge genre nzima kwa Dully Sykes ambaye yeye mwenyewe kashakwambia ni "mzee wa misifa" na siyo authentic hip hopper.Unasikiliza production za "Soundcrafters" unategemea vipi kusikia authentic Tanzanian hip hop.Sikiliza mitwango ya Mika Mwamba na Majani iliyoenda na watu wanaoeleweka kwenye mic, utaelewa kwa nini watu wanashabikia bongoflava.Tatizo ni kuwa kwa kila msanii mmoja wa kweli kuna wengine tisa wana jump on the bandwagon bila talent wala drive, wanatafuta fame na money.

Hayo matatizo unayoyaona kwenye bongoflava yapo mpaka kwenye hip hop na ukiikomalia bongoflava unaweza kuwa self hater au unasikiliza the wrong kind of bongoflava.


Umeongea yote kijana!
Yaani uchambuzi umetulia. Huwezi kuchukua nyimbo za Dully Sykes ama Inspekta Haroun na kuzifanyia uchambuzi, kisha ukatoka na masimamo kwamba bongo flava yote ni nonsense! Hawa wananii tajwa wamejisemea wao wenyewe katika mashairi yao kwamba wanaimba "Mwanasesere" na "rap katuni", hivyo wasitiliwe maanani sana. Ndio sababu Solo Thang akawaambia kwamba "Katuni Tunakataza", katika ule wimbo wa kundi lao la Wateule, kwa sababu kila mtu atadhani wasanii wote wanaimba katuni. Utakuwa hutendi haki kabisa ukiwaweka wanamuziki wote wa bongo flava katika kapu moja.
Katika kundi la "Marepa" tuwaondoe Wagosi wa Kaya, Solo Thang, Afande Sele, Jay, Fid Q, Mike Tee, na pengine bwana mdogo K Sal.
 

Umeongea yote kijana!
Yaani uchambuzi umetulia. Huwezi kuchukua nyimbo za Dully Sykes ama Inspekta Haroun na kuzifanyia uchambuzi, kisha ukatoka na masimamo kwamba bongo flava yote ni nonsense! Hawa wananii tajwa wamejisemea wao wenyewe katika mashairi yao kwamba wanaimba "Mwanasesere" na "rap katuni", hivyo wasitiliwe maanani sana. Ndio sababu Solo Thang akawaambia kwamba "Katuni Tunakataza", katika ule wimbo wa kundi lao la Wateule, kwa sababu kila mtu atadhani wasanii wote wanaimba katuni. Utakuwa hutendi haki kabisa ukiwaweka wanamuziki wote wa bongo flava katika kapu moja.
Katika kundi la "Marepa" tuwaondoe Wagosi wa Kaya, Solo Thang, Afande Sele, Jay, Fid Q, Mike Tee, na pengine bwana mdogo K Sal.


AMINIA BABAKE!!!
 
Afande Sele Ft Solo Thang & Profesa Jay


Verse I - Solo Thang

Yoooh! yoooh!

Hakuna S bila O, L bila O
Mwingine aitwe Thang bila Solo
Shupavu awajibike kama apolo
Jay, Afande ni ukuta wa-vichocholo
Yoooh! Nadhani ni mtazamo wa fani
Ile dhana uhuni wameleta hawa katuni
Kuna kurap na kubwata marepa na marapa
Katuni tungo tata wapi ulipo wee kaka
Unakuwa mtumwa ili upewe promo kuuza
Au kama binti ukalale kwa produza
Mapromota wanauma tu hawajui na kupuliza
Na siku wakipuliza ujue kidonda kishaoza
Natamani kuwa huru mnyonyaji asinidhuru
Wanaitwa Ma'mc hawajui mtindo huru
Huu mtazamo wangu naona vingi vioja
Yaani watangazaji sasa ndio mameneja
Vidato sita nilivyopitia
Ndivyo vinavyonisadia
Mbunifu ukizingatia hata wakinibania
Ni kipaji tu ni mtazamo tu
Msikasirike washkaji haya mawazo tu
*****Ulamaa....

Kiitikio
Ni mtazamo zamo mc usiogope kivuli
Bora ukemee mabaya na usifie mazuri
Ni mtazamo zamo mc usikwepe umande
Okoa sanaa ya bongo ili uchumi upande
Ni mtazamo zamo mc usiogope kivuli
Bora ukemee mabaya na usifie mazuri
Ni mtazamo zamo mc usikwepe umande
(mouth scratch) Ulamaa, Profesa Jay, Afande

Verse II-Profesa Jay
Ni mtazamo rap inakuwa ni mkingamo
Sasa watoto wadogo wanajiita watu wa makamo
Wanakwenda hatua mbili wanarudi kumi na kujipongeza
Bila kuzingatia hatua nane walizopoteza
Hao ni mafukara wa akili zao na uwezo wao
Wasiotambua lini na nini ni hatma zao
Magwiji vichwa chini nadhani wanatunga sheria
Lakini sheria msumeno isije ikawarudia
Yes maandagraund wanafanya rap inang'ara
Lazima muwe vinara imara kwenye msafara
Rap na mazingaombwe abadan haviendani
Msitegemee 'tawiree' iwaokoe katika fani
Ni vema ukafiri kabla ya kufanya maamuzi
Tazama mbele usije ukanywa chao kwa mluzi
Naamini askari shupavu lazima apitie depo
Vinginevyo ndugu yangu utakuwa unapaka rangi upepo
Kama unapata moja kwa nini usipate na mia
Hii inawezekana kwa wote mlio na nia
Sioni sababu za msingi kuomba kwenye mitaa
Kama una kipaji kwa nini ufe na njaa

Rudia kiitikio

Verse III - Afande Sele
Asante Profesa Jay, Majani na Ulamaa mmegusa ninapopataka
Nami kwenye mtazamo nina jambo nataka kuweka
Maana kila kukicha mc's wanaongezeka
Nasema very nice, yes rap kama dhehebu mc's kama wafuasi
Wingi wa wasanii inaonyesha ni dini swafi yaani imekubalika
Waumini tupo wengi lakini bado nina shaka sijapata uhakika
Wote tumesadiki au wengine feki
Mmetumwa kama mamluki manake hamna maana mna rap mradi Rapstairi imekosa vina yenye vina haina maana
Kila mnapokaa mnapenda kusengenyana
Mnapenda kutetana na mnapenda kulumbana
Mi naogopa sana kwa jinsi ninavyoelewa mwishoni mnatukanana
Ama inawezekana mwishoni mtachinjana
Na wote tunaorap tuonekane hatuna maana
Wapi ilipo taarab ilikuja kwa kishindo
Hata wagumu walishahusudu kwa ajili ya malumbano
Mwishoni ikafa kibudu shabiki piga simu
Changia mawazo yako ni nani tutamlaumu
Kama rap itasizi kwa kuendekeza upuuzi
Nani tumchune ngozi produza anayerekodi
Ama labda DJ anayepiga kwenye kipindi
Wengi wanapenda rap ajabu rap haiwapendi
Waungwana wanaicha pumbavu hawaambiliki
Hivi kwani lazima wote tuwe wanamuziki
Mi nadhani ingetosha wengine mbaki ushabiki
Huu ni wangu mtazamo masela msijenge chuki
Hata na majani yooh!

Mheshimiwa Brazameni,
Huu wimbo ume 'summarize' mengi ambayo umeyaongea.
Hebu upitie kwa makini na utoe hoja zako ili uone mtazamo wa wanamuziki hao na utoe utatuzi wa kadhia hiyo uliyoiainisha na kuilalamikia hapo juu!
Tuendelee kuelimishana.
Mheshimiwa Idimi
 

I know its gonna be unpopular opinion lakini potelea mbali...
... sasa nakaribisha watetezi wa huu upuuzi...

Mkuu inaelekea Umeanzisha Vita,na umetupa mabomu yako ktk kila kona ya usanii, nnaelekea kufikiri Umejiandaa kwelikweli!!

Kuhusu ' Miondoko ya Bongo Flava', binafsi sina utaalamu wa mambo ya kimuziki,ila kama mpenzi wa MUZIKI kwa ujumla utagundua kuna kasoro fulaniX2,Achilia mbali videos ambazo nyingi huwa ni 'FAKE' but 'there is always something missing' hii iwe ni kwa Waimbaji,Watunzi na Kuu zaidi Maprodusa wa Tz .(Nahisi Brazameni unafurahia MIDUNDO zaidi ya LYRICS haswa inapokuja kwenye Kwaito Music)

Ukizingatia Ubora/Umahiri wa Maprodusa wa Tz hii leo,hali za kifedha/tungo za Wasanii hata wanapofikia kuingia Studio, kwa ujumla siwezi kulalamika sana kwani Safari Ni Hatua.
Nikikumbuka enzi za 'Kwanza Unit'(X-Tambaza boyz) na Hii Leo Kundi la 'Wanaume Family'(Dar-mpaka- Moro)kuna mabadiliko kidogo,and i suppose there is room for more change.
 
BM you may have a point katika hizi rants zako and I thought this would have been a very good discussion lakini kwa hiyo conclusion hapo juu naona kama hii thread 'umeifunga'. There is no argument you are forcing people to accept what you are saying hapa na it indicates kwamba asiyekubaliana na usemayo ni 'mpuuzi'.Atakayetetea 'upuuzi' ataonekana kwako ni mpuuzi. Its an utter disrespect of others thoughts and opinions. I have my opinions on this but I'll withhold them hadi utakapo edit hiyo statement hapo juu.

Fact! i dont listen or watch any of them stuffs! they suck and bongo movies too! i would never sell my script to any director here!
 
really rubbish!!!!!!!!!!!!!! until they change!!!!!
advice:
LET THEM LEARN THE ART OF MUSIC(if possible in sanaa colleges like bagamoyo)
AND HOW TO TAKE BREATHES OF DIFFERENT AUDIENCES........! not only the 'pullers',MESSAGES SHOULD NOT ONLY BE "LOVE" nk
THIS WILL REALLY MAKE IT BONGO FLAVA(watoto,vijana,wasomi,waswaliina,wazee,wafanyabiashara,wanywaji nk)
 
Kabla ya kuwa diss ma artist wetu... tujiulize how much tumewapa support ya kiukweli hata wale wachahe TUNAO WAKUKUBALI?, fo coz their are some fellas who normally sing nonsese [kwa maoni yako] lakini ivi kama unakumbuka form three ulijifinza nini kuhusu dhamira kuu ya fasihi [simulizi na andishi?],kama umeshau basi come again kwa kuumuliza mdogo wako and then utajua kama bongo flava ni rubbish au uliyoyasema ni rubbish. Twende mbele na lurubi nyuma tatizo letu wabongo ni kwamba HATUWAPI SUPPORT ya ukweli wasanii wetu [ mention kivyovyote vile],wengi tunapenda njia za MKATO tu na kuishia kuwa diss eti ALIKUWA JUU SANA HUYU ONA SASA HANA HATA BAISKELI!, at the very time chumbani kwako una album ya nyimbo yake ya KU BURN kwa mshkaj!

Pengine tofauti na Uganda ambako huku wenzetu wananchi wanatoa support ya ukweli kwa wasanii wao,nasema coz nimejionea mwenyewe,msanii kama bebe cool anatoa hadi sponsorship kwa wanafunzi achilia mbali maisha anayoishi yalivyo juu, hii inaonesha ni jinsi gani Mziki unavyo LIPA huku inhali huko mziki haulipi. Tuwape support wasanii wetu jamani!!
 
Hata Hip-Hop Ilipoanza ilikutana na vikwazo vingi sana na muziki huu ulisemekena haukuwa bora lakini miaka ilivyoenda ndio mambo yakabadilika na muziki ukazidi kuboreshwa. Bongo Flava ni Muziki unaokuwa kila siku, tena kwa hivi sasa si Bongo tu bali ndio Muziki maarufu sana hata kwa nchi jirani kama Kenya, Rwanda, Burundi, Uganda na hata baadhi ya sehemu za DRC Congo. Kila kitu kina mapungufu yake na hakuna ubaya kwenye kuchota utaalamu kutoka nchi nyingine.

Vijana wengi sana Tanzania wamejijenga na kujiajiri kimaisha kutokana na mafanikio ya muziki huu, nadhani kila mtu ana uhuru wa kusikiliza chochote anachopenda kama unaona Bongo Flava haikufai basi sikiliza aina nyingine ya muziki. Utakuta mtu anapiga madongo Bongo Flava lakini unakuta ndio huyo huyo anakuwa wa kwanza kusikiliza nyimbo kama Chicken Noodle Soup au Soulja Boy.
 
Utakuta mtu anapiga madongo Bongo Flava lakini unakuta ndio huyo huyo anakuwa wa kwanza kusikiliza nyimbo kama Chicken Noodle Soup au Soulja Boy.

bado natafuta nguvu na hii thread. ila ngoja nikawasilikize chemba squad kwanza na BWII...au sijui nisikilize Afroman - I got high......shhhhh Kimya Kimyaa.
 
Kwenye Bongo fleva inabidi tupate unique sound yetu kama kwaito vile lakini haya mambo ya kucopy midundo ya watu na kuigeuza geuza haitusaidii....
 
I know its gonna be unpopular opinion lakini potelea mbali. I have tried kusikiliza bongo flava lakini i can confess kuwa nimegive up!

Kama ingekuwa 1980's NINGEKUBALI kuwa hatuna vifaa wala exposure

Mara mia nisikilize KWAITO au hata ORIGINAL TAARAB na siyo MODERN TAARABA kuliko kusikiliza this rubbish so called BONGO FLAVA

Production zao ni poor hii nazungumzia akina DULLY SKYKES mpaka NAKAAYA SUMARI

Wasanii ni kila mtu in short wengi wao ni rubbish

Music video zao zinafanya barbeque video zangu zionekane zimetengenezwa na SPIKE LEE

Sasa hebu niambie how can i love this genre ya BONGO FLAVA?

Sikatai ni nzuri for local market lakini kwa sababu watu hawana much choice lakini kama ni venture capitalist i cannot thubutu kuinvest hata centi tano yangu kwenye hii takataka

BTW
the same applies to:

ZE COMEDY (ambao wanajaribu kuwaiga wale wakenya wanaoiga akina Moi)

MADIZAINA wakibongo (Akina Khadija Mwanamboka na wale wadosi ambao wanafanya shows kila kukicha)

The day hawa wapuuzi watakapo achana kuiga akian RODNEY JENKINS, DALLAS AUTIN, DR DRE, na na wengineo nitawaunga mkono in the mean time nitawasikiliza WANAJENJE for their originality, DARA J from WEST AFRICA for their originality na KWAITO from south Africa for their Originality

end of rant sasa nakaribisha watetezi wa huu upuuzi

Umesema ukweli mwingi lakini.Ila kuna wasanii utakuwa hujawafanyia haki. Msanii niliye nunua album yake nikasema this is as much as worth as I paid for say D'Angelo was Saida Karoli's first album. Ingawa kilugha sielewi, ni sawa sawa usikie Kwaito, upende lakini usielewe lugha. Whether Saida Karoli is bongoflava or not, lakini kaja kipindi hiki cha bongoflava.

Kuhusu beats nakubaliana na wewe. Geeque, nadhani bongoflava has had more than 10 years to perfect beats, ila wapo wengi wanaochemsha.

Brazameni, tukija lyrically na flow hapo nadhani ndo umewatukana kabisa. Prof Jay, Fid Q, Ngwair etc, lyrically wanafurahisha na kuchemsha akili kama NAS au Biggie. Kwa mafunzo na vichekesho, Wagosi wa Kaya. Mr Ebbo akijipanga vizuri ana uwezo wa kutoka international market. Nadhani kufanikiwa kimataifa kama unavyotaka wewe ni jinsi gani msanii anaji-package. Msanii awe tayari ku-target soko lake (lakini aonekane authentic), lakini wengine awatose ambao hawamfaidishi.

Nadhani swali kubwa ni je kuna soko la muziki huu? Nadhani jibu ni Yes and No. Soko lipo kwa wachache waki-target vizuri, ila wengine hamna. Wewe umeongelea international nadhani, na mimi najibu kwa angle ya international.

TID msanii mzuri sana. Kuna nyimbo yake moja ipo kwenye mix ya Putumayor Putumayo. TID anaimba bongoflava, lakini jamaa vocals anazo hands down. Beats zake nyingi ni nzuri. Zeze ilikuwa mix nzuri ya traditional feel na modern feel. Kuna wimbo mwingine naupenda sana personally wa TID, unaitwa 'Nipe Nafasi'. Mkuu hii beat ni kama old skool za kina Johny Gill, angeimba mmarekani mweusi kwa maneno ya kizungu ungekubali. Brazameni, get nice heavy speakers and blast that tune usikie inavyokita na flow ya FID Q, that song is on point man (usisikilize kwenye speaker zinazoyumba kama zimeshikiliwa na waya).

Ndio, wanavyoiga beats, it doesnt sound authentic african. I see where you are coming from, and that is a challenge to them. The market is there to be created, the issue is how you go about it.

Oh yeah. The fact wametengeneza soko nyumbani bila kufisadi, na wamejiajiri ni kitu cha kufurahia na kuheshimu.
 
Back
Top Bottom