Leticia Nyerere: WaTanzania wengi wamepoteza uzalendo kwa taifa lao!

Huyu mama ni mbunge wa chama changu, ila ni kati ya wabunge mzigo ndani ya chama. Uwa hana hoja zenye mashiko. Ni msharuko sana. Si ndio huyu alisema wanaume wasioweza kutongoza mpaka wanabaka waanzishiwe vyuo vya kutongoza. Sasa haya ni maneno ya kutoka kwa mbunge wa CHADEMA kweli?
binafsi nakuunga mkono mkuu, ni miongoni mwa wabunge mizigo.
 
We chizi kweli sasa kama baba wa taifa ka marekani anadhihakiwa ndo iwe pia kwa tanzania??
Sikia dada, nenda kwa kapuya ukachukue ada

Nyerere mwenyewe alikuwa mpenda dhihaka kwanini asidhihakiwe? alikufa na hati miliki ya dhihaka?

Hapa Mwalim anafundihsha ubao mtupu, hauna kitu:

 
Jamani, huyu mama anaejiita Leticia Nyerere, ni bado mke wa mtoto wa Nyerere?

Uongo anaousema ni huu, kuwa na kukaa kwake Merekani hajawahi kuona "Baba wa Taifa la Merekani George Washington" akidhihakiwa;

Dah! huo ni uongo wa wazi wazi, machache haya hapa ya kudhihakiwa George Washington:







Leticia, kuna tons and tons za dhihaka kwa George Washington. Unalidanganya bunge na Watanzania kwa ujumla kwani tunakuona live, kwa kuwa eti umekaa USA.

Wewe inaonesha ulikuwa unakaa USA lakini huijui USA au unaona Watanzania tu wajinga kiasi cha kutudangaya kijinga namna hiyo?

Inaonesha u mfinyu sana wa mawazo.

Wakwanza wewe unalidhihaki jina la Nyerere kwani umeshaachika na bado unalitumia kama una hati miliki nalo.

jambo hili hata kama angelisema mbunge wa CCM bado ningeliunga mkono,,,,kweli wengi wetu si wazalendo,,,nasikia raha nikimuona mbunge wa CHADEMA akihimiza uzalendo,,hii inaonesha umakini wa CHADEMA,,,ccm wajifunze kwetu.
 
Nionavyo mimi serikali na viongoz ndio wamekosa uzalendo kwa kule kusahau misingi iliyowekwa na waasisi wataifa hili kwa kujiusisha na mikataba isiyokuwa na maslahi ya wananchi bali kujinufaisha wenyewe na familia zao.
 
Anachosema mama huyu ni kweli ila mifano anayotumia ndiyo mibovu. Ukweli wa watanzania kukosa uzalendo leo ni wazi kabisa, na hilo siyo kosa lao bali ni matokeo ya umaskini. Ile collective ownership iliyokuwapo nyakati zile ilikuwa inamfanya kila mtu aone mali ya umma kama yake pia na kujiona sehemu ya jumuia na taifa lote. Lakini baada ya ubinafsi kuingia, kila mtu anataka kuwa na cha kwake na hapo kipaumbele kinakuwa ni ubinafsi na mali binafsi kuliko taifa na mali ya umma, na hapo ndipo uzalendo unapoanza kuyeyuka. Kwa bahati mbaya hiyo ni hulka ya bianadamu wote; njia pekee ni kufyeak umaskini ndipo watu wataanza kufikiria utaifa.
 
Jamani, huyu mama anaejiita Leticia Nyerere, ni bado mke wa mtoto wa Nyerere?

Uongo anaousema ni huu, kuwa na kukaa kwake Merekani hajawahi kuona "Baba wa Taifa la Merekani George Washington" akidhihakiwa;

Dah! huo ni uongo wa wazi wazi, machache haya hapa ya kudhihakiwa George Washington:







Leticia, kuna tons and tons za dhihaka kwa George Washington. Unalidanganya bunge na Watanzania kwa ujumla kwani tunakuona live, kwa kuwa eti umekaa USA.

Wewe inaonesha ulikuwa unakaa USA lakini huijui USA au unaona Watanzania tu wajinga kiasi cha kutudangaya kijinga namna hiyo?

Inaonesha u mfinyu sana wa mawazo.

Wakwanza wewe unalidhihaki jina la Nyerere kwani umeshaachika na bado unalitumia kama una hati miliki nalo.
Huyu anakuwa nani yake Yericko?
 
jambo hili hata kama angelisema mbunge wa CCM bado ningeliunga mkono,,,,kweli wengi wetu si wazalendo,,,nasikia raha nikimuona mbunge wa CHADEMA akihimiza uzalendo,,hii inaonesha umakini wa CHADEMA,,,ccm wajifunze kwetu.

Uzalendo wa mtu si kwa kutukuza kila baya. Uzalendo wa mtu si kwa kutukuza jina la fulani.

Uzalendo wa mtu ni kukosoa pale wajina lolote anapopotoka.

Nyerere ananukuliwa humuhumu JF akisema kuwa Wachagga, Wahaya na Wanyakyusa hawafai kuwa Rais. Jee, tukubali tu hilo kwa kuwa kasema Nyerere? tusikosowe?

Ni vibaya kumtukana, kumkosea heshima au kumsingizia kitu. Lakini kumdhihaki na kuonesha makosa yake, huo ndio uzalendo haswa unaotakiwa.

Labda ni punguani wa uzalendo ambae atasifu kila kitu cha Nyerere wakati Nyerere mwenyewe kisha sema yeye si malaika na ana makosa yake, tusiyafate.

Nyerere kafanya makosa mengi tu katika miaka 24 aliyotutawala Watanzania. Hilo tukipenda tusipende ndiyo ukweli na hapo hakuna dhihaka ni ukweli mtupu.

Aje mtu hapa aseme kuwa kila aliyoyafanya Nyerere hakuna aliyokosea.

Na kwanini asifanyiwe dhihaka wakati yeye alikuwa akidhihaki watu?
 
Uzalendo wa mtu si kwa kutukuza kila baya. Uzalendo wa mtu si kwa kutukuza jina la fulani.

Uzalendo wa mtu ni kukosoa pale wajina lolote anapopotoka.

Nyerere ananukuliwa humuhumu JF akisema kuwa Wachagga, Wahaya na Wanyakyusa hawafai kuwa Rais. Jee, tukubali tu hilo kwa kuwa kasema Nyerere? tusikosowe?

Ni vibaya kumtukana, kumkosea heshima au kumsingizia kitu. Lakini kumdhihaki na kuonesha makosa yake, huo ndio uzalendo haswa unaotakiwa.

Labda ni punguani wa uzalendo ambae atasifu kila kitu cha Nyerere wakati Nyerere mwenyewe kisha sema yeye si malaika na ana makosa yake, tusiyafate.

Nyerere kafanya makosa mengi tu katika miaka 24 aliyotutawala Watanzania. Hilo tukipenda tusipende ndiyo ukweli na hapo hakuna dhihaka ni ukweli mtupu.

Aje mtu hapa aseme kuwa kila aliyoyafanya Nyerere hakuna aliyokosea.

Na kwanini asifanyiwe dhihaka wakati yeye alikuwa akidhihaki watu?

Nyerere hajawahi hata siku moja kusema kuwa Kabila moja au jengine halifai kuwa rais. Hizi ndiyo kejeli zenu tunazozungumzia hapa kufikia hatua ya kumtwisha maneno ambayo hajawahi kuyasema. I challenge you Faiza to give us the context, quote, when, and where he uttered such words. Otherwise you owe us, JF, an appology for propagating such lies
 
Uzalendo wa mtu si kwa kutukuza kila baya. Uzalendo wa mtu si kwa kutukuza jina la fulani.

Uzalendo wa mtu ni kukosoa pale wajina lolote anapopotoka.

Nyerere ananukuliwa humuhumu JF akisema kuwa Wachagga, Wahaya na Wanyakyusa hawafai kuwa Rais. Jee, tukubali tu hilo kwa kuwa kasema Nyerere? tusikosowe?

Ni vibaya kumtukana, kumkosea heshima au kumsingizia kitu. Lakini kumdhihaki na kuonesha makosa yake, huo ndio uzalendo haswa unaotakiwa.

Labda ni punguani wa uzalendo ambae atasifu kila kitu cha Nyerere wakati Nyerere mwenyewe kisha sema yeye si malaika na ana makosa yake, tusiyafate.

Nyerere kafanya makosa mengi tu katika miaka 24 aliyotutawala Watanzania. Hilo tukipenda tusipende ndiyo ukweli na hapo hakuna dhihaka ni ukweli mtupu.

Aje mtu hapa aseme kuwa kila aliyoyafanya Nyerere hakuna aliyokosea.

Na kwanini asifanyiwe dhihaka wakati yeye alikuwa akidhihaki watu?

kuna vitu viwili unavichanganya, naam, viko vitatu vinakutatiza ndugu yangu.


1/ Kukosoa ni ruhusa, na ikizingatiwa hakuna aliyekamilika. Bahati nzuri hata Nyerere alikufa huku akijua vizuri kuwa kukosolewa ni ada na wajibu.


2/Dhihaka ni dharau na ni moja kati ya tabia za utovu wa wa nidhamu.


3/ Unapokosoa bila kuzingatia muktadha, istilahi, mila, ada, na desturi ya jamii huko huwa si kukosoa bali dhihaka na kwa hivyo huwa dharau na utovu wa nidhamu.


Mfano Kikwete akiwa anatekeleza majukumu yake kama mwenyekiti wa CCM, alafu Pius Msekwa akamkosoa hadharani ikiwa huyo Msekwa ni mjumbe wa vikao ambavyo Kikwete ni mwenyekiti wa hivyo vikao basi Msekwa atakuwa hajamkosoa Kikwete bali amemdharau na kumdhihaki.


Baba akisimama UWANJANI na kuanza kumwambia mkewe
, "Mke wangu penzi la jana usiku halikuwa zuri, yaani umekuwa mzito sana na mbaya zaidi ulikuja kitandani bila kuoga na kupiga mswaki" Maneno haya huwa ni dhihaka, dharau na matusi kwa huyo mke, lakini wangekuwa chumbani wenyewe tena mume akinong'ona na kusema maneno hayo hayo basi maneno hayo huwa si matusi bali ni kukosoa.


Tumkosoe Nyerere, kuna mengi amekosea, lakini lazima tutumie maneno yaso maanisha tusi, dharau au kubeza na juhudi zake zingine ambazo kama Taifa hatuna budu kujivunia. Tumkosoe Nyerere kwa lengo la kutaka vingozi wa sasa na wajao wasifanye makosa kama ya Nyerere, kama lengo letu likiwa ni kuwafunda viongozi wetu hatuwezi kutumia lugha chafu lakini kama lengo ni kumdharau basi lazima tutatumia lugha chafu.


Watu wa mataifa mbalimbali wanaukubali mchango wa Nyerere katika kuhakikisha nchi za Afrika zinapata uhuru wake, bado pia viongozi wetu wa sasa hawamfikii Nyerere. Hivi niambie, ni mtoto gani wa Nyerere kabebwa na jina la Nyerere hadi huyo mtoto akawa kiongozi? Hivi Nyerere kafa na mali ya kiasi gani? Hivi hamkuona viongozi wengine walipata madaraka mara baada uhuru wa nchi zao walivyokufa matajiri na tena kwa kuwachia watoto zao urithi wa urais? Hebu kitazame kijiji cha Butiama wakati Nyerere anakufa, au Mkoa wa Mara kwa ujumla wake, kwanini asingependela alipotoka? Mambo haya ndio yanatulazimisha tuchague maneno wakati tunamkosoa Nyerere.

Njano5.
0655345394
 
kuna vitu viwili unavichanganya, naam, viko vitatu vinakutatiza ndugu yangu.


1/ Kukosoa ni ruhusa, na ikizingatiwa hakuna aliyekamilika. Bahati nzuri hata Nyerere alikufa huku akijua vizuri kuwa kukosolewa ni ada na wajibu.


2/Dhihaka ni dharau na ni moja kati ya tabia za utovu wa wa nidhamu.


3/ Unapokosoa bila kuzingatia muktadha, istilahi, mila, ada, na desturi ya jamii huko huwa si kukosoa bali dhihaka na kwa hivyo huwa dharau na utovu wa nidhamu.


Mfano Kikwete akiwa anatekeleza majukumu yake kama mwenyekiti wa CCM, alafu Pius Msekwa akamkosoa hadharani ikiwa huyo Msekwa ni mjumbe wa vikao ambavyo Kikwete ni mwenyekiti wa hivyo vikao basi Msekwa atakuwa hajamkosoa Kikwete bali amemdharau na kumdhihaki.


Baba akisimama UWANJANI na kuanza kumwambia mkewe, "Mke wangu penzi la jana usiku halikuwa zuri, yaani umekuwa mzito sana na mbaya zaidi ulikuja kitandani bila kuoga na kupiga mswaki" Maneno haya huwa ni dhihaka, dharau na matusi kwa huyo mke, lakini wangekuwa chumbani wenyewe tena mume akinong'ona na kusema maneno hayo hayo basi maneno hayo huwa si matusi bali ni kukosoa.


Tumkosoe Nyerere, kuna mengi amekosea, lakini lazima tutumie maneno yaso maanisha tusi, dharau au kubeza na juhudi zake zingine ambazo kama Taifa hatuna budu kujivunia. Tumkosoe Nyerere kwa lengo la kutaka vingozi wa sasa na wajao wasifanye makosa kama ya Nyerere, kama lengo letu likiwa ni kuwafunda viongozi wetu hatuwezi kutumia lugha chafu lakini kama lengo ni kumdharau basi lazima tutatumia lugha chafu.


Watu wa mataifa mbalimbali wanaukubali mchango wa Nyerere katika kuhakikisha nchi za Afrika zinapata uhuru wake, bado pia viongozi wetu wa sasa hawamfikii Nyerere. Hivi niambie, ni mtoto gani wa Nyerere kabebwa na jina la Nyerere hadi huyo mtoto akawa kiongozi? Hivi Nyerere kafa na mali ya kiasi gani? Hivi hamkuona viongozi wengine walipata madaraka mara baada uhuru wa nchi zao walivyokufa matajiri na tena kwa kuwachia watoto zao urithi wa urais? Hebu kitazame kijiji cha Butiama wakati Nyerere anakufa, au Mkoa wa Mara kwa ujumla wake, kwanini asingependela alipotoka? Mambo haya ndio yanatulazimisha tuchague maneno wakati tunamkosoa Nyerere.

Njano5.
0655345394

Hebu wacha kutupigia makelele, Hata hujui unachotaka kukisema.

Mabaya ya Nyerere tutayaanika kila tunapopata wasaa ili wengine wasiyarudie na mazuri yake tutayaanika (kama yapo) ili wayafate.

Dhihaka kwa Nyerere ni muhimu sana kwani hata kwake ilikuwa ni muhimu.

Kumkosea adabu kwa kumtukana hapo si vyema, si kwa Nyerere tu hata kwa mwingine yeyote yule.

Moja katika makosa na madhambi makubwa aliyofaya Nyerere ni kudhulumu mali za watu, yeye aliita kutaifisha. Kiislaam tunafundishwa (nna uhakika kuwa hakuna dini yoyote inayofundisha kudhulumu) kuwa hazidishiwi mwenye kudhulumu ila hasara tu. Kumbuka kuwa Nyerere hana malipo ila hasara tu kwa kudhulumu.

Hapo hakuna dhihaka wala tusi ni ukweli mtupu. Upo hapo ulipo?
 
Nyerere hajawahi hata siku moja kusema kuwa Kabila moja au jengine halifai kuwa rais. Hizi ndiyo kejeli zenu tunazozungumzia hapa kufikia hatua ya kumtwisha maneno ambayo hajawahi kuyasema. I challenge you Faiza to give us the context, quote, when, and where he uttered such words. Otherwise you owe us, JF, an appology for propagating such lies

Mi sijui kama kayasema hayo au hajayasema nimeyachukuwa humuhumu JF kwa hiyo waliyoleta hayo wataleta ushahidi kama wanao. Wrong Number.

Mimi nasema hivi, na hii unaweza kuni quote; Nyerere kadhulumu mali na roho za watu kwa maamuzi yake mabovu ya kidikteta, kama vile alipodhulumu, nyumba, viwanda na mashamba na yeye akaita "kutaifisha". Hiyo ni dhulma na hazidishiwi mwenye kudhulumu ila hasara. Na roho za watu nyingi zilitoka alipokuwa akiwahamisha kwa nguvu kutoka makazi yao ya asili na kuwapeleka vijiji vya ujamaa, wengi walikufa kwa maradhi, kukosa kula, kuumwa na nyoka, kuliwa na simba kuliwa na chui. Hiyo ni dhulma ya roho za watu. Kumbuka hapo hakuna kejeli wala dhihaka.

Na wakati yeye ni Rais wa Tanzania, makamu wa Rais Karume akatangaza "forced marriage" ile ilikuwa ni rapping ya kimbari, unaemuona wewe chukuwa tu kwa nguvu, akitaka asitake. Ni udhalilishaji wa kibinaadam wa hali ya juu, Na Nyerere kama Rais hatujamsikia kukemea wala kuzuia. Hiyo ni dhulma ya hali ya juu.

Upo hapo ulipo.
 
Mi sijui kama kayasema hayo au hajayasema nimeyachukuwa humuhumu JF kwa hiyo waliyoleta hayo wataleta ushahidi kama wanao. Wrong Number.

Mimi nasema hivi, na hii unaweza kuni quote; Nyerere kadhulumu mali na roho za watu kwa maamuzi yake mabovu ya kidikteta, kama vile alipodhulumu, nyumba, viwanda na mashamba na yeye akaita "kutaifisha". Hiyo ni dhulma na hazidishiwi mwenye kudhulumu ila hasara. Na roho za watu nyingi zilitoka alipokuwa akiwahamisha kwa nguvu kutoka makazi yao ya asili na kuwapeleka vijiji vya ujamaa, wengi walikufa kwa maradhi, kukosa kula, kuumwa na nyoka, kuliwa na simba kuliwa na chui. Hiyo ni dhulma ya roho za watu. Kumbuka hapo hakuna kejeli wala dhihaka.

Na wakati yeye ni Rais wa Tanzania, makamu wa Rais Karume akatangaza "forced marriage" ile ilikuwa ni rapping ya kimbari, unaemuona wewe chukuwa tu kwa nguvu, akitaka asitake. Ni udhalilishaji wa kibinaadam wa hali ya juu, Na Nyerere kama Rais hatujamsikia kukemea wala kuzuia. Hiyo ni dhulma ya hali ya juu.

Upo hapo ulipo.
Acha kuruka viunzi. Siyo kila kitu kinachoandikwa JF ni sahihi. Na ukinukulu kitu kisicho cha ukweli inaashiria kuwa na wewe unakubaliana na uwongo huo. Nyerere hajawahi kusema popote pale kuwa hakuna kabila lolote Tanzania lisilostahili kutoa rais wa nchi. That is the issue. Hayo ya ndoa za akina Karume ni kuruka viunzi. My issue was Nyerere na ukabila. Full stop.
 
Back
Top Bottom