Leteni Maswali ya Kiafya Niwasaidie

Mchumia juani

Member
Jan 28, 2008
27
13
Napenda kuwa julisha wana JF kuwa nakaribisheni maswali mafupi mafupi yanayohusu tatizo lolote la kiafya.Maswali yote yatajibiwa mara moja kwa wiki iwe ni tatizo ulilonalo wewe binafsi au ndugu,jirani,rafiki au mtu yeyote unayemfahamu,Kumbuka yawe mafupi ili watu wengi zaidi wapate nafasi ya kushauriwa na mimi.

Nitakupa ushauri kadri ninavyoweza.Usiwe na wasiwasi niko ktk profession hii.
 
Napenda kuwa julisha wana JF kuwa nakaribisheni maswali mafupi mafupi yanayohusu tatizo lolote la kiafya.Maswali yote yatajibiwa mara moja kwa wiki iwe ni tatizo ulilonalo wewe binafsi au ndugu,jirani,rafiki au mtu yeyote unayemfahamu,Kumbuka yawe mafupi ili watu wengi zaidi wapate nafasi ya kushauriwa na mimi.Nitakupa ushauri kadri ninavyoweza.Usiwe na wasiwasi niko ktk profession hii
Shukrani sana Mkuu kwa msaada wako hope tutaanza kumimina matatizo yetu hapa.Samahani mkuu unaweza kubadili rangi ya maandishi yako
 
Woga/hofu!
Avatar yako imenitia hofu sana. Teh..teh... yaweza kuwa tiba kwa mtu anayesinzia kazini.
 
Wabongo bwana ,mimi nimeomba maswali niwasaidieni mara ooh Avatar inatisha,tutafika kweli tunakoenda? Anyway msiiogope avatar na kama unataka kujua kama ni tiba asilia au wetern nijaribu kwa swali!
Nawashukuru wote walionipongeza na siwalaumu walioponda-Uhuru maoni
 
Mchumia Juani, nikupashe : nilihisi kutapika nilipoiona hii avatar ukizingatia kuwa nlikuwa nimetoka kupata msosi..........puuuuh! Inatia kinyaaa.....Tuyaache!

Mimi nina Grave's disease au Hyper thyroidism. Kwa ufupi ni ugonjwa ambao hauna maumizu yoyote ila it has got to do with one's hormones!Nimeambiwa nisile baadhi ya vyakula vinavyoweza kuongeza sumu, lkn sijajua ni vyakulka gani,lkn mie sivijui. Je waweza kuniambia ni vyakula gani haswaa?
Pia naambiwa ninaweza kutumia anti-thyroid drugs kwa muda mrefu - can even take two years- je hazina side-effect endapo nitaacha??
 
Mchumia juani,

If you want watu wakuulize kama unavyodai wewe 'doctor' basi badilisha avatar! Au tushtaki kwa Admin akufungie! Sii unajua rules za JF? Onyo- then ban!

Hii avatar inakudhalilisha na kushusha hadhi ya JF!
 
I see MJ naomba nikushukuru sana kwa hii avatar yako- mtoto wangu mdogo hanisumbui tena kwenye kula! hii nayo ni dawa tosha.
Nina swali la jambo ambalo lilishajadiliwa hapa siku za nyuma lakini hakukuwa na mtu aliyetoa point ya kitaalamu, labda ulikua hujajoin by then.Punyeto ina madhara gani kiafya?Hili suala ni nyeti sana kwa kuwa hutusaidia kupunguza vicheche na kutowasumbua wake zetu wanapodai wamechoka.
 
Aisee mganga. Mimi nimekaa nime-relax, ghafla ankle inauma ghafla hata siwezi kutembea. Sijacheza kabumbu kwa wiki kadhaa. Maumivu ni ghafla tu, wala hamna uvimbe. Sijaanguka kwenye baa ya baba Chuwa wala nini. Hii haijawahi tokea. Ni nini? Yaani noma, hata movement ya nanihii ni matatizo kidogo.
 
SteveD, usicheke magonjwa ya wenzako. Mimi niko vere siriasi.

Tatizo huyu mganga anakusanya matatizo, akishajibu watu tuko mahututi. Halafu wikiendi huku hakuna G.P. Ukienda A&E kama hutoki mchuzi kichwani wanakukalisha masaa 4, halafu hapo unaondoka na flu. Duuh, ngoja nivumilie.
 
Mganga Mi Nninashida Mbili Tatu Ntashukuru Sana Kama Utanisaidia::::

1))ninajiskia Nimefanya Mapenzi Kama Nitajitahidi Kwenda Chumvini..hivi Majuzi Nimeenda Chumvini Na Kkutana Na Vitu Kama Si Cid Aliomwagiwa Bwana Kabebene Basi Sulphuric Acid.....sasa Hivi Nina Miezi Mitatu Ninasikia Ukakasi Kama Sijapiga Mswaki Miaka Kumi,,na Toka Hapo Mimi Na Chumvini Basi,,naomba Nisaidie Nitumie Dawa Gani,,,,

22)))pili Nina Tatizo La Kuvua condom Kila Baada Ya goli La Kwanza ...na Nimejitahidi Sana Lakini Mwanzoni Navaa Nikishakoja ,,,nikienda La Pili Uku Nikilamba Chumvi Najikuta Nimeenda Direct Kama Nilivyozaliwa,,,,hili Naona Kama Ugonjwa,,mganga Nsaidie Kwa Hili La Naomba Mchango Wako Wa Sanda Mampema

ahsante
 
Mheshimiwa,

Naomba ufafanuzi wa ugonjwa wa kisukari, kama ifuatavyo:

1) Unasababishwa na nini?

2) Unajuaje kama umeupata?

3) Athari zake kwenye mwili ni zipi?

4) Je, unatibika?

Asante.

./MH
 
Punyeto ina madhara gani kiafya?Hili suala ni nyeti sana kwa kuwa hutusaidia kupunguza vicheche na kutowasumbua wake zetu wanapodai wamechoka.

Haina madhara yoyote, isipokuwa tu psychological effect kama watu watagundua kuwa mtu ana-practice hicho kitu.

Utafiti wa kisayansi umeonyesha kuwa wanaume wanao masturbate wana risk ndogo sana ya kupata saratani ya prostate, ugonjwa ambao hutokea kwa wanaume tu na huweza kutokea hasa kwenye umri mkubwa (say 60s onwards)

Masturbation ambayo lengo lake ni kupunguza hamu tu haina madhara, ila ikifikia kiasi cha kumuathiri mtu katika tendo kujamiiana na mwenziwe, basi inabidi mtu huyo apate ushauri wa kitaalamu toka kwa psychologist au psychiatrist kwa sababu kitu kinachomsukuma mtu kufanya hivyo siyo hamu tena bali ni aina fulani ya "escapism"
 
Shukrani Paloma kwa kutojali Avator yangu hata hivyo kwa kuwa nina muda mfupi leo nitakujibu kwa ufupi sana ila naahidi kukujibu kwa kirefu zaidi nikipata Muda,
Ni kweli unapokuwa na Grave's disease kuna baadhi ya vyakula ambavyo unashauriwa usile,kwa kuwa thyroid hormones (T3 na T4) zinakuwa nyingi mwilini,ni vema kuepuka vyakula ambavyo vitasababisha thyroid hormone zizidi mwilini,kumbuka pia hyperthyroidism inaweza kutokana na Iodine deficiency kwa hiyo vyakula vyenye madini hafifu ya Iodine havitasaidia,lakini hata vyakula vinavyo interfere Iodine metabolism pia si vizuri,vyakula hivyo huitwa Goitrogenic foods na mfano halisi kabisa ni kama Kabeji.
Kuhusu antithyroid hakuna dawa isiyo na madhara,kwa mfano ukitumia antithyroid kwa muda mrefu unaweza kupata hypothyriodism ambayo dalili zake kubwa ni 'Cold intorelance' na kuna athari kubwa zaidi zinazoitwa thyroid crisis ambazo unahitaji kuwasiliana na daktari wako mara kwa mara.
Hata hivyo ni vema daktari akupe elimu ya kutosha kuhusu madhara ya dawa hizo hasa katika nguvu za kiume n.k
Nikipata nafasi ya kutosha nitakujibu kwa kirefu
Ubarikiwe.
 
Pole Nzokanhyilu,Hata hivy tatizo lako inawezekana si kubwa sana,japokuwa hujanipa maelezo ya kutosha na kwa muono wangu naona hujaqualify kusema una Arthritis,jaribu kutumia NSAIDS kama vile Diclofenac tabs 50mg TDS kwa siku tatu au Diclofenac cream ya kuchua kwa siku 3-5 kisha tuwasiliane zaidi kama hutapata nafuu,dawa hizi ni overcounter prescription.
Shukrani
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom