Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muungano

"I support Let Zanzibar Go Movement 2012"! Wazanzibar wanataka kufanya majaribio/Utafiti ili waone nini matokeo yake. Wanatak kutenganisha mabehewa mawili katika treni iliyo kwenye mwendo, nia na madhumuni wajue kipi kitaendelea na safari kati ya kichwa cha treni chenye mabehewa(Tanganyika) na mabehewa mawili(Zanzibar) yaliyochomolewa wakati treni inatembea.
 
yaani umeandika upuuzi mtupuuuuu yaani kama ni mtihani bac 0+++=000000000000000000000, unajua watz wengi ni wajinga hawajui haki zao linapo kuja swala la kudai haki zao watawala ni rahisi sana kubadili upepo hoja sio nani ananufaika na muungano nani hanufaiki wananchi wa znz wanataka mabadiliko ya mfumo wa muungano wameona mfumo uliokuwepo hauna faida kwao je ni kosa kisheria? wanataka kura ya maoni iitishwe ili tusipoteze pesa na muda kuwalazimisha watu kuunda katiba wakati muungano wenyewe haupo kisheria kwa ujinga wetu watz maendeleo tutaendelea kuyaona kwenye tv tu aibu tupu
Wala hujakosea huo mtihani wa 0+++=? nisingeuweza ila weye ulosoma sana.

Kati yetu sisi na wewe nani asojua haki zake maana unachozungumzia sio madai ya haki ya Wazanzibar pale inapostahili. Kama wewe kweli unaijua haki yako kwa nini usimuulize kiongozi wako Dr.Shein, Bilal Maalim Seif na wengineo ambao wananufaika na Muungano? hayo maandamano kwa nini yasielekee Ikulu kwa Dr,Shein mtake kupata majibu lakini mnaandamana kwa kuitazam Bara ambayo haipo huko. haya wee nambie kitu chochote ambacho bara inanufaika kutoka Zanzibar maanake twende kwa maelezo binafsi kusema kweli sielewi bara tunanufaika nini na muungano zaidi ya kuisoma Historia ya nchi hizi. Kwa fikra zako unafikiri hawa watu wanalipwa na Wazanzibar au unataka nasi tunaze kuuliza hawa watu tunaowalipa mabillionni wakati sii Wabara inakuwaje?.

Binafsi mkuu wangu napenda sana muungano uvunjike hata kesho maana sababu hasa ya muungano ilitokana na Zanzibar kuwa nchi ya Kikomunist. Ukomunist haupo tena kina Abraham babu wameisha kufa, hao walobakia kina Nassor Moyo na Salim hawana tena nguvu ya kurudisha Ukomunist kwanza hakuna mtu anaupenda hivyo sioni sababu ya kuendelea kuuliza Muungano.

Kifupi haki yetu haitokani na Muungano wala hakuna jambo lolote ambalo Muungano huu unatuongezea zaidi ya kuwafadhili nyie kama protectorate alipewa Sultan na waingereza. lakini waulize wazanzibar watasema Muingereza alikuwa mbaya sana wakati Sultan mwenyewe alitaka kuwa protected against Portuguese na makoloni mengineyo. Ni akili mbovu kutoelewa maana hasa kwa Wazanzibar wahamiaji ambao wamepoteza uraia huko walikotoka sasa wanatafuta nchi na makazi mapya kwa kudai Uhuru wa Sultan ulopinduliwa.

Huwezi kumnyofoa Mzanzibar kwa kabila hata kidogo isipokuwa kwa mahamiaji ambao wote wana historia ya kukimbia makwao toka hao WaOman, Washiraz, Wabarush, Wanyamwezi hadi Wangazija wote wampewa hifadhi sasa mnataka kuifanya nchi hiyo kama Wayahudi - Mna akili sana nyie!

Sisi tunaelewa matatizo yetu wala hayahusiani na kabila, jinsia wala rangi wa tu isipokuwa uongozi wa CCM ambao nyie wasomi mlipiga kura na kuchagua serikali ya mseto ambayo viongozi wake wote ni Wazanzibar bado hamtaki wakati wenzenu wanakula nchi. Na kibaya zaidi kila kiongozi wenu anapoiba huko anakuja jenga bara pengine hili mngelitazama zaidi kuliko kudai nchi wakati hao viongozi wenu wamefungua biashara na account zao bara. Nimekumaliza mkuu kaa pembeni acha wenye kuelewa maana wazungumze.
 
Let Zanzibar go!! Asante Mzee Mwanakijiji kwa darasa lako, let them decide their destiny kuliko wanavyotuandama wakati uamuzi uko mikononi mwao! Let them go. Waliamua kuvunja katiba ya Jamhuri ya Muungano kwa kujitangazia kuwa wao ni nchi ndani ya nchi na hakuna aliyewauliza, Walivunja katiba ya JMT ya kumpa Rais wa Zanzibar uamiri jeshi mwingine badala ya Rais wa JMT hakuna aliyewauliza!! Sasa kipi kinawashinda kuanzisha mchakato kwenye bunge lao wakaondoka? Ushauri wa Mzee Mwanakijiji ni mzuri sana kwa hatima ya Wazanzibar. Ninaunga mkono ili wachukue hata waondoke! tena ikiwezekana july 1 , 2012
 
na waende wakapewe misaada na ndugu zao wa Oman!lkn for sure watatukumbuka na ukalimu wetu!!

kupewa misaada na waoman kwani kunatatizo gani? na sifikirii kama kuna mzenji hata mmoja atakae kukumbukeni kwa
jema isipokua kwa ujambazi na kutuzalilisha.
 
Mkuu hapo nilipoweka rangi nyekundu umechanganya madawa/ umefanya madudu.

Isomeke Bunge la Tanganyika lilifuata sheria na katika kufuata sheria pia ilivunja sheria kwani baada ya sheria ile Bunge la Tanganyika halikukaa tena kama Bunge la Tanganyika. Nani aliwapa uwezo wa kuiua serikali ya Tanganyika na Bunge la Tanganyika?

Pia isomeke Muungano ni wa Tangayika tu. Hakuna nchi iliyoitwa bara au inayoitwa bara. Usifuate siasa za kisanii/ mazingaombwe.

Jikumbushe jina la Muungano. Lilikuwa ni Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na lilipofupishwa likawa Jamhuri ya Muungano wa TanZanIA.
Mazingaombwe/ kiini macho tu ndio yataleta neno bara.

Sio nia yangu kuanzisha mjadala katika hili lakini tusiwachanganye wananchi na wasomaji wa JF.

Let us call spade a spade!

Nonda, umetoka usingizini au? Uhalali au uharam au 'whatever' juu ya Muungano huu mmeshasema ktk mikutano yenu na JUMIKI, kilichopo hapa ni: LET ZANZIBARI GO!
 
prof. Idrissa Kikula amewajaza wazanzibar pale chuo cha ardhi, amepelekwa UDOM nako admistration wamejaa wazenji, kila sehemu yenye bosi mzenji basi ujue kuna harufu ya uzenji, aaaaagh!! let them go to take our positions, LET THEM GOO!
 
Inasikitisha kuona kuwa sasa tumefikia hapa, tena mara nyingi tu! Tukumbuke kwamba sasa hivi kuna wale ambao wanachekelea mdahalo huu, wanajua fika kuwa tumefika wanapotaka tufike.

Nitasisitiza kuwa muungano wowote ule ambao uko nje na matakwa ya mabepari na watwana wa magharibi(kama wapo) basi ni karaha kwao. Ni mtazamo wangu.


Muungano lazima uudumishwe.
 
Mzee Mwanakijiji;4005445]Ukiwaskiliza sana baadhi ya wapinga muungano kwa kweli kabisa wamejawa chuki isiyo na kifani na chuki hiyo imezaa matunda meusi katika madhihirisho ya chuki dhidi ya watu wa Bara na Wakristu.

Lakini kitu kimoja ambacho watu wengi hawataki kukifikiria ni kuwa hawa watu wanaopinga Muungano wao wanadai "nchi". Sasa hakuna aliyewauliza kwamba mbona katiba ya Zanzibar imefanyiwa mabadiliko na kuitangaza kuwa Zanzibar ni nchi? Sasa kama tayari Zanzibar ni nchi wanachodai hawa ni nini? Haiwezekani kuwa wanachodai ni nchi kwani nchi tayari wanayo na Katiba ya Zanzibar inasema hivyo! Wanachotaka siyo nchi! Wanachotaka ni kuwa nje ya Muungano! Hivi ni vitu viwili tofauti.

Pendekezo langu ni njia nyepesi za Wazanzibari kujiondoa kwenye Muungano bila kufanya maandamano, mihadhara wala kuwashtumu watu wa Tanganyika. Wazanzibari wakitaka kutoka kweli kwenye Muungano wanaweza kufanya hivyo ndani ya wiki chache tu na wakawa nchi. Nina uhakika serikali ya Muungano haitotumia nguvu kuwalazimisha kubakia! Nyerere mwenyewe alishasema kuwa hawezi kuwalazimisha Wazanzibari kubakia kwenye Muungano.

Njia ya kwanza
Njia ya kwanza na nyepesi zaidi ya kuweza kujitoa kwenye Muungano ni kwa wananchi wa Zanzibar wakiongozwa na hawa wana- uamsho wawatake watendaji wote wa Muungano wenye asili ya Zanzibar kuachia nafasi zao mara moja na kurudi Zanzibar!

Hii ni pamoja na majaji, wabunge, mawaziri, maafisa wa polisi na vyombo vingine vya usalama, na wantedaji wengine ambao wako kwenye Muungano. Badala ya kuililia Tanganyika kila kukicha kuwa inawabana mashehe wa Zanzibari wenye kuongoza vuguvugu la kutoka kwenye Muungano waanzishe mihadhara ya kuwataka Wazanzibari wenzao ambao wanatumikia Muungano waachilie nafasi hizo.

Binafsi ningependekeza kama wataniruhusu waanzishe harakati hizo ili viongozi wote hawa waachilie nafasi zo ifikapo Disemba 10, 2012. Hii ni pamoja na Makamu wa Rais Ghaib Bilal, jaji mkuu na wengine.
Hawa wote wakishawishiwa kuondoka Wazanzibari wajiandae ama kuwapatia pensheni au kuwatafutia nafasi kwenye serikali ya nchi ya Zanzibar.
Sasa hawa wote wakikubali kuondoka kwenye nafasi zao za Muungano Zanzibar itapata wataalamu wengine wengi.
Lakini pia itafungua ajira za Watanganyika wengi ambao wangeweza kushika nafasi zinazoshikiliwa na Wazanzibari.
Mashehe wa uamsho waende mbali zaidi katik akudai nchi yao. Waanze kuwahamasisha Wazanzibari walioko bara kuamua kuondoka bara na kurudi Zanzibar ili kuendesha shughuli zao huko.

Wale Wapemba na Wazanzibari waliona maeneo ya ardhi Bara. Hivi ndivyo ilivyotokea Sudan ya Kusini ambapo baada ya nchi hiyo kujitenga Wasudan ya Kusini waliokuwa wanafanya kazi Khartoum waliacha kazi zao na wengi wao wameamua kurudi kwenye nchi yao kuanza kuijenga.

Hili pia litakuwa na faida kubwa sana kwa Zanzibar kwani itapata watu wengi zaidi wenye uwezo na utajiri mkubwa na vile vile itabidi iwaandalie viwanja vipya vya kilimo na makazi maana vile vya bara itabidi waviachilie kuwapisha Watanganyika ambao wanalalamikia kukosa ardhi au kupatiwa ardhi isiy nzuri. Na pia wafanyabiashara hao wa Kizanzibari watakaporudi Zanzibar na kama watataka kuja kufanya biashara Tanganyika itabidi waje kama wawekezaji
Hivyo hilo ni jjambo la kwanza nawashauri wana uamsho; hamasisheni Wazanzibari waondoke Tanzania bara ili warudi Zanzibar ambako watapatiwa nafasi bora zaidi za ajira. Mtakapofanya hivyo, na watu wa Bara nao itabidi waanze kuondoka Zanzibar japo hapo nina uhakika kutakuwa na kazi kidogo. Watu wa Bara ni kina nani Zanzibar?

Nina uhakika wapo Watanganyika ambao watashukuru sana kwa wao pia kupewa nafasi ya kupumua kuliko kila siku kuimbiwa "Zanzibar, Zanzibar"; Watu wa Bara hatutaki kuonekana tunawang'ang'ania Wazanzibari wakati nguvu yote ya kutoka kwenye Muungano wanayo wao.

Nidhahiri kuwa hakuna mwenye uwezo huo na sasa kilichobakia ni sote kwa pamoja kutoka Bara tuseme nasi pasi ya shaka kuwa LET ZANZIBAR GO- Iacheni Zanzibar iende.
Itaenda wapi zaidi ya kuwa kwenye kivuli cha Tanganyika ndani au nje ya Muungano
HUU NI MWANZO WA "LET ZANZIBAR GO MOVEMENT 2012"; Kama unaunga mkono kuwaacha Wazanzibar wajitoe kwenye Muungano weka kwenye sahihi yako "I support Let Zanzibar Go Movement 2012"! Tuwasaidie waharikishe wajitoe kwani hakuna
Mkandara;4004870] Wazanzibar wanataka kujitoa ktk Muungano wajadili na viongozi wao kisha wakilisheni ombi lenu la kujikata halafu ndipo itapangwa ushirika wa kimataifa kama tulivyo na nchi nyingine iwe Kenya au Uganda. uamuzi ni wenu sisi bara hatuna nongwa kabisa isipokuwa mjue tu ya kwamba ni WATU wanaojenga nchi na sii ARDHI kwa watu wake. Maadam wapo Wazanzibar wengi bara ambao kwa matakwa haya watakuja kuwa wageni wakiishi kwa visa na work permit sijui hapa mtakuja sema nini maana huu mungano mnautazama kwa bendera na ramani.

Uhuru ni wa WATU sii wa ardhi na mipaka yake hata siku moja, maana hata wewe unaweza kuja bara ukanunua ardhi na ikawa yako au waarabu wanaweza kuja Zanzibar nunua ardhi ukahamishwa wewe kama ilivyotokea Palestine.

Sasa kama nyie mnaona ardhi ni bora zaidi kuliko wananchi wenyewe jikateni wala hatuna noma kabisa isipokuwa ktk vichwa vyenu wafikirieni WATU wanaoishi mikoani maana kuna waarabu wenye asili ya Zanzibar (kiOman), Washiraz na Wangazija waliohamia bara na wanajulikana kama Wazanzibar. Kama umegundua hakuna Wabara wanaohamia Zanzibar, wamekuja fanya biashara au kufanya kazi huko lakini wao wanajua kuwa ni wageni kama waphilipino kule Dubai kisha ardhi yenyewe iko wapi? lakini kwa Wazanzibar waliohamia bara au wanaotaka kuhamia bara ardhi kubwa na huru kwao kufanya lolote. Muungano huu ni faida kubwa kwa Wazanzibar kuliko bara kumbuka Palestine, Rwanda na Burundi wanachokiomba ni ardhi zaidi wangemshukuru Mungu, nyie ndio kwanza mnataka kujikata kwa ardhi kidogo wakati mko mamillioWazanzibar
tumewafungulia kila kitabu na kila kurasa. Tunawasaidia, nanyi onyesheni nia ya kujitenga July 1 2012. Hii kampeni ya Let Zanzibar go ndiyo imeanza na mwitikio unatia raha. Pita vijiweni uone jinsi Wabara walivyohamasika na nchi yao.

Hakuna Mzanzibar atakayedaiwa chochote midhali kipo ndani ya begi lake. Wale wenye dhamana zisizohamishika hakikisheni mnapata wanunuzi kipindi hiki ili kuepuka hasara.
Huu ni ukarimu kwasababu hakuna mzanzibar aliyewahi kubeba nyumba ardhi au duka kuja nalo. Lakini hatazuiliwa kuondoka na amana zake pale atakapoziuza.

Ni vema mkaondoka wenyewe kwasababu mtakuwa na wakati wa kujipanga. Mkisubiri kufukuzwa mtajikuta katika wakati mgumu.
Hakuna mbara atakayenyanyua dongo, kijiwe,unyoya au njiti kumpiga mtu.
Wabara hatujafikia kiwango hicho cha upuuzi
Tutatumia njia ifuatayo na ambayo imependekezwa na mwenzetu MM.
Tutaomba serikali moja bila kuwa na Mwanza au Zanzibar. Zote ziwe JMT.

Tunajua mlivyo na uchungu wa nchi yenu hili hamtalikubali na hapo mtaondoka bila matayarisho na mtapata hasara.

Kuna mambo ambayo sasa ni 'off the table''
1. Hakuna serikali 3 kwasababu hamna cha kuchangia katika serikali ya muungano. Hatudhani kama mumegoma kulipa umeme wa bilioni 50 mtaweza kulipa bill ya bilioni 500!
Hata kama mtaweza mtabakisha nini chunguni?

2. Hatuhitaji mkataba. Hatuna kitu ambacho tunadhani tutafaidika kutoka katika mkataba.
Mkataba ni njia ya ulaghai ya chako ni chetu, changu ni changu. Hatuna tutakachofadika

3. Hatuhitaji uhusiano special, tutakutana SADC, EAC, COMESA n.k.

Nashadidia yaliyosemwa,kama mnadhani makamu wa rais na mawaziri ni vibaraka, basi ninyi wafanyakazi wa Zanzibar wazalendo ndani ya muungano onyesheni mfano.
Pisheni huko mlikoajiriwa ili Wabara wafaidi matunda ya nchi yao kama mtakavyofaidi yenu.
Vijana wa bara mnaotembea na bahasha za khaki(CV), hili ni kuwakumbusha kuwa dhiki zenu zinalipwa fadhila na matusi, kejeli na moto wa wazanzibar walioziba nafasi zenu.

Watanganyika, hatuna tunachofaidika na Zanzibar zaidi ya hasara kama Mluguru kulipia bill za umeme kwa UAMSHO [/QUOTE]
Wazanzibar this is athe point of no return, hamhitaji maandamano wala kelele, nafasi ya kujitoa ipo wazi nasi tutawasaidia

LET ZANZIBAR GO! ZANZIBAR SHOULD GO ASAP!
 
Tuliwapenda sana kwa miaka 46 lakini naona hawapendeki! potelea mbali, hakuna anayekataa kuwapatia talaka wanayoitaka!!! Wanachotakiwa kufanya ni kuomba talaka yao, waende! Let them go. Tumechoka na kelele zao kila siku.
 
Nonda, umetoka usingizini au? Uhalali au uharam au 'whatever' juu ya Muungano huu mmeshasema ktk mikutano yenu na JUMIKI, kilichopo hapa ni: LET ZANZIBARI GO!
Zinedine
Bado nimelala..niko kwenye ndoto kuwa niko katika mikutano yetu na JUMIKI.:confused2:


Mkuu kama umesoma mchango wangu na kuelewa nimefanya masahihisho kidogo juu ya matumizi ya majina Tanzania na bara katika mchango wa Pasco.

Unasema:Kilichopo hapa ni :Let ZANZIBARI GO!

Why don't we let Zanzibar go?

Haiwezekani baada ya gazabu, hasira tulizonazo kuwaambia "pack and go!"

I would rather have the courage to say "GO!"

Kwa sababu gani hatu"opt" hii option? Hakuna mwenye uwezo/ujasiri katika viongozi,wabunge ,watendaji wa Tanganyika wa kusema" Zanzibar go!"

Nani ametoka usingizini? Zinadine au Nonda?

Kwa bahati mbaya Mijadala ya sasa imeanza/imeanzishwa juu ya dhana kuwa UAMSHO(waislamu wa Zanzibar) wamechoma makanisa. This was a false start kwa mijadala hii. Tumeingia mtego wa Magamba.
 
Nonda, mkuu ebu tazama picha hiyo hapo juu kisha utuambie kama kweli hao ni Magamba?.. Hawa ni wananchi wenye hasira na wenye kuitaka haki yao kwa nini nasi tusiwasikilize ikiwa tunawasikia watu wa Palestine au Burma..

Maadam tunawapa muda tosha ifikapo July mosi 2014 wawe tayari wameisha fanya maamuzi ya kura za maoni basi hatuna sababu ya kuendelea kulonga. Kazi kwao, badala ya kuandamana walivamie bunge lao kesho na kuomba kupiga kura za maoni kama walivyofanya mwaka 2010.

Viongozi wa serikali ya mseto kutoka CUF na CCM Zanzibar (baraza la Mapinduzi) wapeni wananchi wenu haki yao ya msingi, tena kama ikiwezekana nasi bara tuandamane kuwaunga mkono Wazanzibar ili wapewe ruksa ya haki yao kudai kuondoka ktk Muungano ifikapo July 1 2014.
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom