Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muungano

..BOT ilianzishwa kutokana na mtaji wa fedha za Tanganyika na Zanzibar tulizopewa na EA currency board.

Hapa ndipo ambapo Mzee Mtei angesaidia kusema Tanganyika ilichangia asilimia ngapi ya mtaji wa kuanzisha BOT na Zanzibar walichangia ngapi. Hii ingepunguza/ingezima malalamiko ya tunawagawia au tunanyonywa.
Nonda,
..Baada ya kusema hayo naomba unielekeze popote pale ambapo imehalaishwa kwamba Tanganyika ilipie gharama za umeme za Zanzibar, au tuwalipe mishahara SMZ, au tuchangie shughuli za muungano na Zanzibar wasichangie suala lolote lile, au wajumbe toka Zanzibar ktk tume ya katiba walipwe na serikali ya Tanganyika.

Kwa kutaka maelezo kutoka kwangu, umekusudia kutania? Kuchekesha wanajf? Au umekusudia kupandisha mizuka ya walio "bendera hufuata upepo"?

Shirika La umeme ni shirika la kibiashara au shirika la kugawa sadaka?
Je shirika la Umeme,TANESCO linaendeshwa kibiashara au kisiasa?

Nijuavyo ni kuwa TANESCO wanafanya biashara na Shirika la Umeme Zanzibar. Hapo kuna mkataba wa kibiashara. Anaeshindwa kutimiza masharti ya mkataba, apate adhabu. Mteja/mlalahoi ambaye halipi umeme anakatiwa umeme.

Sasa kama TANESCO wanawapa sadaka Shirika la umeme Zanzibar. Huo ni udhaifu wa TANESCO.
Kama Tanganyika analipia gharama za umeme za Zanzibar inawezekana ndio kilainisho/hongo ya kuwafanya wazanzibari wakubali serikali moja.

Mimi ningesema kila mtu ababe msalaba wake! Tanganyika ilipie gharama zake, Zanzibar walipie gharama zao na pale penye mambo ya muungano ndio walipie kwa pamoja.

After all, there is no free lunch!

Nonda,
..Pamoja na hayo Zanzibar wakaanzisha tena PBZ ambayo toka wakati wa Karume mpaka utawala wa Salmini ndiyo walikuwa wanahifadhi fedha zao humo. Yaani PBZ ndiyo ilikuwa benki kuu ya Zanzibar kwa muda wote huo.

..Sasa suala hili lilishughulikiwa na msuluhishi wa kimataifa ambapo pamoja na mambo mengine alielekeza kwamba Zanzibar iwe inapewa hiyo 4.5% na zaidi ilazimishwe kuweka akiba yake BOT. Baada ya uamuzi huo ndiyo ukaona hata Zanzibar inateua Naibu Gavana wa BOT.

..Baada ya kusema hayo naomba unielekeze popote pale ambapo imehalaishwa kwamba Tanganyika tuwalipe mishahara SMZ
JokaKuu,
Hapo umeandika kuwa Zanzibar wameweka pesa zao BOT sasa wakitaka kulipa mishahara ya wafanyakazi wao inawapasa wachote kutoka hiyo akiba yao. Kama walilazimishwa kuweka akiba yao BOT na kuifanya PBZ isite kuwa benki ya serikali ya Zanzibar. Hizo pesa bila shaka zitatoka katika fedha zao zilizopo BOT au BOT wakiweka akiba ya mteja wake huwa hawarudishi pale mteja anapotaka sehemu ya akiba yake?
Nonda,
..Baada ya kusema hayo naomba unielekeze popote pale ambapo imehalaishwa kwamba Tanganyika ilipie gharama za tuchangie shughuli za muungano na Zanzibar wasichangie suala lolote lile, au wajumbe toka Zanzibar ktk tume ya katiba walipwe na serikali ya Tanganyika.
JokaKuu
Hapa ndio utaelewa kuwa sisi wabara(watanganyika) kuwa ni wadanganyika.
Bado hujaelewa kuwa hakuna hazina ya Tanganyika? Tanganyika haipo. Tanganyika haichangii chochote katika Muungano. Hazina ni ya muungano, serikali ya Muungano.
Wabara(wadanganyika) tunapata sadaka kutoka hazina ya muungano. kwa bahati ya werevu wa "wala urojo/mayakhe"
Wao wanapata kutoka hazina ya Zanzibar na hazina ya Muungano.

Kama tutaelewa somo la leo. maujanja ni kurejesha Tanganyika ,ili iwepo hazina ya Tanganyika, hazina ya Zanzibar na hazina ya muungano. Tumelikoroga sasa inabidi tulinywe tu, kaka!

Nafikiri baada ya Mwalimu kuona kosa lake alilolifanya juu ya kuua serikali ya Tanganyika, ndio aliamua afanye jitihada ya kuua serikali ya Zanzibar. Ndio ile janja ya serikali mbili kuelekea moja.

Lakini pia alijitengenezea njia nyengine kusema kuwa EAC ikizaliwa tena, ni vyema iundwe serikali ya Tanganyika na serikali ya Zanzibar iliyopo zijiunge EAC kama serikali zinazojitegemea. Hapa lilitokea G55 lililoanza kutoka usingizini na kuidai Tanganyika.

Tukiipata Tanganyika yetu na udanganyifu wa muungano tunaupatia dawa yake.

Je wadanganyika tutaendela kudanganyika au tutarudi Tanganyika?
JokaKuu
Hakuna serikali ya Tanganyika, in principle; serikali ya Muungano kama unavyosema wewe ni de-facto serikali ya Tanganyika lakini ukweli ni kuwa serikali ya Muungano ni monster tu, anatafuna Tanganyika, anatafuna Zanzibar.
 
Nonda,
Kwa nini unapoteza nguvu zako nyingi sana kutafuta kilichotokea wakati uamuzi wanao Wazanzibar mkononi?.. Nimeshasema sana juu ya mahusiano ya kindoa. Kama mke anataka taraka, huomba hiyo taraka na sii swala la watoto kujadiliana wao kuitaka taraka ya mama/baba. Kama wanataka kweli basi wawashauri mama/baba (Baraza la Mapinduzi) waiombe hiyo taraka kutokana na kwamba Bara inawatesa sijui watoto au hata mzazi mwenyewe.

Kisha baraza hilo litawakilisha hoja hiyo na tutafikia kujitenga wala haina shaka, lakini haya ya mtoto kulalamika kila siku juu ya ndoa kana kwamba wao ndio aanahemewa haiwezi kuharibu ndoa ya wapendanao, na siku zote sisi bara hatuwezi kuitoa taraka wala kuiomba kwa sababu hatuoni matatizo ya ndoa yetu kwani ni wajibu wetu kuwasaidia ndugu zetu Wazanzibar.

Ila nawasihi sana Wazanzibar watazame undani wa kuvunja muungano wapate kujua Zanzibar itatofautiana nini na Zanzibar hii iliyopo maana kinacholiliwa na hawa viongozi wetu ni madaraka zaidi ya waliyopewa, ni hawa watu wachache wapate kufanya maamuzi yao pale inapofikia maswala la Zanzibar japokuwa muda wote Wazanzibar wamehusishwa ktk maswala ya muungano. Kwa upande mwingine niseme kwamba wanataka maswala yasiyokuwa ya muungano yaongezeke kwao japokuwa wao wanaweza kushirikishwa ya bara.

La muhimu kama Jokakuu alivyokueleza ni kwamba sasa hivi hakuna serikali ya Tanganyika isipokuwa kuna serikali ya muungano ambayo viongozi wa Zanzibar wanahusika pia. Kila maamuzi yanayofanyika kuhusu bunge la Muungano Wazanzibar wanahusika, tena labda nikufafanulie zaidi tu kwamba yale yasiyokuwa ya Muungano wabara hawaingilii kabisa Zanzibar ila kwa hayo hayo huku bara Wazanzibar wanaingilia.

Huwezi kuwa na rais kutoka Zanzibar halafu azuiwe kuingilia yasiyokuwa ya muungano, huwezi kuwa na Makamu wa rais Mzanzibar halafu asiruhusiwe kuyaingilia yasokuwa ya muungani, pia waziri mkuu hawezi kuzuiwa kuingilia yasokuwa ya Muungano (Salim A. Salim) na mawaziri wengine wote waliopo tk serikali ya muungano. Wakati huo huo hakuna rais, makamu wala waziri mkuu wa bara anayeweza kuingilia yasiyokuwa ktk muungano Zanzibar. Walisema wazi hawamtambui Pinda..ktk serikali ya muungano hakuna nafasi hata moja ya uongozi ambayo ni stricktly kwa Wabara tu - hakuna! isipokuwa ktk serikali ya Zanzibar mbara haruhusiwi uongozi wa serikali hiyo lazima uwe Mzanzibar na kama utamwona Mbara huko Zanzibar basi kaletwa kusimamia yale ya Muungano. Kwa hiyo ni bara wasiokuwa na uhuru kamili sio Zanzibar ambayo tayari ina serikali mbili.

Ndio maana Mwanakijiji anasema hakuna sababu ya Wazanzibar kutushawishi sisi ili watoke ktk muungano huu maana sisi wenyewe tumesha choka ila hatuna jinsi. wafanye hiyo referendum hata kesho wafikie maamuzi yao kama walivyofanya wakati wa kuunda serikali ya mseto - na maamuzi hayo hayatapingwa hata kidogo tena ni ushahidi tosha kuufikisha UN au vyombo vya sheria vya kimataifa ktk kuweka madai yao.
 
Mnaonaje mkawashawishi viongozi wenu akina Bilal na wenzie wajiuzulu na warudi Zanzibar?
Kwa hilo natawatetea Wazanzibar kwa sababu walitambua mapema kwamba haiwezekani kuwatumia viongozi wao ku secede from the Union. Kiongozi kutoka Zanzibar kama Bilal hawezi, hathubutu kuchokonoa Muungano. Ana maslahi.

Jana kiongozi mmoja, Balozi Karume wa Italy, amefunguka kwamba Muungano hauvunjwi ng'oo, na kwamba yeye anataka agombee Urais. Now this dude Ally Karume yeye ndio Dean of Tanzanian Ambassadors, cheo ambacho amekipata kupitia Muungano, sitegemei huyu ukimwambia tujitoe kwenye Muungano atakubali, akale wapi? Anaota ndoto aje kuwa Rais wa Tanzania, sio kwao Zanzibar, huku Bara! Huyu humwambii kitu na Muungano. Vile vile wakina Billal, na Rais Mwinyi. Yalipochomwa makanisa serikali ilim-dispatch Mzee Mwinyi aende Zanzibar kutetea Muungano na kuwa-lambast UAMSHO, and he did a spectacular job, aliwaambia UAMSHO, "tumekutana wapi mkatuuliza kama hatutaki Muungano"? I was like, no kidding, Mzee Mwinyi ulikuwa Rais wa Zanzibar, umestaafu hutaki hata kuisogelea Zanzibar, uko kwenye executive residences Mikocheni next to presidential residences za kina Kikwete, Nyerere, Warioba, lakini una guts za kuwaambia waliokuwa stuck huko Zanzibar kwamba Muungano unawafaa, halafu ulipomaliza speech yako uka fly back to Mikocheni by night! Such unspeakable self-serving hubris!

Na wale viongozi wa Serikali ya Mapinduzi ambao hawafaidiki moja kwa moja na vyeo vya Muungano, wao wanajiona wana potential ya kuja Serikali kuu on any given Sunday, kwa sababu Mzanzibar - kwa sababu wako wachache - wana probability kubwa sana ya kupewa uongozi huku Muungano, especially kama una vi stashahada vya hapa na pale kidogo. Hawa nao huwezi kuwaambia kitu kuhusu Muungano. Wananchi wa Zanzibar walishajua hivyo, ndo maana hawawatumii.

Kiongozi wa Zanzibar na Mwananchi wa Zanzibar wote hawana uhuru wanaodai kutoka Tanzania, lakini tofauti yao ni ile aliyokuwa akiisema Malcolm X. Kiongozi mwenye ulaji ni kama mtumwa wa kazi za ndani, anafaidi makombo ya chakula cha master, anavalishwa midabwada ya nguo zilioanza kuwabana watoto wa master, yuko comfortable, japo mkewe ana repiwa na master humo humo ndani. Halafu Mwananchi wa kawaida ndio mtumwa wa nje, analala nje kwenye mabanda ya mbwa, anacharazwa mbakora kila uchwao, ana njaa na anakula kwa kujitegemea, basi anakuja anamshtua mtumwa wa ndani, ee bana eeh, tufanya mpango tujitoe, tutoroke hapa mahala, mtumwa wa ndani anamjibu kwa ukali, "TUTOROKE TWENDE WAPI?... WAPI KUNA MAISHA BORA KULIKO HAPA KWA MASTER KIKWETE?" Hajui kumbe yale maisha bora sio kwa kila mtwana.

Maalim Seif pamoja na Mzee Jumbe wananielewa. Wao walikuwa watwana wa ndani, siku moja wakajifanya kuleta chokochoko ya kudai uhuru ndani ya nyumba ya master Nyerere, wakatupwa pembeni wawe watwana wa nje, mpaka leo Jumbe kafungiwa kifungo cha nje kwenye kibanda cha mbwa Gezaulole huko. Maalim Seif ka-compromise principle kawasaliti wenzie karudishwa ndani ya nyumba, sasa ni mtwana wa ndani, ana enjoy makombo ya bwana wa watwana, hataki kusikia habari za kuvunja Muungano.
 
Hapa ndipo ambapo Mzee Mtei angesaidia kusema Tanganyika ilichangia asilimia ngapi ya mtaji wa kuanzisha BOT na Zanzibar walichangia ngapi. Hii ingepunguza/ingezima malalamiko ya tunawagawia au tunanyonywa.


Kwa kutaka maelezo kutoka kwangu, umekusudia kutania? Kuchekesha wanajf? Au umekusudia kupandisha mizuka ya walio "bendera hufuata upepo"?

Shirika La umeme ni shirika la kibiashara au shirika la kugawa sadaka?
Je shirika la Umeme,TANESCO linaendeshwa kibiashara au kisiasa?

Nijuavyo ni kuwa TANESCO wanafanya biashara na Shirika la Umeme Zanzibar. Hapo kuna mkataba wa kibiashara. Anaeshindwa kutimiza masharti ya mkataba, apate adhabu. Mteja/mlalahoi ambaye halipi umeme anakatiwa umeme.

Sasa kama TANESCO wanawapa sadaka Shirika la umeme Zanzibar. Huo ni udhaifu wa TANESCO.
Kama Tanganyika analipia gharama za umeme za Zanzibar inawezekana ndio kilainisho/hongo ya kuwafanya wazanzibari wakubali serikali moja.

Mimi ningesema kila mtu ababe msalaba wake! Tanganyika ilipie gharama zake, Zanzibar walipie gharama zao na pale penye mambo ya muungano ndio walipie kwa pamoja.

After all, there is no free lunch!


JokaKuu,
Hapo umeandika kuwa Zanzibar wameweka pesa zao BOT sasa wakitaka kulipa mishahara ya wafanyakazi wao inawapasa wachote kutoka hiyo akiba yao. Kama walilazimishwa kuweka akiba yao BOT na kuifanya PBZ isite kuwa benki ya serikali ya Zanzibar. Hizo pesa bila shaka zitatoka katika fedha zao zilizopo BOT au BOT wakiweka akiba ya mteja wake huwa hawarudishi pale mteja anapotaka sehemu ya akiba yake?

JokaKuu
Hapa ndio utaelewa kuwa sisi wabara(watanganyika) kuwa ni wadanganyika.
Bado hujaelewa kuwa hakuna hazina ya Tanganyika? Tanganyika haipo. Tanganyika haichangii chochote katika Muungano. Hazina ni ya muungano, serikali ya Muungano.
Wabara(wadanganyika) tunapata sadaka kutoka hazina ya muungano. kwa bahati ya werevu wa "wala urojo/mayakhe"
Wao wanapata kutoka hazina ya Zanzibar na hazina ya Muungano.

Kama tutaelewa somo la leo. maujanja ni kurejesha Tanganyika ,ili iwepo hazina ya Tanganyika, hazina ya Zanzibar na hazina ya muungano. Tumelikoroga sasa inabidi tulinywe tu, kaka!

Nafikiri baada ya Mwalimu kuona kosa lake alilolifanya juu ya kuua serikali ya Tanganyika, ndio aliamua afanye jitihada ya kuua serikali ya Zanzibar. Ndio ile janja ya serikali mbili kuelekea moja.

Lakini pia alijitengenezea njia nyengine kusema kuwa EAC ikizaliwa tena, ni vyema iundwe serikali ya Tanganyika na serikali ya Zanzibar iliyopo zijiunge EAC kama serikali zinazojitegemea. Hapa lilitokea G55 lililoanza kutoka usingizini na kuidai Tanganyika.

Tukiipata Tanganyika yetu na udanganyifu wa muungano tunaupatia dawa yake.

Je wadanganyika tutaendela kudanganyika au tutarudi Tanganyika?
JokaKuu
Hakuna serikali ya Tanganyika, in principle; serikali ya Muungano kama unavyosema wewe ni de-facto serikali ya Tanganyika lakini ukweli ni kuwa serikali ya Muungano ni monster tu, anatafuna Tanganyika, anatafuna Zanzibar.

Nonda,

..Unaposema Tanganyika haipo u r just being legalistic. Practically Tanganyika ipo.

..Kama Tanganyika haipo umeme mnaotumia bure huko Zanzibar unatoka wapi?

..Kwa kifupi Tanganyika tunabeba msalaba wetu na wa Zanzibar vilevile. Muungano huu unatunyonya.

..LET ZANZIBAR GO!!!
 
Kwa hilo natawatetea Wazanzibar kwa sababu walitambua mapema kwamba haiwezekani kuwatumia viongozi wao ku secede from the Union. Kiongozi kutoka Zanzibar kama Bilal hawezi, hathubutu kuchokonoa Muungano. Ana maslahi.

Jana kiongozi mmoja, Balozi Karume wa Italy, amefunguka kwamba Muungano hauvunjwi ng'oo, na kwamba yeye anataka agombee Urais. Now this dude Ally Karume yeye ndio Dean of Tanzanian Ambassadors, cheo ambacho amekipata kupitia Muungano, sitegemei huyu ukimwambia tujitoe kwenye Muungano atakubali, akale wapi? Anaota ndoto aje kuwa Rais wa Tanzania, sio kwao Zanzibar, huku Bara! Huyu humwambii kitu na Muungano. Vile vile wakina Billal, na Rais Mwinyi. Yalipochomwa makanisa serikali ilim-dispatch Mzee Mwinyi aende Zanzibar kutetea Muungano na kuwa-lambast UAMSHO, and he did a spectacular job, aliwaambia UAMSHO, "tumekutana wapi mkatuuliza kama hatutaki Muungano"? I was like, no kidding, Mzee Mwinyi ulikuwa Rais wa Zanzibar, umestaafu hutaki hata kuisogelea Zanzibar, uko kwenye executive residences Mikocheni next to presidential residences za kina Kikwete, Nyerere, Warioba, lakini una guts za kuwaambia waliokuwa stuck huko Zanzibar kwamba Muungano unawafaa, halafu ulipomaliza speech yako uka fly back to Mikocheni by night! Such unspeakable self-serving hubris!

Na wale viongozi wa Serikali ya Mapinduzi ambao hawafaidiki moja kwa moja na vyeo vya Muungano, wao wanajiona wana potential ya kuja Serikali kuu on any given Sunday, kwa sababu Mzanzibar - kwa sababu wako wachache - wana probability kubwa sana ya kupewa uongozi huku Muungano, especially kama una vi stashahada vya hapa na pale kidogo. Hawa nao huwezi kuwaambia kitu kuhusu Muungano. Wananchi wa Zanzibar walishajua hivyo, ndo maana hawawatumii.

Kiongozi wa Zanzibar na Mwananchi wa Zanzibar wote hawana uhuru wanaodai kutoka Tanzania, lakini tofauti yao ni ile aliyokuwa akiisema Malcolm X. Kiongozi mwenye ulaji ni kama mtumwa wa kazi za ndani, anafaidi makombo ya chakula cha master, anavalishwa midabwada ya nguo zilioanza kuwabana watoto wa master, yuko comfortable, japo mkewe ana repiwa na master humo humo ndani. Halafu Mwananchi wa kawaida ndio mtumwa wa nje, analala nje kwenye mabanda ya mbwa, anacharazwa mbakora kila uchwao, ana njaa na anakula kwa kujitegemea, basi anakuja anamshtua mtumwa wa ndani, ee bana eeh, tufanya mpango tujitoe, tutoroke hapa mahala, mtumwa wa ndani anamjibu kwa ukali, "TUTOROKE TWENDE WAPI?... WAPI KUNA MAISHA BORA KULIKO HAPA KWA MASTER KIKWETE?" Hajui kumbe yale maisha bora sio kwa kila mtwana.

Maalim Seif pamoja na Mzee Jumbe wananielewa. Wao walikuwa watwana wa ndani, siku moja wakajifanya kuleta chokochoko ya kudai uhuru ndani ya nyumba ya master Nyerere, wakatupwa pembeni wawe watwana wa nje, mpaka leo Jumbe kafungiwa kifungo cha nje kwenye kibanda cha mbwa Gezaulole huko. Maalim Seif ka-compromise principle kawasaliti wenzie karudishwa ndani ya nyumba, sasa ni mtwana wa ndani, ana enjoy makombo ya bwana wa watwana, hataki kusikia habari za kuvunja Muungano.
Taso, hivi kwani ulikuwa huyajui haya toka mwanzo? mimi nawaambia Wazanzibar toka zamani ya kwamba hakuna kiongozi hata mmoja ndani ya Baraza la Mapinduzi anaweza kuunga mkono wazo lolote la kuvunja muungano kwa sababu wanajua faida zake na wanavyolindwa japokuwa kazi yao imeisha malizika na Zanzibar ni salama.

Sasa kama kweli serikali ya mseto imeundwa kuwaunganisha Wazanzibar, huu ndio wakati muafaka kabisa kwa viongozi hao kuomba kuuvunja lakini wamejichimbia na kuwachochea hao UAMSHO ktk vijiwe na mihadhara lakini hathubutu hata mmoja wao kusimama na kusema tunataka kuuvunja Muungano.

Watu watabisha sana CUF kuhusika na UAMSHO lakini maajabu ni kwamba madai yote ya Seif Hamad yanafanana kikamilifu na madai ya UAMSHO na kwa bahati mbaya madai hayo hayo hayana support ya CUF bara.. Kama chama hiki kitakufa basi bila shaka kitakufa mkononi mwa Seif Hamad (kwa unafiki) maana ndiye aliyewaingiza mkenge CUF wakati walikuwa na uwezo mkubwa wa kushinda uchaguzi wa Zanzibar 2010, lakini akaingia muafaka hata kabla ya uchaguzi kwa kuahidiwa cheo (ananikumbusha Shamte na Sultan) akakubali kuchukua makamu wa rais, cheo ambacho hakina umuhimu wowote kwa wana CUF.
 
huko ndiko mnakoelekea na mambo ya al-qaida , hata wakati wa uchaguzi 2005 tuliambiwa kuna watu walikamatwa na visu eti ni al-qaida , mbinu hizo za polisi na usalama wa taifa zimeshapitwa na wakati

kila chenye kuzaliwa ni lazima kuna siku yake ya kufa ,

nyinyi na makanisa yenu endesheni propaganda lakini hamuwezi kuzuia kifo cha muungano siku yake ikifika

Hivi wewe unajua kusoma kweli??? Karibu wachangiaji wote hapa wanasema WAZANZIBARI TANGAZENI KUJITOA KWENYE MUUNGANO HATA LEO, lakini wewe umeshikilia kuwa tunaung'ang'ania muungano!!!!
 
Baru baru Salaam, Tafadhali sana naomba ufute hiyo quote ya pili (namba 5) post yako # 285. Hayo si maneno yangu na wala sijaandika na kama nimeandika hebu iweke hiyo post namba. Hujanitendea haki kunibambikizia maneno

Baada ya hapo nitaweza kuendelea na mjadala wa BoT n.k.

Ahlan wa sahalam Nguruvi3,

Awali ya yote naomba nikutake radhi sana kwa kuingiza hiyo quote katika bandiko langu wakti najibu hoja yako. Hakika hayo si makusudi yangu kutaka kupotosha au hata kukuvunjia haki zako ila ni bahti mbaya tu. Na nimeshaiondoa.

Hii quote chini ni maneno adhimu sana ya Tamko la Jumuiya za MWAMSHO Znz kwa Serikali yao na waZnz wote. Hii mimi niliipenda sana.
5. Kutumia fursa hii ya mchakato wa katiba mpya kuimarisha muungano wa kijamii na kuondoa dhulma ya muungano wa kiserikali ulioidhulumu nchi yetu kiunyama haki zake za kimataifa na hata za kitaifa na kufikia hadi kuifuta nchi yetu ya Zanzibar katika ramani ya dunia.

Kwa ikhsani yako endelea ...
 
Hivi wewe unajua kusoma kweli??? Karibu wachangiaji wote hapa wanasema WAZANZIBARI TANGAZENI KUJITOA KWENYE MUUNGANO HATA LEO, lakini wewe umeshikilia kuwa tunaung'ang'ania muungano!!!!

Kama wanaojua kusoma wanakuwa na masuala kama yako. Basi ni bora mtu asiende skuli na kubaki mbumbumbu kuliko kujua kusoma wakti usomi.

Nitakusaidia kidogo hapa.

Muungano wenu ni wa kimkataba na umefanywa na upande mmoja tu wa Muungano kwa maana Bunge la Muungano. Na mpaka sasa haujafikishwa kwenye baraza la wawakilishi kuuridhia.

sasa wenye mamlaka kisharia wa kuuvunja muungano huo ni Bunge la Muungano na sio BLW.

Huo ni mwanga tu lakin tumefafanua sana huko nyuma suala .

Kwni elimu ya ngumbaru huko Tz hususan tanganyika imefutwa siku hizi?

Pole sana

 
Taso, hivi kwani ulikuwa huyajui haya toka mwanzo? mimi nawaambia Wazanzibar toka zamani ya kwamba hakuna kiongozi hata mmoja ndani ya Baraza la Mapinduzi anaweza kuunga mkono wazo lolote la kuvunja muungano kwa sababu wanajua faida zake na wanavyolindwa japokuwa kazi yao imeisha malizika na Zanzibar ni salama.

Sasa kama kweli serikali ya mseto imeundwa kuwaunganisha Wazanzibar, huu ndio wakati muafaka kabisa kwa viongozi hao kuomba kuuvunja lakini wamejichimbia na kuwachochea hao UAMSHO ktk vijiwe na mihadhara lakini hathubutu hata mmoja wao kusimama na kusema tunataka kuuvunja Muungano.

Watu watabisha sana CUF kuhusika na UAMSHO lakini maajabu ni kwamba madai yote ya Seif Hamad yanafanana kikamilifu na madai ya UAMSHO na kwa bahati mbaya madai hayo hayo hayana support ya CUF bara.. Kama chama hiki kitakufa basi bila shaka kitakufa mkononi mwa Seif Hamad (kwa unafiki) maana ndiye aliyewaingiza mkenge CUF wakati walikuwa na uwezo mkubwa wa kushinda uchaguzi wa Zanzibar 2010, lakini akaingia muafaka hata kabla ya uchaguzi kwa kuahidiwa cheo (ananikumbusha Shamte na Sultan) akakubali kuchukua makamu wa rais, cheo ambacho hakina umuhimu wowote kwa wana CUF.

Taso,

Ahali yangu hapo nilipo BLUE.

Ninapenda kukufahamisha kuwa Znz ni wananchi na jamii yote na SIO VIONGOZI. Kumbuka viongozi ni wachaguliwa au wateuliwa tu wa kuwakilisha jamii na hawafiki hata 1% ya wazanzibari wote na wanatoka kwenye jamii hiyo.

Sasa unaposema viongozi wa Znz wanaukubali muungano ujue unasema watu chini ya 1% ndio wanaoukubali na kuulinda kwa nguvu zote na 99% hawautaki na wanaona machungu yake kutokana na dhulma wanayofanyiwa.

na hapo ndipo wana UAMSHO wanapo waamsha waZnz kuhusu hilo. Hebu soma Tamko lao hili hususan no 5.
5. Kutumia fursa hii ya mchakato wa katiba mpya kuimarisha muungano wa kijamii na kuondoa dhulma ya muungano wa kiserikali ulioidhulumu nchi yetu kiunyama haki zake za kimataifa na hata za kitaifa na kufikia hadi kuifuta nchi yetu ya Zanzibar katika ramani ya dunia.
 
Hii ina maana gani hasa "Muungano wa Kijamii"?

Hapa wanamaanisha kuwa kuna watu kutoka tanganyika wameoa au kuolewa kule Znz na kuna watu kutoka Znz wameoa au kuolewa Tanganyika.Na vile vile kuna watu maswahiba kutoka pande hizo. Hapo kuna kuwa na muungano wa kiudugu ambao hauwezi vunjika hata kama nchi hizo zitatengana. Huo ndio unaitwa Muungano wa kijamii na sio muungano wa nchi.
 
Hapa wanamaanisha kuwa kuna watu kutoka tanganyika wameoa au kuolewa kule Znz na kuna watu kutoka Znz wameoa au kuolewa Tanganyika.Na vile vile kuna watu maswahiba kutoka pande hizo. Hapo kuna kuwa na muungano wa kiudugu ambao hauwezi vunjika hata kama nchi hizo zitatengana. Huo ndio unaitwa Muungano wa kijamii na sio muungano wa nchi.

Kwa hiyo hawa wenye muungano wa kijamii wakiamua kuunganisha nchi ni mwiko? lakini wenyewe muungano wao udumu tu. This sounds silly... muungano gani huo wa kijamii ambapo upande mmoja unawaona kwa dharau watu wa upande mwingine?
 
Kwa hiyo hawa wenye muungano wa kijamii wakiamua kuunganisha nchi ni mwiko? lakini wenyewe muungano wao udumu tu. This sounds silly... muungano gani huo wa kijamii ambapo upande mmoja unawaona kwa dharau watu wa upande mwingine?

Kinachotazamwa hapa ni uchumi zaidi na sio maslahi binafsi. Udugu ni kitu binafsi lakin nchi ni maslahi ya jamii. Kwa mtazamo huo Muungano wa Kijamii ni wa kidugu zaidi na unajengwa na damu lakin muungano wa Nchi ni kama koti likichosha unalivua.

Hata mimi binafsi nina ndugu zangu Znz na hata Tanganyika tena wa damu sana. Kuwa Mu Oman hakunizuilii mimi kuja huko au wao kuja huku na kutusabahi mradi tu wafuate taratibu za uamiaji.

WaZnz wanasisi tiza wanataka muungano wa Kijamii na kuuimarisha zaidi na zaidi.
 
Kama wanaojua kusoma wanakuwa na masuala kama yako. Basi ni bora mtu asiende skuli na kubaki mbumbumbu kuliko kujua kusoma wakti usomi.

Nitakusaidia kidogo hapa.

Muungano wenu ni wa kimkataba na umefanywa na upande mmoja tu wa Muungano kwa maana Bunge la Muungano. Na mpaka sasa haujafikishwa kwenye baraza la wawakilishi kuuridhia.

sasa wenye mamlaka kisharia wa kuuvunja muungano huo ni Bunge la Muungano na sio BLW.

Huo ni mwanga tu lakin tumefafanua sana huko nyuma suala .

Kwni elimu ya ngumbaru huko Tz hususan tanganyika imefutwa siku hizi?

Pole sana


Barubaru, kama kuelimika ni kujipinga mwenyewe (au kuwa na selective amnesia) mimi nitaikataa "elimu" ya namna hiyo any day! Kama jukumu la kuvunja muungano ni la Tanganyika kisheria, iweje baraza la wawakilishi litunge sheria zinazopingana na katiba ya JMT bila kibali wala kuishirikisha serikali ya muungano? USSR si ulikuwa muungano? Yeltsin aliomba kibali kwa Gorbachev Russia kujitoa kwenye USSR? Ukraine walipewa kibali na nani? Czech Republic na Slovenia zimetokeaje? Ina maana "usomi" wako umekufanya uamini kuwa mkataba - na tunaambiwa mkataba wenyewe haukuwa ratified na upande usioridhika nao - hauwezi kuvunjwa?

Aaah Barubaru, acha hizo bana!
 
Hapa wanamaanisha kuwa kuna watu kutoka tanganyika wameoa au kuolewa kule Znz na kuna watu kutoka Znz wameoa au kuolewa Tanganyika.Na vile vile kuna watu maswahiba kutoka pande hizo. Hapo kuna kuwa na muungano wa kiudugu ambao hauwezi vunjika hata kama nchi hizo zitatengana. Huo ndio unaitwa Muungano wa kijamii na sio muungano wa nchi.

Kwa mantiki hiyo kuna "miungano" lukuki inayoihusu Tanganyika maana Watanganyika lukuki wameoa/wameolewa na watu kutoka karibu kila kona ya dunia. Kwa hiyo hilo nalo ni la kujadili kisheria?
 
Barubaru, kama kuelimika ni kujipinga mwenyewe (au kuwa na selective amnesia) mimi nitaikataa "elimu" ya namna hiyo any day! Kama jukumu la kuvunja muungano ni la Tanganyika kisheria, iweje baraza la wawakilishi litunge sheria zinazopingana na katiba ya JMT bila kibali wala kuishirikisha serikali ya muungano? USSR si ulikuwa muungano? Yeltsin aliomba kibali kwa Gorbachev Russia kujitoa kwenye USSR? Ukraine walipewa kibali na nani? Czech Republic na Slovenia zimetokeaje? Ina maana "usomi" wako umekufanya uamini kuwa mkataba - na tunaambiwa mkataba wenyewe haukuwa ratified na upande usioridhika nao - hauwezi kuvunjwa?

Aaah Barubaru, acha hizo bana!

Mtoboasiri

Kumbuka kuwa Muungano wa USSR ni tofauti sana na Muungano wenu wa Tanzania.
Muungano wa USSR ni muungano wa KIKATIBA na muungano wa Tanzania ni muungano wa MKATABA.

Tanzania mliungana kwa mambo 11 na sasa yapo 22 tu. mengine yote kila mtu na lake.

Nilitaka kukumbusha hilo kwani ulikuwa unajaribu kulinganisha faida za mbingu na ardhwi.

 
Mtoboasiri

Kumbuka kuwa Muungano wa USSR ni tofauti sana na Muungano wenu wa Tanzania.
Muungano wa USSR ni muungano wa KIKATIBA na muungano wa Tanzania ni muungano wa MKATABA.

Tanzania mliungana kwa mambo 11 na sasa yapo 22 tu. mengine yote kila mtu na lake.

Nilitaka kukumbusha hilo kwani ulikuwa unajaribu kulinganisha faida za mbingu na ardhwi.


Acha kuruka viunzi, jibu hoja. Sasa huo mkataba hauwezi kuvunjwa kama kuna upande hauridhiki nao? Na tuseme muungano wa mkataba hauna katiba (au kukiwa na katiba hakuna mkataba)?
 
Acha kuruka viunzi, jibu hoja. Sasa huo mkataba hauwezi kuvunjwa kama kuna upande hauridhiki nao? Na tuseme muungano wa mkataba hauna katiba (au kukiwa na katiba hakuna mkataba)?

Mtoboasiri.

Nafikiri hili nimelirudia sana sana kuwa masuala yote yanayokhusu muungano yapo kwenye afisi ya makamo wa raisi kwenye Muungano na sio SMZ.

Vile vile Bunge lililoketi kama Bunge la Katiba kupitisha katiba yenu ya Muungano ni Bunge la Muungano SIO BLW. Kwa taarifa yako mpaka leo hiyo hati ya makubaliano ya mkataba wenu wa Muungano bado kuridhiwa na BLW

Kwa mantiki hiyo mwenye mamlaka kisharia kuhoji au kuujadili Muungano wenu ni Bunge la Muungano na sio BLW.

Nafikiri unakumbuka enzi za G57 wabunge waliodai Serikali ya Tanganyika Bungeni muungano. hao wabunge wa Muungano ndio wenye mamlaka kisharia kuujadili Mvungano wenu.

Vile vile kwa kuwa mumeungana KIMKATABA ndio maana kila upande una KATIBA yake. Ila ya JMTz kwa Muungano Tzna ile ya SMZnz kwa nchi ya Znz.

Nafikiri nimekidhi haja ya masuala yako. kama una ziada basi Bismillah

 
Mtoboasiri.

Nafikiri hili nimelirudia sana sana kuwa masuala yote yanayokhusu muungano yapo kwenye afisi ya makamo wa raisi kwenye Muungano na sio SMZ.

Vile vile Bunge lililoketi kama Bunge la Katiba kupitisha katiba yenu ya Muungano ni Bunge la Muungano SIO BLW. Kwa taarifa yako mpaka leo hiyo hati ya makubaliano ya mkataba wenu wa Muungano bado kuridhiwa na BLW

Kwa mantiki hiyo mwenye mamlaka kisharia kuhoji au kuujadili Muungano wenu ni Bunge la Muungano na sio BLW.

Nafikiri unakumbuka enzi za G57 wabunge waliodai Serikali ya Tanganyika Bungeni muungano. hao wabunge wa Muungano ndio wenye mamlaka kisharia kuujadili Mvungano wenu.

Nafikiri nimekidhi haja ya masuala yako. kama una ziada basi Bismillah


Barubaru, nakiri kuwa umerudia rudia sana maneno yale yale isipokuwa hujajibu swali la msingi (na ndio hoja ya Mzee Mwanakijiji): iweje BLW liweze kutunga sheria zinazovunja katiba ya JMT lakini lishindwe kujitoa kwenye muungano? Kama Wanzibari hawaridhiki na muungano wanashindwa nini kujitoa ukitilia maanani kuwa muungano wenyewe hauna nguvu ya kisheria (kwa mujibu wa madai kuwa the union articles were never ratified by any competent authority in Zanzibar)?

Na hata mkataba wa muungano ungekuwa halali kisheria, ina maana hauwezi kuvunjwa? Mkataba unatakiwa ama kubadilishwa au kuvunjwa endapo kuna upande usioridhika iwe na kipengele kimoja au zaidi ndani ya mkataba, na initiator ni yule asieridhika!
 
Kinachotazamwa hapa ni uchumi zaidi na sio maslahi binafsi. Udugu ni kitu binafsi lakin nchi ni maslahi ya jamii. Kwa mtazamo huo Muungano wa Kijamii ni wa kidugu zaidi na unajengwa na damu lakin muungano wa Nchi ni kama koti likichosha unalivua.
Hata mimi binafsi nina ndugu zangu Znz na hata Tanganyika tena wa damu sana. Kuwa Mu Oman hakunizuilii mimi kuja huko au wao kuja huku na kutusabahi mradi tu wafuate taratibu za uamiaji.
WaZnz wanasisi tiza wanataka muungano wa Kijamii na kuuimarisha zaidi na zaidi.
Kwa mantiki hiyo hakuna kitu muungano wa kijamii kwasababu hakuna anyekatazwa kuwa na mahusiano na Mnigeria, Mfilipino au Mkorea kama usivyozuiliwa kuwa na mahusiano na Tanganyika au Zanzibar.

Kwanini tusivunje tu muungano tukabaki na muungano wa kijamii kama tulio nao na Wakenya, Warundi, Wanyarwanda n.k
Kwanini Tanganyika na Zanzibar ziwe na muungano wa kijamii tofauti na majirani wengine.
Mtoboasiri
Kumbuka kuwa Muungano wa USSR ni tofauti sana na Muungano wenu wa Tanzania.
Muungano wa USSR ni muungano wa KIKATIBA na muungano wa Tanzania ni muungano wa MKATABA.

Tanzania mliungana kwa mambo 11 na sasa yapo 22 tu. mengine yote kila mtu na lake.
Nilitaka kukumbusha hilo kwani ulikuwa unajaribu kulinganisha faida za mbingu na ardhwi

Katika mambo 11 yaliyoongezwa kufikia 22 ni lipi au yapi unadhani yameongezwa na yanaiumiza Zanzibar.
Nina maana ni yapi ya hila za kuihujumu Zanzibar

Pili, suala la elimu ya juu ni miongoni mwa yale 11 yaliyoongezwa sasa nani anafaidika na hayo ni Zanzibar au Tanganyika
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom