KijanaHuru
JF-Expert Member
- Jan 7, 2017
- 1,822
- 2,290
Ndugu Mtukutu wa Nyaigela mimi pia ni Mkristo naomba nikuongeze hoja hapa nanukuuBiblia iliandikwa na watu waiovuviwa roho mtakatifu. Hivyo kuielewa inahitaji uwezo wako + uwezo wa roho mtakatifu. Hivyo omba kwa Mungu kabla ya kuanza kusoma. Na kama maarifa yoyote yalivyo upate mtu mjuzi akupe msaada.Ndivyo ninavyojua
"Biblia iliandikwa na watu waiovuviwa roho mtakatifu. Hivyo kuielewa inahitaji uwezo wako + uwezo wa roho mtakatifu...''
Inamaana hujui kama kuna vitabu vingine viliandikwa kama unavyoandika diary vile? mfano ukisoma injili ya Luka,Mathayo na Marko hawa waliandika maisha ya kila siku ama matukio ya kila siku ambayo walikuwa wanashuhudia na kuona kuhusu Yesu ndio maana kuna baadhi ya maeneo unakuta huyu kaweka huyu hajaweka so
mambo Mengine kuyaelewa usisingizie Roho mtakatifu tu bali tunapaswa kusoma na kuelewa na kufundishwa kama masomo mengine yalivyo ndio maana tulisoma Bible Knowledge na Divinity