Leo Tarehe 10 Desemba, ni siku ya Uhuru wa Zanzibar

Gavana

JF-Expert Member
Jul 19, 2008
33,233
8,779
Leo ni siku ya uhuru wa Jamhuri ya watu wa Zanzibar. Tunawapongeza wale waliochukuwa juhudi za kuitoa hii nchi chini ya makucha ya wakoloni wa kiengereza , kwa njia za amani na kistaarabu.

Tunawaombea Wazanzibar wote mafanikio katika juhudi zao za kuitoa tena Zanzibar katika makucha ya mkoloni mweusi kutoka Tanganyika

Mungu ibariki Zanzibar na Wazanzibari, Aaamin.

1575981675718.png








======

Katika sehemu hizi za Afrika Mashariki na kati dola ambayo ilitambulikana katika miaka ya karne ya 19 ni Zanzibar. Hapa Zanzibar palikuwa na Mabalozi wa nachi mbali mbali Wakiziwakilisha nchi zao.

Hii Zanzibar ilikuwa ni Dola kabla ya Tanganyika, Kenya, Uganda na katika nchi nyingine Afrika ya Mashariki na ya kati. Huo ndio utukufu wa Zanzibar.

Katika miaka ya 1880 na 1885, Wakoloni walianza kuingia sehemu hizi... Wakaamua kugawana Afrika. Katika mkutano uliofanyika Berlin 1885 wakamnyang'anya mtawala wa Zanzibar sehemu yote ya Afrika. Zanzibar wakaachiwa visiwa pamoja na Mwambao wa maili kumi kwenda ndani.

Kuanzia kaskazini mwa Kenya mpaka kusini ya Tanganyika. Ilikuwa yote hayo ni mamlaka ya Zanzibar. Wajerumani wakaamua kuununua ule mwambao wa maili kumi wa Tanganyika. Kenya Wajerumani hawakuinunua, mwambao wa Kenya ulibaki sehemu ya Zanzibar, Lamu ilikuwa sehemu ya Zanzibar mpaka mwaka 1963, Kenya ilipopata Uhuru wakakubaliana waache. Tukabaki na Unguja na Pemba kama nchi.

Katika miaka ya 1950, 56, 57, Wazanzibari wakaunda vyama vya siasa, kumwondoa mkoloni.

Tukawa na Afro - Shirazi Party, Zanzibar Nationalist Party au Hizbu, Zanzibar and Pemba People's Party (ZPPP), tukawa na Umma Party.

Hivi ni vyama vilivyotafautiana kwa sera, kwa itikadi, lakini vyote vilishirikiana kumuondoa mkoloni Zanzibar.

Zanzibar ikapata uhuru tarehe 10/12/1963. Hapo Muingereza akaondoka. Alipoondoka Muingereza, Mkuu wa nchi akawa Sultani.

Zanzibar na Kenya zikajiunga na Umoja wa Mataifa kama wanachama kamili 13/12/1963 na bendera ya Zanzibar ilipanda katika Umoja wa Mataifa kama nchi nyingine.

12/1/1964 tukapinduana. Afro-Shiraz Party wakafanya mapinduzi, wakaipindua serikali ya Sultan, na Sultan akakimbia nchi.

Sasa, baada ya hapo ikaundwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar ... ilikuwa ni serikali kamili, ni dola yake ya Wazanzibari. Tukawa na wimbo wetu wa Taifa. Tukawana Rais wetu Zanzibar.

Credit: Hotuba ya Maalim Seif Kibanda Maiti
 
Mbona Mapinduzi ya Zanzibar ni January 12?

Hizo habari zako umezitoa wapi

Zanzibar ilikuwa huru baada ya mapinduzi ya Zanzibar
Kabla ya hapo ilikuwa chini ya mwarabu kwa maamuzi ya kiserkali japo kuwa Mohamed shamte alisimama kama figure ya uongozi wa kiserikali akiwa Waziri Mkuu wa Zanzibar

Hii ni kutokana na vuguvugu la Chini kwa chini Ndani ya Zanzibar hasa wale ambao hawakuwa machotara kulalamikia utawala wa mwarabu Au sultan

Ndio maana chama cha ASP ambacho kwa kiasi kikubwa kilikuwa kinaundwa na Wazanzibar weusi hawakuwa tayari kushirikiana na vyama vilivyokuwa na mrengo wa kisultan kuunda Serkali viligoma kabisa

Ndio maana baada ya mapinduzi vyombo vikubwa duniani vilitipoti habari za mapinduzi ya Zanzibar

Hii ni gazeti la The newyork times likiripoti kuangushwa kwa utawala wa kiarabu Zanzibar

Overtturns arab regime in Zanzibar
 
Historia toka Maktaba : Pilikapilika za Zanzibar kusheherekea Uhuru wa Zanzibar toka kwa Waingereza (10 December 1963)



(10 Dec 1963) Scenes in Zanzibar about time when it gained independence from Great Britain

Source: AP Archive
 
Historia ya Zanzibar uhuru toka kwa Mwingereza

Zanzibar ilipata uhuru wake tarehe 10 Desemba 1963. Uhuru wa usultani ukadumu muda mdogo tu. Mapinduzi ya tarehe 12 Januari 1964 yakamuondoa Sultani. Mauaji ya familia nyingi zenye asili ya Kiarabu yakafuata. Tarehe 26 Aprili 1964 Zanzibar ikaunganika na Tanganyika kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Global TV Online iko visiwani Zanzibar na imetembelea ndani ya jumba la kifahari (Kasri) iliyoishi familia ya Sulatani Sayyid Said kuanzia mwaka 1856 - 1964 ulipoondolewa utawala wa kisultani visiwani Zanzibar.



Source: Global TV online
 
Historia ya Taifa la Zanzibar

Zanzibar Kubwa kabla ya Mkutano wa Berlin 1884 iliyokuwa na himaya kubwa mpaka maeneo ya ndani ndani kabisa ya DR Congo ya Mashariki



Surce:BinMazrouy OnlinevTV
 
bagamoyo,
Unafanya makosa . Iliyopinduliwa si serikali ya mfalme. Mfalme hakuwa na serikali. Hakukuwa na mapinduzi ,kulikuwa na uvamizi. Nyerere aliivamia Zanzibar tarehe 12 Januari 1964 na kumkamata Waziri Mkuu Muhammed Shamte aliyechaguliwa kwa kura na wananchi na kumfunga kwenye jela za Tanganyika kabla huo uliopewa jina la muungano haujafanywa hapo April 26 ,1964.
Shamte Januari 1964 tayari ,keshafungwa bila kufikishwa mahakamani ,Tanganyika
 
Uchaguzi Zanzibar 1961

Zanzibar Elections (1961)



Various shots, including CUs. of the Vice-President of the Zanzibar and Pemba People's Party, Mr. Ameri Tajo, with Aba Leil Mbwana another candidate of the a party (in cap and suit) and some followers of the party outside their H.Q. CU. The emblem of the Zanzibar Nationalist Party, a cockerel stencilled on the wall outside the Party's H.Q.

Various shots of Mr. Abeid Amani Karume, the President of the Afro Shirazi Party, addressing his followers at the last political meeting before the actual elections at Mpakani, pan on to women supporters raising right hands and shouting "Uhuru" (freedom). CUs. of Mr. Abeid Amani Karume, pan to women supporters shouting "Uhuru". MSs. CU. Arabs waiting to cast their votes outside the Malindi Polling station.
Surce: British Pathe
 
Mbona Mapinduzi ya Zanzibar ni January 24?

Hizo habari zako umezitoa wapi
Ukweli mchungu ndio huo. Uhuru wa zanzibar ulipatikana kwa kupigwa kura. Kama Tanganyika ilipopata Uhuru na Nyerere kuwa Waziri Mkuu wa Kwanza lakini chini ya British Monarch kabla ya Uhuru kamili 9 Dec 1962 katiba ilipobadilishwa na Nyerere kuwa Rais kamili. Zanzibar pia ilikuwa hivyo huru chini ya utawala wa sultan.

Hivyo uhuru walipata 10 dec 1963 ... Na January 12 ndio yakafanyika mapinduzi ambayo ndio yanalazimishwa kuwa ndio Uhuru wao. Jiulize kwa nini Tanganyika ilipata uhuru 1961 na Nyerere akiwa waziri mkuu utawala ulibaki kwa malkia mpaka 9 dec 1962 kwa nini hatusemi uhuru wetu Tanganyika ni 1962 tunasema 1961? Halafu tulazimishe Zanzibar ni 1964 bad ala ya 1963!!?
 
Back
Top Bottom